Barua Kwa Mwanangu Mpendwa!
-
0:00 - 0:10Barua kwa mwanangu, Josiah Timothy Tonge.
-
0:10 - 0:19Mpendwa Josiah, ninapokushika mikononi mwangu
kama baba wa mara ya kwanza, -
0:19 - 0:24Nimepigwa na ukumbusho mtakatifu.
-
0:24 - 0:32Wewe ni wetu wa kushikilia, sio wetu kumiliki.
-
0:32 - 0:40Wewe ni zawadi kutoka kwa Mungu, uliofumwa kiustadi na Mbuni wa Kimungu,
-
0:40 - 0:49umesanifiwa mahali pa siri kwa mikono ile ile iliyopanga nyota angani.
-
0:49 - 1:01Zawadi ya thamani iliyokabidhiwa kwetu -
kwa msimu, kwa sababu. -
1:01 - 1:07Na katika dhamana hiyo kuna uzito mtakatifu
wa utumishi - -
1:07 - 1:18kuuchunga moyo wako kuelekea
Yule aliyepulizia uhai ndani yake, -
1:18 - 1:25ambaye alama za vidole vyake
zipo katika kila nyuzi ya nafsi yako. -
1:25 - 1:33Kupenda kwa dhati, lakini kushikilia kwa uhuru -
-
1:33 - 1:44imara vya kutosha katika kusaidia kukua
lakini legevu vya kutosha kuachilia. -
1:44 - 1:55Kwa maana sio uimara wa kushikilia kwetu,
bali utimilifu wa ukuaji wako. -
1:55 - 2:05Na upendo wa kweli hujiandaa kuondoka.
-
2:05 - 2:16Kwa hivyo ninakubeba kwa uangalifu na ufahamu wa Yule anayetubeba sisi sote.
-
2:16 - 2:23Upitapo kutoka tumboni hadi
kwenye ulimwengu uliokaribia, -
2:23 - 2:28kulikuwa na maswali mengi ambayo yalizunguka kichwani mwangu.
-
2:28 - 2:35Lakini sauti ya kilio chako cha kwanza
ikayanyamazisha yote. -
2:35 - 2:39Ilikuwa ni ufunuo rahisi.
-
2:39 - 2:46Kinachohitajika kwa kazi
tayari kiko ndani, -
2:46 - 2:56kwa maana hakuna kazi ya kimungu inayokuja
bila mgawo wa kimungu. -
2:56 - 3:06Kwa kweli, Yosia, ujio wako uliamsha sehemu yangu ambayo ilikuwa imelala,
-
3:06 - 3:16kwa maana hakuna wajibu mtakatifu zaidi kama jukumu la kumlea mtoto katika kumcha Bwana.
-
3:16 - 3:23Ndiyo, Yosia, umeingia
ulimwengu uliojaa mashaka. -
3:23 - 3:31Lakini kuna jambo moja unaweza kuwa na uhakika nalo - hiyo ni nafasi yako katika mioyo yetu.
-
3:31 - 3:41Hatuna uwezo wa kuamua nini kinakungoja wewe, Yosia, katika safari hii ya maisha.
-
3:41 - 3:51Lakini maadamu Mungu anatupa pumzi kwenye mapafu yetu, mimi na mama yako tutatembea nawe.
-
3:51 - 3:57Pale maisha yatakapojaribu kukuangusha,
tutakusaidia kusimama. -
3:57 - 4:05Wakati usiku unahisi kuwa mrefu na wenye upweke,
tutakaa nawe mpaka kutakapopambazuka. -
4:05 - 4:17Wakati maono yanaonekana kutoeleweka, tutakuelekeza kwa maombi kuelekea kusudi lako.
-
4:17 - 4:27Wakati mstari kati ya tumaini na kukata tamaa haunoekani wazi,
-
4:27 - 4:36tutakuwa ishara kwa Mmoja pekee ambaye hawezi kamwe kukukatisha tamaa.
-
4:36 - 4:40Na wakati ulimwengu utajaribu
kuhoji utambulisho wako, -
4:40 - 4:47tutakukumbusha wewe ni nani -
mtoto wa ahadi. -
4:47 - 4:56Tutakukumbusha wewe ni nani - iwe kwa kutia moyo kwa upole au kemeo kali.
-
4:56 - 5:07Tutakulea na kukulisha kwa yote ambayo Mungu ametupa,
-
5:07 - 5:12tukijua hilo wakati sisi
tukitunza lishe, -
5:12 - 5:18Anatunza kustawi.
-
5:18 - 5:39Thamani halisi ya zawadi za Mungu inategemea uwezo wetu wa kuzirejesha kwake.
