Baraka mara nyingi huambatana na vita.
Ni vita gani kwa mwili huu vinaweza kuwa na manufaa kwa roho yako.
Kile ambacho ni kigumu kwa mwili mara nyingi ni msaada kwa roho yako.
Ikiwa unamtumikia Mungu kwa namna iliyo rahisi tu kwako, basi huduma yako itakosa kujitolea.
Sisemi hakutakuwa na kujitolea kokote.
Kunaweza kuwa na kujitolea kwa sehemu, sio kujitolea kamili.
Unajua tatizo hapa?
Ikiwa kujitolea kwako kwa Mungu ni kwa sehemu -
unamtumikia Mungu kwa namna iliyo rahisi wako tu -
na unakabiliwa na hali ambapo imani yako katika Kristo inapingana
na imani ya jadi,
na matarajio ya kitamaduni,
na shinikizo la nafasi,
na mambo ya dunia hii...
Ikiwa kujitolea kwako kwa Mungu ni kwa sehemu na unakumbana na mzozo kama huo,
una uwezekano wa kubaki bila tofauti, kujaribu na kukaa kwenye uzio
hasa wakati ambapo kushikilia imani yako kunahusisha maumivu fulani, dhabihu fulani.
Lakini ukijaribu kuepuka maumivu katika mwili, hivi karibuni utakaribisha maumivu katika roho.
Kwa sababu kile kinachoanza na kuridhika muda si mrefu kitamalizika kwa ukiukwaji wa kanuni.
Ni suala la muda tu.
Njia ya kukiuka kanuni haina mwisho na inazidi kupanuka.
Ndio maana linapokuja swala la mambo ya Mungu, huduma ya Mungu -
lazima tujitoe kwa moyo wote.
Ahadi kamili, sio sehemu.
Hatumtumikii Mungu tu wakati inapotufaa.
Hatumtumikii Mungu tu nyakati zinapokuwa nzuri. Hapana!