-
-
Tuna mistari miwili hapa.
-
Tuuite huu mstari hapa, AB.
-
A na B zote ziko kwenye mstari.
-
Tuna mstari mwingine hapa.
-
Huu tunauita mstari CD.
-
Hivyo umepita kwenye nukta C na nukta D.
-
Na unaendelea bila kikomo.
-
Hii mistari imekaa sehemu moja.
-
Kwa hali hii, sehemu yenyewe ni kioo chetu,
-
au sehemu ndogo ya karatasi ambayo
-
tunaiangalia hapa.
-
Na haijawahi kuingiliana.
-
Hivyo ipo sehemu moja, lakini
-
haijawahi kukutana.
-
Kama hivi ni kweli na endapo sio
-
mstari mmoja, haiwezi kukutana
-
na ipo sehemu moja,
-
hivyo tunasema hii mistari ni sambamba.
-
-
Inaelekea kwenye uelekeo mmoja,
-
uelekeo mmoja.
-
Kama tukiitazama kama algebra,
-
tungeweza kusema ina mteremko sawa.
-
ila haiwezi kukutana.
-
Zinatumia nukta tofauti.
-
Tukichora mistari ya majira hapa,
-
zingekutana katika nukta tofauti,
-
ila zingekuwa na mporopoko sawa.
-
Ninachotaka kufanya ni kutafuta
-
pembe zinazohusiana na mistari sambamba.
-
Hivyo hapa, tuna mistari sambamba miwili.
-
Tunaweza kusema mstari AB ni sambamba kwa mstari CD.
-
Wakati mwingine unaweza kuona imebainishwa
-
kwenye mchoro kama huu.
-
Wanaweka mshale kuonesha
-
kuwa hii ni mistari sambamba.
-
Na kama umeshatumia mshale mmoja,
-
wanaweza kuweka mishale miwili kuonesha huu mstari ni sambamba
-
na huu mstari hapa.
-
Sasa baada ya hapo, ninachotaka kufanya
-
ni kuchora mstari utakaoingiliana na hii mistari sambamba.
-
Huu ndio mstari unaoingiliana na yote.
-
Ngoja nichore vizuri.
-
Nachora huo mstari hapo.
-
-
Nitafanya kitu hapa.
-
Ninauita huu mstari L.
-
Na huu mstari unaoingiliana na mistari sambamba,
-
tunauita mkingamo.
-
Huu ni mstari kingamo.
-
Unapishana na mistari sambamba yote.
-
Huu ni mkingamo.
-
Ninachotafuta ni pembe zinazotengenezwa,
-
na zinavyoendana na nyingine.
-
Pembe zilizotengenezwa kwenye mapishano
-
baina ya mstari kingamo na mistari sambamba.
-
Kwanza, tunaweza kuanza na
-
hii pembe hapa.
-
Tunaweza kuiita hii pembe--
-
kama nikiamua kUweka jina, itakuwa
-
D, hii nukta na kisha kitu kingine.
-
Ninaweza kuiita hii pembe hapa.
-
Tunafahamu hii itakuwa sawa na pembe inayoelekeana nayo.
-
Hivyo hii pembe inaelekeana na hii.
-
Hivyo itakuwa sawa na hiyo pembe hapo.
-
Pia tunafahamu hii pembe hapa,
-
itakuwa sawa na pembe inayoelekeana nayo, au pembe
-
inayotizamana nayo baada ya kukutana.
-
Hivyo itakuwa sawa na hiyo.
-
Wakati mwingine inaweza kubainishwa hivi,
-
ambapo unaweza kuona alama za pembe mbili kama hiyo.
-
Au wakati mwingine mtu anaweza kuandika
-
hivi ilikuonesha kuwa hizi pembe zinalingana
-
na hizi mbili hapa pia zinalingana.
-
Sasa jambo lingine tunalofahamu ni
-
tunaweza kufanya zoezi kama hilo hapa juu,
-
hizi mbili zitakuwa zinalingana
-
na hizo zitakuwa zinalingana.
-
Zote ni pembe mshabaha.
-
Kinachoshangaza hapa ni kuangalia mahusiano
-
baina ya hii pembe hapa, na hii pembe
-
hapa juu.
-
Na kama ukiangalia tu, utaona
-
uhusiano wenyewe ni upi--ni kwamba
-
zinakuwa ni pembe zinazolingana, kama
-
ukiweka kipima pembe na kupima,
-
utapata vipimo sawa.