-
5:39 - 5:47Josiah, naomba siku moja, utasoma maneno haya
-
5:47 - 5:54na upate ndani yake ujasiri wa kukabiliana na dhoruba zako mwenyewe kwa imani,
-
5:54 - 6:00kujua kwamba Yule aliye kuumba anaenda mbele yako.
-
6:00 - 6:06Kumbuka yule wajina lako,
-
6:06 - 6:15mfalme katika 2 Mambo ya Nyakati 34 aliyemtafuta Mungu kwa moyo wake akiwa na umri mdogo
-
6:15 - 6:24na kuona vyema - vyema sana kiasi kwamba nguvu ya utawala wa kifalme wa kidunia
-
6:24 - 6:29haikuathiri usafi wa uwana wa kiroho.
-
6:29 - 6:38Mtu ambaye shauku yake kwa Neno la Mungu haikuwa ya kupita.
-
6:38 - 6:50lakini ilipita kwenye vitendo na dhamira ambazo ziliishi zaidi ya maisha yake.
-
6:50 - 6:55Tukio lake likupe motisha.
-
6:55 - 7:07Na maisha yetu yawe mafundisho ya viwango tunavyotafuta kuviweka.
-
7:07 - 7:14Kwa kuwa Wakristo, tunajitahidi kuelekea ukamilifu.
-
7:14 - 7:26kutoka mahali pa kujisalimisha kwa Yule anayetukamilisha.
-
7:26 - 7:40Josiah, ni furaha yetu, haki yetu, heshima yetu kukuwasilisha kwa Mungu Aliye Juu Sana.
-
7:40 - 7:47na katika uwepo wake, natangaza baraka hizi juu yako
-
7:47 - 7:54kulingana na Hesabu 6:24-26.
-
7:54 - 8:02Josiah, BWANA akubarikie, na kukilinda
-
8:02 - 8:11BWANA akuangazie nuru za uso wake, na kukufadhili;
-
8:11 - 8:21BWANA akuinulie uso wake, na kukupa amani.
-
8:21 - 8:35Katika jina kuu la YESU, Amina!
-
8:35 - 8:39Mwanangu, nakupenda kwa moyo wangu wote.
-
8:39 - 8:46Asante kwa kuniongoza kutoka kuwa ndugu hadi kuwa baba.
-
8:46 - 8:55Juu ya yote, naomba ukuwe katika upendo kwa Yesu Kristo,
-
8:55 - 9:03kwa moyo wako wote, akili, roho, nafsi na nguvu.
-
9:03 - 9:12Kwa maana hiyo ni msingi thabiti ambao kila kitu kingine kinatoka.
-
9:12 - 9:16Kwa upendo kutoka kwa baba yako.
-
9:16 - 9:25P.S. - Natumai utakua na uweza wa kucheza kama mama yako, si kama baba yako!
-
9:25 - 9:28Katika jina la Yesu.
-
9:31 - 9:40Neema na amani kwenu nyote, watu wa Mungu, katika jina kubwa la Yesu Kristo.
-
9:40 - 9:46Kuna matukio mawili katika maisha
-
9:46 - 9:55ambayo yanatoa fursa isiyoweza kuepukwa ya kuamka kiroho -
-
9:55 - 10:05kuona mwanzo wa maisha na kuona mwisho wa maisha.
-
10:05 - 10:13Siwezi kufikiria jinsi inavyowezekana mtu kuona
-
10:13 - 10:19kuibuka au kuondoka kwa maisha,
-
10:19 - 10:29bila kufikiria kwa undani juu ya maana ya maisha, juu ya kile maisha yanahusisha kweli.
-
10:29 - 10:35Ninashiriki hili nawe leo, kwa sababu siku chache zilizopita za maisha yangu
-
10:35 - 10:42hakika zimekuwa miongoni mwa matukio ya kukumbukwa, ya ajabu, yenye unyenyekevu,
-
10:42 - 10:47ya changamoto, kuchoka katika maisha yangu-
-
10:47 - 10:56kuwa na fursa ya kushuhudia kuwasili kwa mtoto wetu wa kwanza, Josiah,
-
10:56 - 11:03mnamo Alhamisi, tarehe 29 Mei, 2025.
-
11:03 - 11:07Kwanza kabisa - utukufu kwa Mungu!
-
11:07 - 11:12Asante Yesu kwa zawadi zzuri ya maisha.
-
11:12 - 11:17Nataka pia kumpongeza mke wangu, Allison,
-
11:17 - 11:22na kwa kweli, nataka kuwapongeza akina mama duniani kote.
