Je! unajua kuwa wewe ni kazi ya sanaa?
Mwanadamu ndiye zao kuu la Mungu.
Ninamaanisha, mtu aliyeundwa kufikiria,
kuzungumza na kutenda pamoja na Mungu.
Je, unaishi sambamba na Mungu?
Je, hali yako ikoje mbele za Mungu leo?
Bila neema ya Roho Mtakatifu inayokaa ndani yake,
mwanadamu ni kivuli tu cha yule aliyeumbwa na Mungu!
Mwanadamu ambaye Mungu alimuumba
hakuwa mtu wa kimwili tu
anayetawaliwa na hisi zake
bali ni mjumbe kati ya ulimwengu
unaoonekana na usioonekana.
Mungu na mwanadamu walikuwa wakizungumza
pamoja kama marafiki.
Lakini siku moja, mwanadamu
alivunja uhusiano kwa kutokutii
na akaenda mbali na Mungu.
Kisha akaenda mbali zaidi hadi,
mwishowe akaondoka nyumbani.
Aliiacha nchi yake ya asili, Edeni,
ambako aliishi na Mungu.
Alihama kutoka kwenye uwepo wa Mungu.
Tangu wakati huo, Mungu amekuwa
na shauku ya kuweza
kuzungumza tena
na rafiki yake wa zamani
lakini mwanadamu,
kwa kuondoka katika uwepo wa Muumba wake,
alipoteza lugha yake mama.
Namaanisha, alipoteza lugha yake
ya asili na Mungu.
Na akawa hawezi kuwasiliana na
Muumba wake katika roho na kweli.
Mwanadamu wa kawaida hawezi kusikia
au kuzungumza na Mungu;
hii ndiyo changamoto tunayokabiliana
nayo leo.
Ingawa Mungu huzungumza tena na tena,
wengi sana hawapo makini kusikia
kile Anachosema (Ayubu 33:14).
Ukimya ni mgumu kwa Mungu.
Kama vile baba wa mwana mpotevu
alivyokuwa na shauku ya kumwona
mwanawe akirudi nyumbani,
Mungu ana shauku ya kuwa na uhusiano
wa karibu tena na mwanadamu,
Rafiki yake wa zamani.
Ndiyo maana ilimbidi achague lugha
ambayo mwanadamu angeelewa.
Kwa hivyo alimtuma Mwanawe,
Yesu Kristo duniani kumrudisha mwanadamu,
Rafiki Yake wa zamani, arudi Kwake tena.
Mungu aliheshimu lugha ya mwanadamu
kwa kumwita Yesu Neno.
Neno alifanyika mwili na akaingia
ulimwenguni.
Yesu ni Mungu akijieleza Mwenyewe
kwa lugha ambayo mwanadamu
anaweza kuelewa,
lugha ya roho na uzima (Yohana 6:63).
Je, ni kwa muda gani tutaendelea kuwaza,
kuzungumza na kuishi katika hali
ya kimwili
ilihali Yesu anakungoja katika mahala
pa Roho Wake?
Ni wasaa wa kurudi tena katika chuo
cha Mungu
Na kuanza kumtafuta Roho.
Kutoka kwenye miaka mingi ya kujifunza
chini ya, na kutembea
pamoja na Jenerali wa Mungu, Nabii
TB Joshua,
hadi alipoitwa Nyumbani Mbinguni,
shauku imewasha mioyoni mwetu
kutoa hazina tuliyopewa na Mungu;
Neno lililo hai katika nguvu za
Roho Mtakatifu!
Maandishi ya Neno hayawezi kusonga,
haiwezi kufanya kazi bila
uhai wa Mungu (Yohana 6:63).
Kila Neno la Mungu ni Roho na uzima.
Na ni uzima halisi wa Mungu
katika Neno hilo unaotia nguvu,
nishati katika Neno.
Hili ndilo Neno linaloponya, kuokoa,
kukomboa
na kumwezesha mwamini kuishi maisha
ya ushindi katika Kristo.
Kama vile Simoni Petro katika Yohana 6:68,
tumegundua kwamba hakuna mbadala wa Yesu
kwa sababu Yeye peke yake ndiye mwenye
Maneno ya uzima wa milele.
Baada ya mshauri wetu kuitwa Nyumbani
tarehe 5 Juni 2021,
kama wanafunzi wa zamani,
Yesu alipopaa Mbinguni,
tumekuwa tukingoja katika imani.
Na katika tarehe 8 ya Desemba 2021,
nilipokea ufunuo toka kwa Mungu.
Na nikapewa jina la
'Chuo Kikuu Cha Mungu'.
[muziki]
Nilijikuata katika chumba cha glasi
ndani ya pango
lisilokuwa na sehemu ya kutokea
Ghafla mwamba wenye nguvu ukaja
kutoka Mbinguni
na kugonga mlima wa mawe.
ulitoboa lile pango.
Mlima ulitikisika, lakini nilibaki
thabiti ndani ya chumba cha kioo.
Jiwe lilitoboa kwenye mlima wa mawe.
