< Return to Video

Barua Kwa Mwanangu Mpendwa!

  • 0:00 - 0:10
    Barua kwa mwanangu, Josiah Timothy Tonge.
  • 0:10 - 0:19
    Mpendwa Josiah, ninapokushika mikononi mwangu
    kama baba wa mara ya kwanza,
  • 0:19 - 0:24
    Nimepigwa na ukumbusho mtakatifu.
  • 0:24 - 0:32
    Wewe ni wetu wa kushikilia, sio wetu kumiliki.
  • 0:32 - 0:40
    Wewe ni zawadi kutoka kwa Mungu, uliofumwa kiustadi na Mbuni wa Kimungu,
  • 0:40 - 0:49
    umesanifiwa mahali pa siri kwa mikono ile ile iliyopanga nyota angani.
  • 0:49 - 1:01
    Zawadi ya thamani iliyokabidhiwa kwetu -
    kwa msimu, kwa sababu.
  • 1:01 - 1:07
    Na katika dhamana hiyo kuna uzito mtakatifu
    wa utumishi -
  • 1:07 - 1:18
    kuuchunga moyo wako kuelekea
    Yule aliyepulizia uhai ndani yake,
  • 1:18 - 1:25
    ambaye alama za vidole vyake
    zipo katika kila nyuzi ya nafsi yako.
  • 1:25 - 1:33
    Kupenda kwa dhati, lakini kushikilia kwa uhuru -
  • 1:33 - 1:44
    imara vya kutosha katika kusaidia kukua
    lakini legevu vya kutosha kuachilia.
  • 1:44 - 1:55
    Kwa maana sio uimara wa kushikilia kwetu,
    bali utimilifu wa ukuaji wako.
  • 1:55 - 2:05
    Na upendo wa kweli hujiandaa kuondoka.
  • 2:05 - 2:16
    Kwa hivyo ninakubeba kwa uangalifu na ufahamu wa Yule anayetubeba sisi sote.
  • 2:16 - 2:23
    Upitapo kutoka tumboni hadi
    kwenye ulimwengu uliokaribia,
  • 2:23 - 2:28
    kulikuwa na maswali mengi ambayo yalizunguka kichwani mwangu.
  • 2:28 - 2:35
    Lakini sauti ya kilio chako cha kwanza
    ikayanyamazisha yote.
  • 2:35 - 2:39
    Ilikuwa ni ufunuo rahisi.
  • 2:39 - 2:46
    Kinachohitajika kwa kazi
    tayari kiko ndani,
  • 2:46 - 2:56
    kwa maana hakuna kazi ya kimungu inayokuja
    bila mgawo wa kimungu.
  • 2:56 - 3:06
    Kwa kweli, Yosia, ujio wako uliamsha sehemu yangu ambayo ilikuwa imelala,
  • 3:06 - 3:16
    kwa maana hakuna wajibu mtakatifu zaidi kama jukumu la kumlea mtoto katika kumcha Bwana.
  • 3:16 - 3:23
    Ndiyo, Yosia, umeingia
    ulimwengu uliojaa mashaka.
  • 3:23 - 3:31
    Lakini kuna jambo moja unaweza kuwa na uhakika nalo - hiyo ni nafasi yako katika mioyo yetu.
  • 3:31 - 3:41
    Hatuna uwezo wa kuamua nini kinakungoja wewe, Yosia, katika safari hii ya maisha.
  • 3:41 - 3:51
    Lakini maadamu Mungu anatupa pumzi kwenye mapafu yetu, mimi na mama yako tutatembea nawe.
  • 3:51 - 3:57
    Pale maisha yatakapojaribu kukuangusha,
    tutakusaidia kusimama.
  • 3:57 - 4:05
    Wakati usiku unahisi kuwa mrefu na wenye upweke,
    tutakaa nawe mpaka kutakapopambazuka.
  • 4:05 - 4:17
    Wakati maono yanaonekana kutoeleweka, tutakuelekeza kwa maombi kuelekea kusudi lako.
