< Return to Video

2025 IS YOUR YEAR—START IT RIGHT WITH THIS SIMPLE TRUTH!!!

  • 0:00 - 0:07
    Mwaka unapokaribia kufika mwisho, mara nyingi tunajitahidi kuona ni sherehe gani tutahudhuria, sivyo?
  • 0:08 - 0:13
    Utasherehekea wapi mwaka huu? Jibu ni wazi: katika uwepo wa Bwana!
  • 0:13 - 0:17
    Ni jambo jema kwetu, kila tarehe 31 Desemba
  • 0:19 - 0:26
    kutumia muda kidogo kutafakari yale tuliyofanikiwa mwaka uliopita.
  • 0:26 - 0:32
    Tunakaribia kuingia mwaka mpya, "Wacha nitazame nyuma. Nimeweza kufanya nini hadi sasa?"
  • 0:33 - 0:35
    "Nimefanikiwa nini maishani mwangu?"
  • 0:36 - 0:41
    "Je, ninaweza kuwa na furaha? Je, ninaweza kujivunia kitu,
  • 0:41 - 0:48
    na kusema kwamba kwa hakika nimefanikiwa mambo kadhaa mwaka huu?"
  • 0:48 - 0:52
    Au je, unapoangalia nyuma, unaona makosa yako tu?
  • 0:53 - 0:57
    Je, unaona maamuzi mabaya uliyoyafanya?
  • 0:57 - 1:00
    Unaona watu uliowaumiza unapotazama nyuma.
  • 1:00 - 1:05
    Kama mtoto wa Mungu, ni hatari kutazama nyuma kwenye maisha yako ya zamani.
  • 1:06 - 1:10
    "Lakini kwa nini, ndugu, umetueleza tuangalie mafanikio yetu ya zamani!"
  • 1:11 - 1:16
    Ndiyo, tunapaswa kutazama nyuma tu kwa ajili ya utukufu wa Mungu.
  • 1:17 - 1:19
    Kwa nini ni hatari kutazama nyuma kama mtoto wa Mungu?
  • 1:20 - 1:25
    Kwa sababu kutazama maisha yako ya zamani ni mtego wa shetani!
  • 1:26 - 1:30
    Anakujaribu kukumbusha jinsi ulivyokuwa mzuri na kile unachokosa sasa.
  • 1:30 - 1:38
    Anakujaribu kukumbusha muda mzuri uliokuwa nao na marafiki zako, ukifanya chochote ulichotaka,
  • 1:38 - 1:43
    lakini sasa unatumia muda wako na Wakristo.
  • 1:43 - 1:50
    Kisha, unaanza kufikiria ungemalizia wapi kama hungekuwa kwenye uwepo wa Mungu.
  • 1:50 - 1:56
    Kwa maneno haya machache, tutafika kwenye kichwa cha ujumbe wa leo, ambacho ni:
  • 1:56 - 1:58
    "MTIZAMO WAKO KWA MAISHA."
  • 1:59 - 2:07
    Kama mtoto wa Mungu, mtazamo wako kwa maisha lazima uwe tofauti na watu wa kidunia.
  • 2:07 - 2:09
    mtazamo wako kwa maisha ni nini?
  • 2:09 - 2:14
    Mke wa Lutu alilipa kwa uhai wake kwa kutotii Neno la Mungu!
  • 2:14 - 2:18
    Ingawa alijua Neno la Mungu,
  • 2:18 - 2:22
    ingawa alijua maelekezo ya haki yaliyopewa na Mungu,
  • 2:23 - 2:31
    alisisitiza kufanya mambo kwa njia yake mwenyewe, na ikamgharimu uhai wake, kama wengi wetu tunavyofanya leo.
  • 2:33 - 2:37
    Kujua Neno la Mungu hakutakuokoa.
  • 2:37 - 2:41
    Shetani pia anajua Neno la Mungu, hata zaidi yako!
  • 2:42 - 2:50
    Shetani alipoenda kumjaribu Yesu Kristo, alimwambia: "Imeandikwa."
  • 2:51 - 2:53
    Ni ujasiri gani!
  • 2:54 - 2:59
    Adui wa nafsi ya mwanadamu alikwenda kwa Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, na kumwambia,
  • 2:59 - 3:04
    "Tazama, imeandikwa! Mungu alisema hivyo, kwa hiyo unapaswa kufanya hivyo!"
  • 3:05 - 3:12
    Alijaribu kutumia maneno ya Mungu kumwelekeza Yesu Kristo afanye nini!
  • 3:12 - 3:16
    Unadhani kwa sababu unajua Neno la Mungu, utaingia mbinguni siku moja!
  • 3:16 - 3:20
    Wengi wetu tunafanya vivyo hivyo. Tuna njia zetu wenyewe.
  • 3:20 - 3:24
    Tunajua Neno la Mungu, tunasoma Biblia, tunajua Neno la Mungu linasema nini,
  • 3:24 - 3:25
    lakini tuna njia zetu!