Niliangalia.
Kisha nikatoka na kutembea.
Nilisimama na kushtuka pale nilipoona
mwamba ulikuwa umechimba handaki zuri kabisa
iliyotengenezwa kwa dhahabu!
Nilijiambia, lazima kuwe na maji
mwishoni mwa handaki hili.
Nilianza kutembea.
Ghafla sauti ikasikika kutoka juu:
“Baki hapo ulipo. Usiingie!
Maji yanakujia.”
Nilisimama na kubaki pale nilipokuwa.
Niliposimama tuli, ghafla niliona maji
yakitiririka kutoka mwishoni mwa handaki
kuelekea kwangu.
Maji yalikuwa safi, yakimeta kwa uhai.
Yalitiririka karibu zaidi
mpaka yakafika kwenye vidole vyangu
na kunawisha miguu yangu kama wimbi
kwenye ufuo wa bahari.
Nilipokuwa nikitafakari juu ya ono hilo,
moyo wangu ulinisukuma kwenye
Kitabu cha Danieli 2:44. Nitasoma;
Na katika siku za wafalme hao Mungu
wa mbinguni atausimamisha ufalme
ambao hautaangamizwa milele, wala watu
wengine hawataachiwa enzi yake;
bali utavunja falme hizi zote
vipande vipande na kuzikomesha,
nao utasimama milele na milele.
Hii ndiyo maana ya maono ya mwamba
uliochongwa kutoka mlimani,
lakini si kwa mikono ya binadamu
— mwamba uliovunja
chuma, shaba, udongo, fedha na dhahabu
vipande vipande.
Kusudi la mwamba ni nini?
Kama inavyosema katika kitabu cha
Yeremia 1:10, nitasoma;
angalia, nimekuweka leo juu ya mataifa
na juu ya falme, ili kung'oa, na kubomoa,
na kuharibu, na kuangamiza;
ili kujenga na kupanda.
Kusudi la mwamba ni kuondoa kizuizi kati ya
moyo wetu na Mungu.
Wakati mtu anapokabidhi moyo wake kwa
Roho Mtakatifu, pazia huondolewa.
Neno la Mungu ni mbegu ya uzima wa kiungu
ambayo huja ndani ya mioyo yetu
na kusababisha imani kukua.
Maono hayo ni ya wakati uliowekwa (Habakuki 2:3).
Maono ni kuunganisha mwanadamu na Mungu
kupitia Neno Lake, kwa Roho Wake,
ili kuujenga Mwili wa Kristo.
na kushirikiana na mtandao wa makanisa
kote ulimwenguni.
Maono hayo yanaendana na wito na
zawadi ya Mungu katika maisha yetu.
Mwamba ulioanguka kutoka Mbinguni
ni Neno la Ufalme
kama Yesu alivyosema katika Mathayo 13:19.
Maono yetu ni kusaidia kuingiza Neno
katika mioyo ya watu -
kwa sababu ni pale tu ndipo linafanya kazi
kwa ufanisi.
Katika miongo miwili iliyopita chini ya ushauri
wa Nabii TB Joshua,
mwingiliano wetu na maelfu ya waumini na
viongozi wa kanisa ulimwenguni kote
na maswali ya mara kwa mara yaliyoulizwa
na wengi wakati wa mihadhara
yamevuta mtazamo wetu kwa upande
wa vitendo wa Ukristo,
Namaanisha, matembezi yetu
ya kila siku na Roho Mtakatifu:
jinsi ya kukuza ufahamu wa kiroho,
jinsi ya kusikia kutoka kwa Mungu,
jinsi ya kujenga imani ya mtu katika
uso wa kutokuwa na uhakika wa maisha.
Masuala haya ya msingi na mengine
yatashughulikiwa
chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu
kupitia vipindi vya ufundishaji wa kina
na muda wa maswali shirikishi na majibu.
Maono yetu pia yanakumbatia
makanisa ya mtaa.
Tunataka kushirikiana na mtandao wa
huduma ili kutoa ujuzi wetu, uzoefu,
na karama za kiroho kama Roho anavyoongoza.
Hadi kanisa la leo linatambua kwamba
roho ya mwanadamu ni chemchemi ya imani,
hapo ndipo Roho Mtakatifu atakapohusika
katika mambo yetu.
Kama mshauri wetu, Nabii TB Joshua
alitufundisha,
“Katika Chuo Kikuu cha Mungu, hata uwe
na kipaji gani, hutapewa vyeo maradufu,
lazima usome kila kozi kwa
kila kozi ina kusudi lake.”
Kwa hiyo, unahitaji nini?
Moyo wazi.
Ni nyenzo gani zinazohitajika kuchukua
kila kozi - kutokukata tamaa,
kutafuta njia mbadala au kukata tamaa kwa
vipigo vya kikatili vya maisha mara nyingi?
Unyenyekevu, imani, saburi, saburi,
msamaha na upendo bila kutarajia.
Nani anaashiria kazi yetu?
Roho Mtakatifu.