  • 4:17 - 4:27
    Wakati mstari kati ya tumaini na kukata tamaa haunoekani wazi,
  • 4:27 - 4:36
    tutakuwa ishara kwa Mmoja pekee ambaye hawezi kamwe kukukatisha tamaa.
  • 4:36 - 4:40
    Na wakati ulimwengu utajaribu
    kuhoji utambulisho wako,
  • 4:40 - 4:47
    tutakukumbusha wewe ni nani -
    mtoto wa ahadi.
  • 4:47 - 4:56
    Tutakukumbusha wewe ni nani - iwe kwa kutia moyo kwa upole au kemeo kali.
  • 4:56 - 5:07
    Tutakulea na kukulisha kwa yote ambayo Mungu ametupa,
  • 5:07 - 5:12
    tukijua hilo wakati sisi
    tukitunza lishe,
  • 5:12 - 5:18
    Anatunza kustawi.
  • 5:18 - 5:39
    Thamani halisi ya zawadi za Mungu inategemea uwezo wetu wa kuzirejesha kwake.
  • 5:39 - 5:47
    Josiah, naomba siku moja, utasoma maneno haya
  • 5:47 - 5:54
    na upate ndani yake ujasiri wa kukabiliana na dhoruba zako mwenyewe kwa imani,
  • 5:54 - 6:00
    kujua kwamba Yule aliye kuumba anaenda mbele yako.
  • 6:00 - 6:06
    Kumbuka yule wajina lako,
  • 6:06 - 6:15
    mfalme katika 2 Mambo ya Nyakati 34 aliyemtafuta Mungu kwa moyo wake akiwa na umri mdogo
  • 6:15 - 6:24
    na kuona vyema - vyema sana kiasi kwamba nguvu ya utawala wa kifalme wa kidunia
  • 6:24 - 6:29
    haikuathiri usafi wa uwana wa kiroho.
  • 6:29 - 6:38
    Mtu ambaye shauku yake kwa Neno la Mungu haikuwa ya kupita.
  • 6:38 - 6:50
    lakini ilipita kwenye vitendo na dhamira ambazo ziliishi zaidi ya maisha yake.
  • 6:50 - 6:55
    Tukio lake likupe motisha.
  • 6:55 - 7:07
    Na maisha yetu yawe mafundisho ya viwango tunavyotafuta kuviweka.
  • 7:07 - 7:14
    Kwa kuwa Wakristo, tunajitahidi kuelekea ukamilifu.
  • 7:14 - 7:26
    kutoka mahali pa kujisalimisha kwa Yule anayetukamilisha.
  • 7:26 - 7:40
    Josiah, ni furaha yetu, haki yetu, heshima yetu kukuwasilisha kwa Mungu Aliye Juu Sana.
  • 7:40 - 7:47
    na katika uwepo wake, natangaza baraka hizi juu yako
  • 7:47 - 7:54
    kulingana na Hesabu 6:24-26.
  • 7:54 - 8:02
    Josiah, BWANA akubarikie, na kukilinda
  • 8:02 - 8:11
    BWANA akuangazie nuru za uso wake, na kukufadhili;
  • 8:11 - 8:21
    BWANA akuinulie uso wake, na kukupa amani.
  • 8:21 - 8:35
    Katika jina kuu la YESU, Amina!
  • 8:35 - 8:39
    Mwanangu, nakupenda kwa moyo wangu wote.
  • 8:39 - 8:46
    Asante kwa kuniongoza kutoka kuwa ndugu hadi kuwa baba.
  • 8:46 - 8:55
    Juu ya yote, naomba ukuwe katika upendo kwa Yesu Kristo,
  • 8:55 - 9:03
    kwa moyo wako wote, akili, roho, nafsi na nguvu.
  • 9:03 - 9:12
    Kwa maana hiyo ni msingi thabiti ambao kila kitu kingine kinatoka.
  • 9:12 - 9:16
    Kwa upendo kutoka kwa baba yako.
  • 9:16 - 9:25
    P.S. - Natumai utakua na uweza wa kucheza kama mama yako, si kama baba yako!
  • 9:25 - 9:28
    Katika jina la Yesu.