-
11:22 - 11:30Ninasifu uvumilivu wenu, ustahimilivu, na imani yenu inapohusiana na kuzaa. Wow!
-
11:30 - 11:37Na neno la ushauri kwa waume ambao huenda wananitazama sasa hivi.
-
11:37 - 11:50Wakati mkeo anapojifungua, simama pamoja naye katika maombi.
-
11:50 - 11:58Kaa karibu na yeye kimwili na simama wima na yeye kiroho.
-
11:58 - 12:09Kuwa sauti ya utulivu na nanga ya amani katika bahari ya maumivu.
-
12:09 - 12:14Hii ni siri. Ni siri, ndugu zangu na dada zangu katika Kristo -
-
12:14 - 12:27jinsi kitu kizuri namna hiyo kinavyotokana na mchakato wa kitu chenye maumivu makubwa.
-
12:27 - 12:38Lakini hiyo ni kanuni ya maisha. Ni funzo la maisha.
-
12:38 - 12:48Kujisalimisha kwenye mchakato wa Mungu hakumaanishi kuondoa maumivu.
-
12:48 - 12:54Lakini maumivu yataisha (Yohanna 16:21).
-
12:54 - 13:00Watu wa Mungu, maumivu yataisha.
-
13:00 - 13:06Labda unatazama sasa hivi na kuna hali ya maumivu katika maisha yako.
-
13:06 - 13:11Maumivu ya mwili. Maumivu ya kihisia. Maumivu ya kiroho.
-
13:11 - 13:20Kama mtoto wa Mungu, maumivu yanaweza kuwa sehemu ya mchakato wa Mungu,
-
13:20 - 13:26lakini maumivu yataisha.
-
13:26 - 13:36Somo la maisha - ikiwa tutajaribu kuchukua njia fupi, kujaribu kuepuka mchakato,
-
13:36 - 13:41kujaribu kuharakisha wakati wa Mungu -
-
13:41 - 13:49tazama, ikiwa utaweza kuepukana na uchungu,
-
13:49 - 13:57usishangazwe kama utaepuka uzuri wake.
-
13:57 - 14:10Kwa sababu maumivu kwenye safari yanafanya mwisho wake kuwa mzuri zaidi.
-
14:10 - 14:18Pia nina neno la ushauri, watu wa Mungu,
-
14:18 - 14:23katika mwangaza wa uzoefu huu, katika siku chache zilizopita.
-
14:23 - 14:34Ikiwa tutatazama Maandiko, mfumo wa Mungu wa familia umeonyeshwa wazi.
-
14:34 - 14:39Tazama kile ambacho Maandiko yasema katika Mwanzo 1:28 na Mwanzo 2.
-
14:39 - 14:47Mfumo wa kimungu wa Mungu kwa familia, kwa ndoa umeonyeshwa wazi.
-
14:47 - 14:57Ni wazi kwamba wajibu wa kulea watoto unapaswa kubebwa ndani
-
14:57 - 15:08ya agano la ndoa ya kimungu.
-
15:08 - 15:18Ndio maana shetani anashughulikia kwa nguvu kushambulia nyumba, familia, na ndoa.
-
15:18 - 15:25Anataka kubadilisha mpango mkamilifu wa Mungu.
-
15:25 - 15:36Na athari za kuharibu mpango huu kwa kweli ni za vizazi.
-
15:36 - 15:47Lakini kumbuka - kukimbia kutoka kwenye wajibu ni sawa na kukimbia ukweli.
-
15:47 - 15:52Na ni mbio ambazo hutaweza kushinda kamwe.
-
15:52 - 15:56Kwa vijana wanaotazama sasa hivi -
-
15:56 - 16:03ukisema huko tayari kuwa na watoto, huko tayari kwa ndoa.
-
16:03 - 16:08Kama hauko tayari kwa ndoa, hauko tayari kwa ngono.
-
16:08 - 16:13Tafadhali uepuke uasherati.
-
16:13 - 16:20Kimbia mbali na uasherati.
-
16:20 - 16:33Ikiwa tutachochea 'upendo' kabla ya wakati wake, tutazindua tu tamaa.
-
16:33 - 16:40Kwa wale wanaomngojea Bwana kwa ajili ya ndoa - vema.
-
16:40 - 16:49Lakini usimsubiri tu Bwana. Hakikisha unasubiri ukiwa ndani ya Bwana.
-
16:49 - 16:55Kwa sababu wakati wa kusubiri si wakati wa kupoteza.
-
16:55 - 17:02Nidhamu inayohitajika
kukuhifadhi kwa ajili ya ndoa -
17:02 - 17:08pia unahitajika kukuweka ndani ya ndoa.
