UJUMBE MUHIMU WA MWAKA WA 2024 | Ndugu Chris
-
0:00 - 0:05USIKIVU WA KIROHO
NDUGU CHRIS -
0:06 - 0:11Neema na amani iwe kwenu nyote katika jina zuri la Yesu Kristo.
-
0:11 - 0:19Na wacha nianze kwa kukukaribisha
katika Mwaka huu Mpya, 2024. -
0:19 - 0:20Asante, Yesu.
-
0:20 - 0:24Asante, Yesu, kwa neema ya
kuingia Mwaka Mpya - -
0:24 - 0:29hakika, kwa neema ya kuingia katika siku mpya,
dakika mpya, sekunde mpya. -
0:29 - 0:33Kwa sababu yote ni ya neema.
-
0:33 - 0:41Na watu wa Mungu,
maandalizi bora zaidi ya 2024 -
0:41 - 0:48huanza na tathmini ya kila siku, kuanzia leo.
-
0:48 - 0:57Kwa sababu haijalishi uzito wa nia au maazimio yetu, jua hili -
-
0:57 - 1:10maisha yako hayatabadilika mnamo 2024 mpaka
ubadilishe kitu unachofanya kila siku. -
1:10 - 1:20Ili kubaki thabiti mwaka wote wa 2024,
kaa thabiti leo. -
1:20 - 1:30Ili kujiandaa kwa mambo hayo ambayo huwezi kujiandaa kwa ajili ya 2024, jali leo
-
1:30 - 1:34kwa sababu leo tu ni yako.
-
1:34 - 1:41Sasa leo, nataka kushiriki nanyi ujumbe ambao kwa kweli umekuwa ukikua moyoni mwangu
-
1:41 - 1:50katika wiki za hivi karibuni na somo la ujumbe huu ni 'Usikivu wa Kiroho'.
-
1:50 - 1:55Narudia, usikivu wa kiroho.
-
1:55 - 2:11Unaona, hatari kubwa zaidi inayoletwa na giza iko katika kushindwa kwetu kulitambua.
-
2:11 - 2:15Kwa maneno mengine, wacha niweke kama hivi -
-
2:15 - 2:24kutokuwa na uwezo wetu wa kutambua tatizo halisi
ndilo tatizo. -
2:24 - 2:31Hilo ni tatizo kubwa zaidi kuliko ambalo wengi wetu tunayachukulia kama matatizo katika maisha yetu leo.
-
2:31 - 2:34Na angalieni hili, enyi watu wa Mungu.
-
2:34 - 2:46njia ya uhakika ya kuongeza muda na hata kuongeza tatizo lako ni kutolitambua.
-
2:46 - 2:59Jinsi unavyokabiliana na tatizo lako ni tatizo kubwa kuliko tatizo lenyewe.
-
2:59 - 3:02Natumaini mtafuata
ninachosema, watu wa Mungu. -
3:02 - 3:10Tatizo tunalokabiliana nalo leo liko katika
jinsi tunavyokabili matatizo yetu. -
3:10 - 3:18Na ujue hili - kuna baadhi ya majaribio,
baadhi ya hali katika safari ya maisha -
3:18 - 3:27kwamba rasilimali za ndani pekee
zinaweza kukudumisha. -
3:27 - 3:32Katika dokezo hili, kumbuka
nilisema kuhusu 'usikivu wa kiroho'. -
3:32 - 3:38Ninataka kukupeleka kwenye Maandiko katika Waebrania 3.
-
3:38 - 3:50Hilo litakuwa andiko la uthibitisho la
ujumbe wa leo - Waebrania 3:12-14. -
3:50 - 3:53Tusome watu wa Mungu.
-
3:53 - 4:03“Angalieni, ndugu zangu, kusiwe na moyo wa uovu miongoni mwenu
-
4:03 - 4:08ya kutoamini na kujitenga na Mungu aliye hai;
-
4:08 - 4:16bali tuonyane kila siku,
maadamu iitwapo, Leo; -
4:16 - 4:23asije mmoja wenu akafanywa mgumu kwa udanganyifu wa dhambi.