  • 9:31 - 9:40
    Neema na amani kwenu nyote, watu wa Mungu, katika jina kubwa la Yesu Kristo.
  • 9:40 - 9:46
    Kuna matukio mawili katika maisha
  • 9:46 - 9:55
    ambayo yanatoa fursa isiyoweza kuepukwa ya kuamka kiroho -
  • 9:55 - 10:05
    kuona mwanzo wa maisha na kuona mwisho wa maisha.
  • 10:05 - 10:13
    Siwezi kufikiria jinsi inavyowezekana mtu kuona
  • 10:13 - 10:19
    kuibuka au kuondoka kwa maisha,
  • 10:19 - 10:29
    bila kufikiria kwa undani juu ya maana ya maisha, juu ya kile maisha yanahusisha kweli.
  • 10:29 - 10:35
    Ninashiriki hili nawe leo, kwa sababu siku chache zilizopita za maisha yangu
  • 10:35 - 10:42
    hakika zimekuwa miongoni mwa matukio ya kukumbukwa, ya ajabu, yenye unyenyekevu,
  • 10:42 - 10:47
    ya changamoto, kuchoka katika maisha yangu-
  • 10:47 - 10:56
    kuwa na fursa ya kushuhudia kuwasili kwa mtoto wetu wa kwanza, Josiah,
  • 10:56 - 11:03
    mnamo Alhamisi, tarehe 29 Mei, 2025.
  • 11:03 - 11:07
    Kwanza kabisa - utukufu kwa Mungu!
  • 11:07 - 11:12
    Asante Yesu kwa zawadi zzuri ya maisha.
  • 11:12 - 11:17
    Nataka pia kumpongeza mke wangu, Allison,
  • 11:17 - 11:22
    na kwa kweli, nataka kuwapongeza akina mama duniani kote.
  • 11:22 - 11:30
    Ninasifu uvumilivu wenu, ustahimilivu, na imani yenu inapohusiana na kuzaa. Wow!
  • 11:30 - 11:37
    Na neno la ushauri kwa waume ambao huenda wananitazama sasa hivi.
  • 11:37 - 11:50
    Wakati mkeo anapojifungua, simama pamoja naye katika maombi.
  • 11:50 - 11:58
    Kaa karibu na yeye kimwili na simama wima na yeye kiroho.
  • 11:58 - 12:09
    Kuwa sauti ya utulivu na nanga ya amani katika bahari ya maumivu.
  • 12:09 - 12:14
    Hii ni siri. Ni siri, ndugu zangu na dada zangu katika Kristo -
  • 12:14 - 12:27
    jinsi kitu kizuri namna hiyo kinavyotokana na mchakato wa kitu chenye maumivu makubwa.
  • 12:27 - 12:38
    Lakini hiyo ni kanuni ya maisha. Ni funzo la maisha.
  • 12:38 - 12:48
    Kujisalimisha kwenye mchakato wa Mungu hakumaanishi kuondoa maumivu.
  • 12:48 - 12:54
    Lakini maumivu yataisha (Yohanna 16:21).
  • 12:54 - 13:00
    Watu wa Mungu, maumivu yataisha.
  • 13:00 - 13:06
    Labda unatazama sasa hivi na kuna hali ya maumivu katika maisha yako.
  • 13:06 - 13:11
    Maumivu ya mwili. Maumivu ya kihisia. Maumivu ya kiroho.
  • 13:11 - 13:20
    Kama mtoto wa Mungu, maumivu yanaweza kuwa sehemu ya mchakato wa Mungu,
  • 13:20 - 13:26
    lakini maumivu yataisha.
  • 13:26 - 13:36
    Somo la maisha - ikiwa tutajaribu kuchukua njia fupi, kujaribu kuepuka mchakato,
  • 13:36 - 13:41
    kujaribu kuharakisha wakati wa Mungu -
  • 13:41 - 13:49
    tazama, ikiwa utaweza kuepukana na uchungu,
  • 13:49 - 13:57
    usishangazwe kama utaepuka uzuri wake.