-
Na nikichora mistari sambamba--
-
Ninachora imenyooka kulia na kushoto,
-
itakuwa kawaida kidogo.
-
Nikichukulia hii mistari miwili ni sambamba,
-
na nina mstari mkingamo hapa, ninachosema ni
-
hii pembe itakuwa
-
na vipimo sawa na hii.
-
Ili kuona hilo, fikiria kama unachora mstari.
-
Na kadiri unavyoona tofauti-- hivyo
-
inaonekana ndicho kinachotokea hapa.
-
Ukichukua mstari kama huu na kuuangalia hapa,
-
ni wazi kuwa zinalingana.
-
Na hakuna uhakika kwenye hili.
-
Hiki ni moja wapo ya vitu ambavyo mtu wa hesabu
-
atasema ni kawaida, kama ukiangalia
-
ukiwa unachora mstari, unaweza
-
kusema hizi pembe zinalingana.
-
Au unaweza kuweka kipima pembe hapa
-
ili upime hizi pembe.
-
Ukiweka kipima pembe hapa, utakuwa
-
na upande mmoja wa pembe hapa kwenye nyuzi sifuri,
-
na upande mwingine utaonesha hiyo alama.
-
Ukiweka kipima pembe hapa,
-
kitatokea kitu kilekile.
-
Upande mmoja utakuwa kwenye huu mstari sambamba,
-
na upande mwingine utakuwa kwenye nukta ileile.
-
Kwa kupewa hiyo, tunafahamu kwamba sio tuu
-
upande huu ni sawa na upande huu,
-
ni sawa pia na huu upande hapa.
-
Na hiyo inatuambia kuwa pale
-
pia ni sawa na ule upande pale.
-
Hivyo hizi zote zenye kijani ni sawa.
-
Kwa makubaliano yaleyale, hii pembe
-
itakuwa na vipimo sawa na hii pembe.
-
Na hiyo itakuwa sawa na hii pembe,
-
kwa sababu zinaelekeana, au ni pembe mshabaha.
-
Jambo muhimu la kufahamu
-
ni tulichokifanya hapa.
-
Pembe mshabaha zinalingana na pembe mkabala
-
kwenye sehemu za muingiliano zinalingana.
-
Hivyo hilo ni jina jipya
-
ninalitoa hapa.
-
Hii pembe na hii pembe zinalingana.
-
Zinawakilisha kona ya juu upande wa kulia,
-
kwenye huu mfano, tulioufanya.
-
Hapa pia nafikiri zinawakilisha upande wa juu kona ya kulia
-
mwa makutano.
-
Hii itakuwa kona ya juu upande wa kushoto.
-
Zitakuwa pembe zinazoelekeana na zinalingana.
-
Kwa mara nyingine nadhani,
-
kwa kukosekana jina zuri.
-
Mbali na hilo kuna jina lingine
-
tutaliona.
-
Tumehakikisha kuwa sio kwamba tu, hii pembe
-
ni sawa na hii, bali pia
-
ni sawa na hii pembe pia.
-
Na hizi pembe mbili-- ngoja nizipe majina
-
ili tupige hatua hapa.
-
Hivyo nitatumia herufi ndogo
-
kwenye pembe.
-
Tuiite hii a, hii b
-
Hii herufi c, herufi d,
-
kisha hii itakuwa e, f, g, h.
-
Tunafahamu kwenye pembe mshabaha b ni sawa na c.
-
Pia tunafahamu b ni sawa na f
-
kwa sababu ni pembe mkabala.
-
Kama f ni sawa na g.
-
Basi pembe mshabaha zinalingana,
-
Pembe mkabala nazo zinalingana,
-
pia tunafahamu b ni sawa na g.
-
Pia tunaweza kusema pembe za ndani zinalingana.
-
Unaziona zipo kwa ndani
-
ya mwingiliano.
-
Zipo kati ya mistari, ila zipo
-
pande zinazokinzana.
-
Sio lazima ufahamu hii dhana,
-
pembe za ndani zinazokinzana, inatakiwa
-
ufahamu tulichokifanya hapa.
-
Fahamu pembe mshabaha zinakuwa sawa
-
na pembe mkabala zinakuwa sawa pia.
-
Umeona na kwingine pia.
-
Tunafahamu itakuwa sawa na d, ambayo
-
itakuwa sawa na h, ambayo itakuwa sawa na e.
-