0:00:00.000,0:00:09.040 Mahali pa kwanza unapaswa kufanikiwa ni maisha yako ya kiroho, 0:00:09.040,0:00:16.680 kwa sababu maisha yako ya kiroho ndio injini inayobeba mafanikio yako. 0:00:16.680,0:00:22.320 Ukifanikiwa kifedha bila kufanikiwa kiroho, 0:00:22.320,0:00:27.680 ni kama kumiliki gari zuri lisilo na injini. 0:00:27.680,0:00:33.520 Inaweza kuonekana nzuri, lakini haina thamani kwa sababu haiwezi kwenda popote. 0:00:33.520,0:00:36.400 Thamani yake halisi imepotea. 0:00:36.400,0:00:38.960 Kusudi lake la kweli halipo. 0:00:38.960,0:00:42.600 Imekuwa gwaride la mtindo tu. 0:00:42.600,0:00:48.600 Hivi ndivyo alivyo mtu ambaye anafanikiwa kifedha bila kufanikiwa kiroho. 0:00:48.600,0:00:50.640 Unaweza kuwaona wakiwa na pesa. 0:00:50.640,0:00:54.120 Wana pesa lakini bado wana maswali ambayo hayajajibiwa maishani mwao. 0:00:54.120,0:00:58.120 Wana mali, lakini bado wanalalamikia wasichonacho. 0:00:58.120,0:01:02.600 Kwa faragha, wakati taa zimezimwa na hakuna mtu anayeangalia, 0:01:02.600,0:01:07.680 wanalilia wasichonacho. 0:01:07.680,0:01:11.760 Na kutembeza gari lao bila injini. 0:01:11.760,0:01:14.280 Ninasemaje, ndugu? 0:01:14.280,0:01:31.040 “Itamfaa nini mtu kuupata ulimwengu wote na kupoteza nafsi yake? 0:01:31.040,0:01:39.560 Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?” 0:01:39.560,0:01:50.280 Usichafue mikono yako kwa ajili ya kitu ambacho hakiwezi kukuhakikishia umilele. 0:01:50.280,0:02:00.840 Usichafue moyo wako kwa ajili ya mtu ambaye hashikilii hatima yako. 0:02:00.840,0:02:05.880 Ikiwa mikono yako imejaa pesa, kichwa chako kimejaa taarifa 0:02:05.880,0:02:11.480 lakini moyo wako ni mtupu, basi maisha yako ni tupu.