-
4:23 - 4:26Kwa maana tumekuwa washirika wa Kristo
-
4:26 - 4:36ikiwa tutashikilia mwanzo wa imani yetu
imara hadi mwisho...” -
4:36 - 4:50Sasa, adui mkubwa wa maendeleo ya kiroho ni moyo mgumu -
-
4:50 - 4:57moyo ambao hauna usikivu wa kiroho,
-
4:57 - 5:04moyo uliotiwa giza, uliotiwa giza,
uliodanganywa na dhambi. -
5:04 - 5:15Na kadiri udanganyifu ulivyo ndani zaidi, ndivyo giza linavyozidi kuwa kubwa.
-
5:15 - 5:23"Basi ikiwa nuru iliyo ndani yako ni giza,
giza hilo ni kuu jinsi gani" -
5:23 - 5:27maneno ya Yesu katika Mathayo 6:23.
-
5:27 - 5:39Kwa sababu ikiwa shetani anaweza kukudanganya,
basi anaweza kukupotosha kwa urahisi sana. -
5:39 - 5:47Sasa, angalia tu karibu nawe
kile kinachotokea ulimwenguni. -
5:47 - 5:55Haichukui muda mrefu kutambua
athari za giza - -
5:55 - 5:58uasi dhidi ya Mungu na Neno lake.
-
5:58 - 6:01Lakini usiangalie tu mazingira yaliyo nje yako. Hapana!
-
6:01 - 6:05Ninakuita leo kutazama ndani yako.
-
6:05 - 6:12Kwa sababu kiini cha uasi wetu
ni uasi ndani ya mioyo yetu. -
6:12 - 6:23Tamaa za mwili zinapozingatiwa vibaya, matendo ya dhambi hayako mbali kamwe.
-
6:23 - 6:29Lakini siri ya neema ya ajabu ya Mungu
-
6:29 - 6:34ni kwamba daima kuna nafasi ya toba.
-
6:34 - 6:38Lakini kumbuka, watu wa Mungu -
-
6:38 - 6:53wepesi wa toba yetu huakisi kiwango cha usikivu wetu wa kiroho.
-
6:53 - 7:03Kupinga toba kunaonyesha
ugumu wa moyo. -
7:03 - 7:05Sio kwamba sisi Wakristo
hatufanyi makosa. -
7:05 - 7:08Tunafanya. Tunaweza kufanya makosa.
-
7:08 - 7:13Lakini unapokuwa na hisia za kiroho,
unakuwa mwepesi kutambua, -
7:13 - 7:18mwepesi wa kujibu, mwepesi wa kujipatanisha,
mwepesi wa kutubu. -
7:18 - 7:29Lakini upinzani dhidi ya toba unaonyesha
ugumu wa moyo. -
7:29 - 7:40Hii mara nyingi hujidhihirisha katika
namna ya kuhalalisha dhambi ya ndani. -
7:40 - 7:48Na shetani akiweza kufanikiwa kuufanya moyo wako kuwa mgumu,
-
7:48 - 7:57uhalalishaji dhambi wa siri hivi karibuni utageukia kuwa
utenda dhambi wa hadharani, -
7:57 - 8:01hata kusheherekea dhamba hadharani -
-
8:01 - 8:06si tu kwa yale tunayofanya bali
kwa yale tunayoshindwa kufanya. -
8:06 - 8:17Ikiwa hausimamii kitu fulani,
basi hakika utaangukia kwa kitu fulani. -
8:17 - 8:24Nataka mtafakari juu ya hili,
watu wa Mungu - -
8:24 - 8:35upinzani dhidi ya toba huonyesha
ugumu wa moyo. -
8:35 - 8:42Na ikiwa uangalifu hautachukuliwa,
ikiwa dhamiri haijaamshwa; -
8:42 - 8:53tunaweza kuhama kutoka katika utambuzi wa makosa hadi uthibitisho wa makosa.
-
8:53 - 8:54Hivyo ndivyo shetani anataka.
-
8:54 - 9:00Anataka tuhamishe ardhi hadi
eneo lililo nje ya nuru. -
9:00 - 9:10Kwa sababu tunapokuwa gizani,
'ukweli' unaweza kupotoshwa kwa urahisi. -
9:10 - 9:14Kipofu akiwaongoza vipofu...