  • 13:57 - 14:10
    Kwa sababu maumivu kwenye safari yanafanya mwisho wake kuwa mzuri zaidi.
  • 14:10 - 14:18
    Pia nina neno la ushauri, watu wa Mungu,
  • 14:18 - 14:23
    katika mwangaza wa uzoefu huu, katika siku chache zilizopita.
  • 14:23 - 14:34
    Ikiwa tutatazama Maandiko, mfumo wa Mungu wa familia umeonyeshwa wazi.
  • 14:34 - 14:39
    Tazama kile ambacho Maandiko yasema katika Mwanzo 1:28 na Mwanzo 2.
  • 14:39 - 14:47
    Mfumo wa kimungu wa Mungu kwa familia, kwa ndoa umeonyeshwa wazi.
  • 14:47 - 14:57
    Ni wazi kwamba wajibu wa kulea watoto unapaswa kubebwa ndani
  • 14:57 - 15:08
    ya agano la ndoa ya kimungu.
  • 15:08 - 15:18
    Ndio maana shetani anashughulikia kwa nguvu kushambulia nyumba, familia, na ndoa.
  • 15:18 - 15:25
    Anataka kubadilisha mpango mkamilifu wa Mungu.
  • 15:25 - 15:36
    Na athari za kuharibu mpango huu kwa kweli ni za vizazi.
  • 15:36 - 15:47
    Lakini kumbuka - kukimbia kutoka kwenye wajibu ni sawa na kukimbia ukweli.
  • 15:47 - 15:52
    Na ni mbio ambazo hutaweza kushinda kamwe.
  • 15:52 - 15:56
    Kwa vijana wanaotazama sasa hivi -
  • 15:56 - 16:03
    ukisema huko tayari kuwa na watoto, huko tayari kwa ndoa.
  • 16:03 - 16:08
    Kama hauko tayari kwa ndoa, hauko tayari kwa ngono.
  • 16:08 - 16:13
    Tafadhali uepuke uasherati.
  • 16:13 - 16:20
    Kimbia mbali na uasherati.
  • 16:20 - 16:33
    Ikiwa tutachochea 'upendo' kabla ya wakati wake, tutazindua tu tamaa.
  • 16:33 - 16:40
    Kwa wale wanaomngojea Bwana kwa ajili ya ndoa - vema.
  • 16:40 - 16:49
    Lakini usimsubiri tu Bwana. Hakikisha unasubiri ukiwa ndani ya Bwana.
  • 16:49 - 16:55
    Kwa sababu wakati wa kusubiri si wakati wa kupoteza.
  • 16:55 - 17:02
    Nidhamu inayohitajika
    kukuhifadhi kwa ajili ya ndoa
  • 17:02 - 17:08
    pia unahitajika kukuweka ndani ya ndoa.
  • 17:08 - 17:15
    Usipoteze kusubiri kwako.
  • 17:15 - 17:27
    Masomo unayojifunza katika safari ya imani kwenye barabara kuelekea hatima yako
  • 17:27 - 17:35
    yatakuendeleza wewe hadi kwenye hatua na kutoka kwenye hatua
  • 17:35 - 17:42
    ambapo wakati sahihi utaleta mtu sahihi.
  • 17:42 - 17:45
    Hili ni himizo kwa wale wanaotazama leo.
  • 17:45 - 17:55
    Nina mengi ya kushiriki nanyi kuhusu mada hii baada ya niliyoyapitia siku chache zilizopita.
  • 17:55 - 18:01
    Kuna mafunzo mengi ya kushiriki, lakini nitakomea hapa
  • 18:01 - 18:11
    na kusema tu asante kwa watazamaji wote, marafiki, washirika, na wafuasi wa God's Heart TV.
  • 18:11 - 18:15
    Asante kwa upendo wenu, sala zenu, msaada wenu, na motisha zenu.
  • 18:15 - 18:23
    Na nakwambia hivi - kuwasili kwa Josiah kumeongeza tu hamu yetu
  • 18:23 - 18:29
    kuendelea kueneza Habari Njema kwenye pembe nne za dunia,
  • 18:29 - 18:37
    kuhubiri Habari Njema za Yesu Kristo kwa nguvu ya Roho Mtakatifu.
