< Return to Video

Barua Kwa Mwanangu Mpendwa!

  • 0:00 - 0:10
    Barua kwa mwanangu, Josiah Timothy Tonge.
  • 0:10 - 0:19
    Mpendwa Josiah, ninapokushika mikononi mwangu
    kama baba wa mara ya kwanza,
  • 0:19 - 0:24
    Nimepigwa na ukumbusho mtakatifu.
  • 0:24 - 0:32
    Wewe ni wetu wa kushikilia, sio wetu kumiliki.
  • 0:32 - 0:40
    Wewe ni zawadi kutoka kwa Mungu, uliofumwa kiustadi na Mbuni wa Kimungu,
  • 0:40 - 0:49
    umesanifiwa mahali pa siri kwa mikono ile ile iliyotupa nyota angani.
  • 0:49 - 1:01
    Zawadi ya thamani iliyokabidhiwa kwetu -
    kwa msimu, kwa sababu.
  • 1:01 - 1:07
    Na katika amana hiyo kuna uzito mtakatifu
    wa uwakili -
  • 1:07 - 1:18
    kuuchunga moyo wako kuelekea
    Yule aliyepulizia uhai ndani yake,
  • 1:18 - 1:25
    ambaye alama zake za vidole
    kila nyuzi ya nafsi yako.
  • 1:25 - 1:33
    Kupenda kwa dhati, lakini kushikilia kwa uhuru -
  • 1:33 - 1:44
    kusongwa ya kutosha kusaidia kukua
    lakini nyepesi vya kutosha kuachilia.
  • 1:44 - 1:55
    Kwa maana sio uimara wa kushikilia kwetu,
    bali utimilifu wa ukuaji wako.
  • 1:55 - 2:05
    Na upendo wa kweli hujiandaa kuondoka.
  • 2:05 - 2:16
    Kwa hivyo ninakubeba kwa uangalifu na ufahamu wa Yule anayetubeba sisi sote.
  • 2:16 - 2:23
    Upitapo kutoka tumboni hadi
    kwa ulimwengu uliokaribia,
  • 2:23 - 2:28
    kulikuwa na maswali mengi ambayo yalizunguka kichwani mwangu.
  • 2:28 - 2:35
    Lakini sauti ya kilio chako cha kwanza
    ikayanyamazisha yote.
  • 2:35 - 2:39
    Ilikuwa ni ufunuo rahisi.
  • 2:39 - 2:46
    Kinachohitajika kwa kazi
    tayari kiko ndani,
  • 2:46 - 2:56
    kwa maana hakuna kazi ya kimungu inayokuja
    bila mgawo wa kimungu.
  • 2:56 - 3:06
    Kwa kweli, Yosia, kuja wako uliamsha sehemu yangu ambayo ilikuwa imelala,
  • 3:06 - 3:16
    kwa maana hakuna wajibu mtakatifu zaidi kama jukumu la kumlea mtoto katika kumcha Bwana.
  • 3:16 - 3:23
    Ndiyo, Yosia, umeingia
    ulimwengu uliojaa mashaka.
  • 3:23 - 3:31
    Lakini kuna jambo moja unaweza kuwa na uhakika nalo - hiyo ni nafasi yako katika mioyo yetu.
  • 3:31 - 3:41
    Hatuna uwezo wa kuamua nini kinakungoja wewe, Yosia, katika safari hii ya maisha.
  • 3:41 - 3:51
    Lakini maadamu Mungu anatupa pumzi kwenye mapafu yetu, mimi na mama yako tutatembea nawe.
  • 3:51 - 3:57
    Wakati maisha itajaribu kukuangusha,
    tutakusaidia kusimama.
  • 3:57 - 4:05
    Wakati usiku unahisi kuwa mrefu na wenye upweke,
    tutakaa nawe mpaka kutakapopambazuka.
  • 4:05 - 4:17
    Wakati maono yanaonekana kutoeleweka, tutakuelekeza kwa maombi kuelekea kusudi lako.