-
9:14 - 9:22Hii ndiyo sababu kudharau dhambi
ni hatari sana sana. -
9:22 - 9:35Hakuna hatua ya kupunguza viwango vya
ya Mungu inaisha vyema. -
9:35 - 9:38Narudia tena, watu wa Mungu.
-
9:38 - 9:47Hakuna hatua ya kupunguza, kushusha
viwango kamili vya Mungu huisha vyema. -
9:47 - 9:52Sasa, nataka kutoa dokezo
la onyo katika hatua hii. -
9:52 - 9:59Jihadharini na hatia ya usadikisho wa kughushi -
-
9:59 - 10:06wakati matendo yako yanasukumwa na chanzo nje ya Neno la Mungu,
-
10:06 - 10:12kwa sababu nje ya utukufu wa Mungu. Jihadhari!
-
10:12 - 10:19Ibilisi hufurahia kujivika uadilifu, ubinafsi
-
10:19 - 10:28katika mavazi ya kuonekana kuwa mema,
muonekano wa fadhili, unaoonekana kuwa wa huruma -
10:28 - 10:34wenye kuonekana kuwa na utauwa
lakini akikana nguvu zake (2 Timotheo 3:5). -
10:34 - 10:38Jihadharini na hatia ya usadikisho wa kughushi.
-
10:38 - 10:48Chanzo pekee cha usadikisho wa kweli
ni Neno na Roho. -
10:48 - 10:54Ni Neno la Mungu, kama lilivyofunuliwa na
Roho Mtakatifu, ambalo hufichua giza. -
10:54 - 10:58Kwa hiyo kadiri moyo wako unavyojishughulisha zaidi na Neno la Mungu,
-
10:58 - 11:06kadiri Neno la Mungu linavyotawala moyo wako, ndivyo unavyokuwa mwangalifu zaidi kiroho.
-
11:06 - 11:12Inaamsha, inakuza
sauti ya dhamiri. -
11:12 - 11:29Na wewe ndivyo ulivyo leo kwa sababu ya kusikiliza au kupuuza dhamiri yako.
-
11:29 - 11:32Wewe ndivyo ulivyo leo
-
11:32 - 11:43kama matokeo ya kusikiliza au kupuuza
sauti ya dhamiri yako. -
11:43 - 11:54Kadiri tunavyojikita zaidi katika Neno la Mungu, ndivyo mioyo yetu inavyozidi kuwa na nidhamu.
-
11:54 - 12:01Mioyo yetu inaamshwa na
uovu mkubwa wa dhambi. -
12:01 - 12:05Ndiyo maana tunakuwa wepesi wa kutubu.
-
12:05 - 12:07Ndiyo maana tupo wepesi kutambua makosa yetu.
-
12:07 - 12:13Na hii hutuhifadhi, inatulinda dhidi ya mitego hiyo hatari
-
12:13 - 12:19tunapokutana na njia ya udanganyifu.
-
12:19 - 12:24Watu wa Mungu, ninasisitiza nini
katika ujumbe huu leo? -
12:24 - 12:29Dawa ya moyo mgumu
-
12:29 - 12:37ni kukaa ukiwa umeshiba katika Maandiko
na kulowekwa katika maombi. -
12:37 - 12:46Ili uendelee kuwa mwenye kujali mambo ya kiroho, tunza moyo wako ukitumia Neno la Mungu.
-
12:46 - 12:53Maombi kila siku huzuia udanganyifu.
-
12:53 - 13:02Lakini kutokuwa na mudai wa kila siku na Mungu ni kichocheo cha maafa katika maisha yako ya kiroho.
-
13:02 - 13:08Kwa hivyo, ninataka kuwapa changamoto
sasa hivi na swali hili. -
13:08 - 13:20Je, unafanya nini kila siku ambacho
kinakutajirisha kiroho? -
13:20 - 13:24Maana nina neno la kukupa ushauri.
-
13:24 - 13:30Na tazama, enyi watu wa Mungu, ushauri huu haupaswi kuchukuliwa kwa lenzi ya dini.