-
17:08 - 17:15Usipoteze kusubiri kwako.
-
17:15 - 17:27Masomo unayojifunza katika safari ya imani kwenye barabara kuelekea hatima yako
-
17:27 - 17:35yatakuendeleza wewe hadi kwenye hatua na kutoka kwenye hatua
-
17:35 - 17:42ambapo wakati sahihi utaleta mtu sahihi.
-
17:42 - 17:45Hili ni himizo kwa wale wanaotazama leo.
-
17:45 - 17:55Nina mengi ya kushiriki nanyi kuhusu mada hii baada ya niliyoyapitia siku chache zilizopita.
-
17:55 - 18:01Kuna mafunzo mengi ya kushiriki, lakini nitakomea hapa
-
18:01 - 18:11na kusema tu asante kwa watazamaji wote, marafiki, washirika, na wafuasi wa God's Heart TV.
-
18:11 - 18:15Asante kwa upendo wenu, sala zenu, msaada wenu, na motisha zenu.
-
18:15 - 18:23Na nakwambia hivi - kuwasili kwa Josiah kumeongeza tu hamu yetu
-
18:23 - 18:29kuendelea kueneza Habari Njema kwenye pembe nne za dunia,
-
18:29 - 18:37kuhubiri Habari Njema za Yesu Kristo kwa nguvu ya Roho Mtakatifu.
-
18:37 - 18:46Na hakuna njia bora kwangu kusema, 'Asante, Yesu', kwa zawadi hii ya thamani ya maisha
-
18:46 - 18:51kuliko kufanya kile Mungu ameniita nifanye.
-
18:51 - 18:56Hivi sasa nataka kukuombea kwa jina la Yesu.
-
18:57 - 19:06Hivi sasa, hebu tuombe kwa ajili ya wanandoa ambao wamejiunga pamoja nasi wakati huu
-
19:06 - 19:13wakiutafuta uso wa Mungu kwa ajili ya mtoto.
-
19:13 - 19:19Tumia kisa cha Josiah kama mahali pa mawasiliano.
-
19:19 - 19:24Wacha ushuhuda huu uwashe imani yako.
-
19:24 - 19:35Chukua nafasi hii kuweka hitaji juu ya upako.
-
19:35 - 19:45Kwanza kabisa, kumbuka hili - kiungo kikuu cha nyumba iliyo na amani ni moyo ulio na amani.
-
19:45 - 19:50Chochote kinachokusumbua moyo wako - Nasema, pata utulivu sasa hivi!
-
19:50 - 19:58Tulia katika jina kuu la Yesu Kristo!
-
19:58 - 20:06Ni kipi kimezuia uzazi wako?
-
20:06 - 20:22Kizuizi hicho kinachohusiana na kutopata mtoto - kiondolewe kwa jina kuu la Yesu!
-
20:22 - 20:30Kila roho ya kuharibika kwa mimba - Nasema, ondoka sasa hivi!
-
20:30 - 20:37Ondoka, katika jina kuu la Yesu!
-
20:37 - 20:44Adha gani hiyo inakatisha tamaa
juu ya wewe kuzaa matunda? -
20:44 - 20:45Je, ni uvimbe katika mfuko wa uzazi?
-
20:45 - 20:48Je, ni uvimbe wa ovari?
-
20:48 - 20:51Je, ni hesabu ya mbegu za kiume kuwa chini?
-
20:51 - 20:53Je, ni homoni kutokuwa sawa?
-
20:53 - 21:00Haijalishi ni kitu gani, kwa damu ya thamani ya Yesu Kristo, uponyaji upo.
-
21:00 - 21:02Ponywa katika tumbo lako!
-
21:02 - 21:04Ponywa katika viungo vyako!
-
21:04 - 21:06Ponywa katika mfumo wako!
-
21:06 - 21:10Pokea uponyaji katika jina kuu la Yesu!
-
21:10 - 21:18Pokea uzalishaji katika jina kuu la Yesu!
-
21:18 - 21:26Kila shambulio la kiroho dhidi ya nyumba yako, familia yako, ndoa yako -
-
21:26 - 21:34jinamizi hilo la ajabu, nasema liondoshwe!
-
21:34 - 21:36Uondolewe katika jina la Yesu.
-
21:36 - 21:42Jinamizi hilo katika hatua ya mafanikio ya kutafuta tunda la tumbo,
-
21:42 - 21:49ndoto hiyo mbaya - iondolewe,
katika jina kuu la Yesu. -
21:49 - 21:52Asante, Bwana.
-
21:52 - 21:58Nitaombea wazazi wanaotazama kipindi hiki.