  • 18:37 - 18:46
    Na hakuna njia bora kwangu kusema, 'Asante, Yesu', kwa zawadi hii ya thamani ya maisha
  • 18:46 - 18:51
    kuliko kufanya kile Mungu ameniita nifanye.
  • 18:51 - 18:56
    Hivi sasa nataka kukuombea kwa jina la Yesu.
  • 18:57 - 19:06
    Hivi sasa, hebu tuombe kwa ajili ya wanandoa ambao wamejiunga pamoja nasi wakati huu
  • 19:06 - 19:13
    wakiutafuta uso wa Mungu kwa ajili ya mtoto.
  • 19:13 - 19:19
    Tumia kisa cha Josiah kama mahali pa mawasiliano.
  • 19:19 - 19:24
    Wacha ushuhuda huu uwashe imani yako.
  • 19:24 - 19:35
    Chukua nafasi hii kuweka hitaji juu ya upako.
  • 19:35 - 19:45
    Kwanza kabisa, kumbuka hili - kiungo kikuu cha nyumba iliyo na amani ni moyo ulio na amani.
  • 19:45 - 19:50
    Chochote kinachokusumbua moyo wako - Nasema, pata utulivu sasa hivi!
  • 19:50 - 19:58
    Tulia katika jina kuu la Yesu Kristo!
  • 19:58 - 20:06
    Ni kipi kimezuia uzazi wako?
  • 20:06 - 20:22
    Kizuizi hicho kinachohusiana na kutopata mtoto - kiondolewe kwa jina kuu la Yesu!
  • 20:22 - 20:30
    Kila roho ya kuharibika kwa mimba - Nasema, ondoka sasa hivi!
  • 20:30 - 20:37
    Ondoka, katika jina kuu la Yesu!
  • 20:37 - 20:44
    Adha gani hiyo inakatisha tamaa
    juu ya wewe kuzaa matunda?
  • 20:44 - 20:45
    Je, ni uvimbe katika mfuko wa uzazi?
  • 20:45 - 20:48
    Je, ni uvimbe wa ovari?
  • 20:48 - 20:51
    Je, ni hesabu ya mbegu za kiume kuwa chini?
  • 20:51 - 20:53
    Je, ni homoni kutokuwa sawa?
  • 20:53 - 21:00
    Haijalishi ni kitu gani, kwa damu ya thamani ya Yesu Kristo, uponyaji upo.
  • 21:00 - 21:02
    Ponywa katika tumbo lako!
  • 21:02 - 21:04
    Ponywa katika viungo vyako!
  • 21:04 - 21:06
    Ponywa katika mfumo wako!
  • 21:06 - 21:10
    Pokea uponyaji katika jina kuu la Yesu!
  • 21:10 - 21:18
    Pokea uzalishaji katika jina kuu la Yesu!
  • 21:18 - 21:26
    Kila shambulio la kiroho dhidi ya nyumba yako, familia yako, ndoa yako -
  • 21:26 - 21:34
    jinamizi hilo la ajabu, nasema liondoshwe!
  • 21:34 - 21:36
    Uondolewe katika jina la Yesu.
  • 21:36 - 21:42
    Jinamizi hilo katika hatua ya mafanikio ya kutafuta tunda la tumbo,
  • 21:42 - 21:49
    ndoto hiyo mbaya - iondolewe,
    katika jina kuu la Yesu.
  • 21:49 - 21:52
    Asante, Bwana.
  • 21:52 - 21:58
    Nitaombea wazazi wanaotazama kipindi hiki.
  • 21:58 - 22:09
    Kumbuka, kulea mtoto, kulea watoto ni kazi kutoka kwa Mungu.
  • 22:09 - 22:20
    Naomba upokee nguvu kutoka juu ili uendelee kuzingatia kazi hiyo,
  • 22:20 - 22:27
    kubaki na wajibu huo, kubaki gangari kwenye wajibu huo,
  • 22:27 - 22:31
    katika jina kuu la Yesu.