-
13:30 - 13:35Hapana. Ni lazima upokelewe kupitia ufahamu wa uhusiano na Mungu.
-
13:35 - 13:41Dini inakimbilia kwenye utamaduni
kwa sababu haina uhai, -
13:41 - 13:45lakini uhusiano hutia moyo
na kukuza tabia za kiungu, -
13:45 - 13:48utaratibu wa kimungu katika nuru ya Neno la Mungu.
-
13:48 - 13:53Kwa hivyo, neno la ushauri kwako:
-
13:53 - 14:00Katika nyumba yako, nakuhimiza kuweka kando
-
14:00 - 14:08mahali pa sala, pa kutaamali,
pa kutafakari. -
14:08 - 14:13Najua wengi wetu wanaweza kusema hatuna nafasi ya chumba kizima.
-
14:13 - 14:15Ikiwa unayo nafasi, utukufu kwa Mungu.
-
14:15 - 14:26Lakini katika nyumba yako, tenga eneo -
kama bado hujafanya hivyo - -
14:26 - 14:34kujizungusha kwa uangalifu na mambo ambayo yanakukumbusha uhusiano wako na Mungu.
-
14:34 - 14:38Kwa nini? Kwa sababu sisi sote ni dhaifu.
-
14:38 - 14:44Katika ulimwengu uliojaa ukengeufu,
Nakutia moyo leo - -
14:44 - 14:49tafuta kitu cha asili kukukumbusha
kuhusu kitu kisicho cha kawaida. -
14:49 - 14:57Unda kitu unachoweza kuona ili kuuelekeza moyo wako kuelekea mambo ambayo hayaonekani.
-
14:57 - 15:03Tazama, watu wa Mungu, nawaambia -
moyo wenu ndio chumba halisi cha maombi. -
15:03 - 15:06Sijaribu kupinga ukweli huo.
-
15:06 - 15:08Moyo wetu ndio chumba halisi cha maombi.
-
15:08 - 15:15Lakini lazima tukubali kwamba hakuna mtu aliye juu ya ushawishi na mazingira yana nafasi yake.
-
15:15 - 15:17Mazingira ni muhimu.
-
15:17 - 15:20Wakati fulani unarudi nyumbani
na moyo wako unafadhaika. -
15:20 - 15:22Labda umekuwa na mgongano
na mfanyakazi mwenzako. -
15:22 - 15:25Labda kuna kutoelewana
na mwenzi wako. -
15:25 - 15:29Labda umepata shinikizo na mvutano katika eneo fulani la maisha yako
-
15:29 - 15:31na moyo wako unafadhaika.
-
15:31 - 15:37Kuwa na mahali nyumbani kwako ambapo unaweza kwenda na kupatana na Mungu -
-
15:37 - 15:40mahali panapokukumbusha uhusiano wako na Mungu,
-
15:40 - 15:42mahali panapoelekeza mwelekeo wako kwa Mungu,
-
15:42 - 15:44mahali ambapo unaweza kuomba,
-
15:44 - 15:47mahali unapoweza kulala
na kutafakari wema wa Mungu, -
15:47 - 15:52mahali ambapo unaweza kusikiliza muziki wa kuabudu na kuruhusu moyo wako uinuke katika sifa.
-
15:52 - 15:58Tafuta kitu cha asili kukukumbusha kitu kisicho cha rohoni.
-
15:58 - 16:03Hili ni neno la ushauri kwako
-
16:03 - 16:15ili kukusaidia kuendelea kuwa mwangalifu katika kipindi chote cha 2024 na kuendelea.
-
16:15 - 16:20Sasa hivi, watu wa Mungu,
mnapotafakari maneno haya, -
16:20 - 16:23Nataka nikupeleke kwenye muda wa maombi.
-
16:25 - 16:28WAKATI WA MAOMBI
-
16:30 - 16:35Sasa hivi, watu wa Mungu, tuombe.
-
16:35 - 16:45Mwombe Mungu sasa hivi akusafishe
kwa Damu yake ya thamani -
16:45 - 16:56na kukuosha uwe mweupe kuliko theluji!
-
16:56 - 17:01Katika jina kuu la Yesu Kristo!