  • 3:27 - 3:28
    Tunatii kwa njia zetu!
  • 3:29 - 3:32
    Tunafanya kile Neno la Mungu kinasema kwa njia zetu.
  • 3:33 - 3:36
    Mke wa Lutu alitii Neno la Mungu kwa njia yake mwenyewe.
  • 3:39 - 3:42
    Alikuwa akimfuata mumewe. Si hivyo Biblia inavyosema?
  • 3:43 - 3:46
    Inasema kwamba Lutu alikuwa akitembea, na mke wake alikuwa akimfuata.
  • 3:47 - 3:52
    Kama watu wengi leo, mwanaume huenda kanisani na mke hufuata
  • 3:53 - 3:59
    Kuja kwako kanisani ukimfuata mume au mke hakutakuokoa.
  • 4:01 - 4:05
    Kutii Neno la Mungu ndiko kutakuokoa!
  • 4:06 - 4:12
    Yesu Kristo anajua jinsi tusivyostahili neema Yake,
  • 4:13 - 4:21
    ndiyo maana Ameamua kuacha mbali yaliyopita ili kubainisha yajayo!
  • 4:21 - 4:30
    Kumbuka, kutoka kwa Lutu na familia yake kutoka Sodoma na Gomora ni mfano.
  • 4:30 - 4:39
    Inawakilisha kutoka kwako na kwangu kutoka maisha ya dhambi na kuingia maisha ya haki!
  • 4:40 - 4:44
    Kutoka maisha yasiyo ya haki kwenda maisha ya utakatifu.
  • 4:45 - 4:49
    Wengi wetu, ingawa tulifanya uamuzi wa kutembea na Bwana, na Yesu Kristo,
  • 4:50 - 4:58
    katikati ya safari, tunasema: "Kuna nini kibaya na kuvuta sigara moja tu?"
  • 4:58 - 5:01
    Tunapojaribu kutafuta sababu za makosa yetu, tunataja neema.
  • 5:03 - 5:07
    Tunapojaribu kumhukumu mtu, tunasema: "Neno la Mungu linasema hivi na vile
  • 5:07 - 5:08
    kwa nini unafanya hivi?"
  • 5:08 - 5:09
    "Wewe ni mnafiki!"
  • 5:11 - 5:16
    Hakuna neema katika hali hii. Unajua Neno la Mungu na unalitumia katika hali hii!
  • 5:16 - 5:24
    Tumeitwa kumfuata Mungu, kwa njia ya Mungu, si kwa njia yetu!
  • 5:24 - 5:27
    Njia ya Mungu iko hapa, katika Neno Lake.
  • 5:27 - 5:36
    Ukipenda kufanikiwa maishani, lazima ujifunze kutazama mbele,
  • 5:38 - 5:42
    kwenye vita vyako vya kiroho pamoja na Yesu Kristo.
  • 5:42 - 5:49
    Kwa sababu kwa kutazama mbele ndipo unapoona mambo mapya, upeo mpya,
  • 5:50 - 5:54
    na fursa mpya ambazo usingewahi kuota ndoto kuzihusu!
  • 5:54 - 5:56
    Unajua kwa nini Mungu alitupa Neno Lake?
  • 5:58 - 6:07
    Alitupa Neno Lake kutufundisha hekima Yake ili tusije kuwa wahanga wa ujinga wetu.
  • 6:09 - 6:15
    Neno la Mungu linasema:
    "Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa." (Hosea 4:6)
  • 6:15 - 6:23
    Tunahitaji kutatua matatizo ya leo kwa kutumia maarifa ya jana.
  • 6:25 - 6:27
    Matumizi ya mbinu za jana
  • 6:28 - 6:29
    hakuwezi kusaidia!
  • 6:29 - 6:35
    Ikiwa mbinu za jana zingeweza kutatua matatizo yako, matatizo yako yangekuwa yamekwisha leo!!
  • 6:36 - 6:42
    Kwa wengi wetu, tupo jangwani sasa, tupo kwenye ardhi kavu.
  • 6:43 - 6:48
    Tuko mahali ambapo hakuna njia, bila njia ya kutoka, na tunajihisi tumepotea
  • 6:49 - 6:54
    Neno la Mungu linakuambia leo kwamba ikiwa hutatazama nyuma,
  • 6:56 - 7:01
    ikiwa hutatazama nyuma kwenye yaliyopita, Mungu atafanya jambo jipya maishani mwako.
  • 7:02 - 7:06
    Jambo hili jipya ni kwamba Atakufanyia njia mahali ambapo hakuna njia!
  • 7:07 - 7:15
    [♪ Muziki ♪]
Title:
2025 IS YOUR YEAR—START IT RIGHT WITH THIS SIMPLE TRUTH!!!
Description:

more » « less
Video Language:
English
Duration:
07:21

Swahili subtitles

Incomplete

Revisions Compare revisions