-
21:58 - 22:09Kumbuka, kulea mtoto, kulea watoto ni kazi kutoka kwa Mungu.
-
22:09 - 22:20Naomba upokee nguvu kutoka juu ili uendelee kuzingatia kazi hiyo,
-
22:20 - 22:27kubaki na wajibu huo, kubaki gangari kwenye wajibu huo,
-
22:27 - 22:31katika jina kuu la Yesu.
-
22:31 - 22:40Je, una mtoto au watoto wenye tabia ya kuasi?
-
22:40 - 22:41Wacha niombee mtoto huyo.
-
22:41 - 22:44Wacha niombee watoto hao sasa hivi.
-
22:44 - 22:48Na kuwe na mabadiliko.
-
22:48 - 22:55Na kuwe na mabadiliko yasiyo ya kawaida kutoka ndani hadi nje!
-
22:55 - 23:04Pokea mabadiliko hayo katika jina kuu la Yesu.
-
23:04 - 23:12Kuchelewa kwa muujiza wa Hana ulikuwa tu maandalio
-
23:12 - 23:18Kwa mtoto wa ajabu wa ahadi kutoka juu.
-
23:18 - 23:27Watu wa Mungu, je, unakumbana na kuchelewa katika kutafuta mtoto?
-
23:27 - 23:34Usijaribu kukata tamaa kwa sababu ya kuchelewa.
-
23:34 - 23:40Usikate tamaa kwa sababu ya kuchelewa.
-
23:40 - 23:46Jazwa kustahimili!
-
23:46 - 23:56Jazwa kuvumulia bila uoga, katika jina kuu la Yesu!
-
23:56 - 24:04Ndio, najua kuna wale wanatazama sasa hivi ambao wako na uchungu.
-
24:04 - 24:11Uchungu wa kimwili, uchungu wa hisia, uchungu wa mawazo, uchungu wa kiroho.
-
24:11 - 24:17Kama mtoto wa Mungu, uchungu huo utapita.
-
24:17 - 24:32Kila roho nyuma ya huo uchungu - ondoka! Ondoka katika jina la Yesu!
-
24:32 - 24:38Kila aina ya uchungu - uchungu wa kimwili, uchungu wa kiroho, uchungu wa hisia -
-
24:38 - 24:43pokea uponyaji katika jina la Yesu!
-
24:43 - 24:58Pokea uponyaji kupitia damu ya thamana ya Yesu Kristo.
-
24:58 - 25:12Watu wa Mungu, mchakato wa Mungu hauwezi kuondoa maumivi.
-
25:12 - 25:15lakini maumivu yatapita.
-
25:15 - 25:21Nakuhakikishia - maumivu yatapita.
-
25:21 - 25:31Naomba sasa hivi upokee nguvu ya kustahimili bila kuingiza uoga.
-
25:31 - 25:36Usiruhusu sauti ya maumivu
kukupotosha kwenye hofu. -
25:36 - 25:49Pokea nguvu ya kustahimili katika jina la Yesu, ukijua maumivu yatapita.
-
25:49 - 25:57Kama vile kuwasili kwa Josiah kumeleta furaha, kama mtoto wa Mungu, furaha ni sehemu yako!
-
25:57 - 26:00Na kuwe na sherehe katika nyumba yako.
-
26:00 - 26:03Na kuwe na kushangilia katika familia yako.
-
26:03 - 26:12Na kuwe na ushuhuda wa kipekee katika nyumba yako katika jina kuu la Yesu.
-
26:12 - 26:22Asante, Yesu, kwa zawadi ya thamani ya uhai.
-
26:22 - 26:27Katika jina kuu la Yesu tunaomba, amina.
- Title:
- Barua Kwa Mwanangu Mpendwa!
- Description:
-
Josiah Timothy Tonge alizaliwa salama siku ya Alhamisi tarehe 29 Mei 2025. Sikia kutoka moyoni mwa Ndugu Chris katika barua hii kutoka kwa baba mpya kwenda kwa mwanawe mzaliwa wa kwanza! Asante, Yesu, kwa zawadi ya uhai.
- Video Language:
- English
- Team:
God's Heart TV
- Duration:
- 26:58
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for A Letter To My Precious Son! | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for A Letter To My Precious Son! | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for A Letter To My Precious Son! | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for A Letter To My Precious Son! | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for A Letter To My Precious Son! | |
![]() |
babubiko edited Swahili subtitles for A Letter To My Precious Son! | |
![]() |
babubiko edited Swahili subtitles for A Letter To My Precious Son! | |
![]() |
babubiko edited Swahili subtitles for A Letter To My Precious Son! |