-
17:01 - 17:10Ni nini kinachoufanya moyo wako kuwa mgumu
katika wakati huu? -
17:10 - 17:15KIondoshwe katika
jina kuu la Yesu Kristo! -
17:15 - 17:18Ondoshwa sasa hivi!
-
17:18 - 17:26Roho hiyo ya ajabu inayokuza sauti ya udanganyifu ndani - inyamazishwe!
-
17:26 - 17:28Nyamaza sasa hivi!
-
17:28 - 17:36Sauti hiyo inayopinga toba -
nyamazishwa! -
17:36 - 17:43Katika jina la Yesu Kristo!
-
17:43 - 17:56Mwombe Mungu sasa hivi akuongezee usikivu wako wa kiroho ili kuitambua sauti yake.
-
17:56 - 18:02Katikati ya sauti nyingi zinazokinzana na zinazopingana katika ulimwengu huu -
-
18:02 - 18:06acha roho yako iwe sikivu kwa Roho Mtakatifu!
-
18:06 - 18:09Acha kuwe na usikivu!
-
18:09 - 18:11Acha kuwe na ufunuo!
-
18:11 - 18:17Acha kuwe na ufahamu
unaoangazwa na Neno! -
18:17 - 18:26Katika jina kuu la Yesu.
-
18:26 - 18:38Bwana Yesu Kristo, hatujui la kufanya lakini macho yetu yako kwako (2 Mambo ya Nyakati 20:12).
-
18:38 - 18:43Acha macho yako yawe kwa Kristo peke yake.
-
18:43 - 18:50Hebu moyo wako utengwe kwa ajili ya Kristo pekee.
-
18:50 - 18:54Katika jina kuu la Yesu Kristo.
-
18:54 - 19:06Bwana Yesu, tupe neema hiyo ya kuishi maisha adili yanayolitukuza jina lako -
-
19:06 - 19:11kwa maneno, kwa mawazo na kwa vitendo -
-
19:11 - 19:20kote 2024 na zaidi,
katika jina kuu la Yesu Kristo! -
19:20 - 19:28Katika jina la Yesu tunaomba. Amina!
-
19:28 - 19:30Asante, Yesu.
-
19:30 - 19:32Mungu awabariki, watu wa Mungu,
-
19:32 - 19:40unapoendelea kuutafuta moyo wake
ili kuona maisha waziwazi.
- Title:
- UJUMBE MUHIMU WA MWAKA WA 2024 | Ndugu Chris
- Description:
-
Sikia Neno la Mungu lenye nguvu kutoka kwa Ndugu Chris ili kukutayarisha kwa ajili ya Mwaka Mpya wa 2024!
➡️ Pata Kutiwa Moyo Kila Siku kwenye WhatsApp - https://godsheart.tv/whatsapp/
➡️ Saidia TV ya Moyo wa Mungu kifedha - https://godsheart.tv/financial/
➡️ Habari kuhusu Maombi Shirikishi - https://godsheart.tv/interactive-prayer/
➡️ Jitolee kama Mtafsiri wa TV ya Moyo wa Mungu - https://godsheart.tv/translate/
➡️ Shirikisha ushuhuda wako - https://godsheart.tv/testimony
➡️ Jiunge na Ibada yetu ya Maombi ya Moja kwa Moja Jumamosi ya kwanza ya kila mwezi - https://www.youtube.com/godshearttv/live - Video Language:
- English
- Team:
God's Heart TV
- Duration:
- 20:11
![]() |
Stephenmigwi edited Swahili subtitles for IMPORTANT MESSAGE FOR 2024! | Brother Chris | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for IMPORTANT MESSAGE FOR 2024! | Brother Chris | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for IMPORTANT MESSAGE FOR 2024! | Brother Chris | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for IMPORTANT MESSAGE FOR 2024! | Brother Chris | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for IMPORTANT MESSAGE FOR 2024! | Brother Chris | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for IMPORTANT MESSAGE FOR 2024! | Brother Chris | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for IMPORTANT MESSAGE FOR 2024! | Brother Chris | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for IMPORTANT MESSAGE FOR 2024! | Brother Chris |