  • 22:31 - 22:40
    Je, una mtoto au watoto wenye tabia ya kuasi?
  • 22:40 - 22:41
    Wacha niombee mtoto huyo.
  • 22:41 - 22:44
    Wacha niombee watoto hao sasa hivi.
  • 22:44 - 22:48
    Na kuwe na mabadiliko.
  • 22:48 - 22:55
    Na kuwe na mabadiliko yasiyo ya kawaida kutoka ndani hadi nje!
  • 22:55 - 23:04
    Pokea mabadiliko hayo katika jina kuu la Yesu.
  • 23:04 - 23:12
    Kuchelewa kwa muujiza wa Hana ulikuwa tu maandalio
  • 23:12 - 23:18
    Kwa mtoto wa ajabu wa ahadi kutoka juu.
  • 23:18 - 23:27
    Watu wa Mungu, je, unakumbana na kuchelewa katika kutafuta mtoto?
  • 23:27 - 23:34
    Usijaribu kukata tamaa kwa sababu ya kuchelewa.
  • 23:34 - 23:40
    Usikate tamaa kwa sababu ya kuchelewa.
  • 23:40 - 23:46
    Jazwa kustahimili!
  • 23:46 - 23:56
    Jazwa kuvumulia bila uoga, katika jina kuu la Yesu!
  • 23:56 - 24:04
    Ndio, najua kuna wale wanatazama sasa hivi ambao wako na uchungu.
  • 24:04 - 24:11
    Uchungu wa kimwili, uchungu wa hisia, uchungu wa mawazo, uchungu wa kiroho.
  • 24:11 - 24:17
    Kama mtoto wa Mungu, uchungu huo utapita.
  • 24:17 - 24:32
    Kila roho nyuma ya huo uchungu - ondoka! Ondoka katika jina la Yesu!
  • 24:32 - 24:38
    Kila aina ya uchungu - uchungu wa kimwili, uchungu wa kiroho, uchungu wa hisia -
  • 24:38 - 24:43
    pokea uponyaji katika jina la Yesu!
  • 24:43 - 24:58
    Pokea uponyaji kupitia damu ya thamana ya Yesu Kristo.
  • 24:58 - 25:12
    Watu wa Mungu, mchakato wa Mungu hauwezi kuondoa maumivi.
  • 25:12 - 25:15
    lakini maumivu yatapita.
  • 25:15 - 25:21
    Nakuhakikishia - maumivu yatapita.
  • 25:21 - 25:31
    Naomba sasa hivi upokee nguvu ya kustahimili bila kuingiza uoga.
  • 25:31 - 25:36
    Usiruhusu sauti ya maumivu
    kukupotosha kwenye hofu.
  • 25:36 - 25:49
    Pokea nguvu ya kustahimili katika jina la Yesu, ukijua maumivu yatapita.
  • 25:49 - 25:57
    Kama vile kuwasili kwa Josiah kumeleta furaha, kama mtoto wa Mungu, furaha ni sehemu yako!
  • 25:57 - 26:00
    Na kuwe na sherehe katika nyumba yako.
  • 26:00 - 26:03
    Na kuwe na kushangilia katika familia yako.
  • 26:03 - 26:12
    Na kuwe na ushuhuda wa kipekee katika nyumba yako katika jina kuu la Yesu.
  • 26:12 - 26:22
    Asante, Yesu, kwa zawadi ya thamani ya uhai.
  • 26:22 - 26:27
    Katika jina kuu la Yesu tunaomba, amina.
Title:
Barua Kwa Mwanangu Mpendwa!
Description:

Josiah Timothy Tonge alizaliwa salama siku ya Alhamisi tarehe 29 Mei 2025. Sikia kutoka moyoni mwa Ndugu Chris katika barua hii kutoka kwa baba mpya kwenda kwa mwanawe mzaliwa wa kwanza! Asante, Yesu, kwa zawadi ya uhai.

more » « less
Video Language:
English
Team:
God's Heart TV
Duration:
26:58

Swahili subtitles

Revisions Compare revisions