  • 4:17 - 4:27
    Wakati mstari kati ya tumaini na kukata tamaa haunoekani wazi,
  • 4:27 - 4:36
    tutakuwa ishara kwa Mmoja pekee ambaye hawezi kamwe kukukatisha tamaa.
  • 4:36 - 4:40
    Na wakati ulimwengu utajaribu
    kuhoji utambulisho wako,
  • 4:40 - 4:47
    tutakukumbusha wewe ni nani -
    mtoto wa ahadi.
  • 4:47 - 4:56
    Tutakukumbusha wewe ni nani - iwe kwa kutia moyo kwa upole au kemeo kali.
  • 4:56 - 5:07
    Tutakulea na kukulisha kwa yote ambayo Mungu ametupa,
  • 5:07 - 5:12
    tukijua hilo wakati sisi
    tukitunza lishe,
  • 5:12 - 5:18
    Anatunza kustawi.
  • 5:18 - 5:39
    Thamani halisi ya zawadi za Mungu inategemea uwezo wetu wa kuzirejesha kwake.
  • 5:39 - 5:47
    Josiah, naomba siku moja, utasoma maneno haya
  • 5:47 - 5:54
    na upate ndani yao ujasiri wa kukabiliana na dhoruba zako mwenyewe kwa imani,
  • 5:54 - 6:00
    kujua kwamba Yule aliye kuumba anaenda mbele yako.
  • 6:00 - 6:06
    Kumbuka ni nani unayeitwa baada yake,
  • 6:06 - 6:15
    mfalme katika 2 Mambo ya Nyakati 34 aliyemtafuta Mungu kwa moyo wake akiwa na umri mdogo
  • 6:15 - 6:24
    na kuona vyema - vyema sana kiasi kwamba nguvu ya utawala wa kifalme wa kidunia
  • 6:24 - 6:29
    haikuathiri usafi wa uwana wa kiroho.
  • 6:29 - 6:38
    Mtu ambaye shauku yake kwa Neno la Mungu haikuwa ya kupita.
  • 6:38 - 6:50
    lakini ilipita kwenye vitendo na dhamira ambazo ziliishi zaidi ya maisha yake.
  • 6:50 - 6:55
    Tukio lake likupe motisha.
  • 6:55 - 7:07
    Na maisha yetu yawe mafundisho ya viwango tunavyotafuta kuweka.
  • 7:07 - 7:14
    Kwa kuwa Wakristo, tunajitahidi kuelekea ukamilifu.
  • 7:14 - 7:26
    kutoka mahali pa kujisalimisha kwa Yule anayetukamilisha.
  • 7:26 - 7:40
    Josiah, ni furaha yetu, haki yetu, heshima yetu kukuwasilisha kwa Mungu Aliye Juu Sana.
  • 7:40 - 7:47
    na katika uwepo wake, natangaza baraka hizi juu yako
  • 7:47 - 7:54
    kulingana na Hesabu 6:24-26.
  • 7:54 - 8:02
    Josiah, BWANA akubarikie, na kukilinda
  • 8:02 - 8:11
    BWANA akuangazie nuruza uso wake, na kukufadhili;
  • 8:11 - 8:21
    BWANA akuinulie uso wake, na kukupa amani.
  • 8:21 - 8:35
    Katika jina kuu la YESU, Amina!
  • 8:35 - 8:39
    Mwanangu, nakupenda kwa moyo wangu wote.
  • 8:39 - 8:46
    Asante kwa kuniongoza kutoka kwa ndugu hadi baba.
  • 8:46 - 8:55
    Juu ya yote, naomba ukuwe katika upendo kwa Yesu Kristo,
  • 8:55 - 9:03
    kwa moyo wako wote, akili, roho, nafsi na nguvu.
  • 9:03 - 9:12
    Kwa maana hiyo ni msingi thabiti ambao kila kitu kingine kinatoka.
  • 9:12 - 9:16
    Kwa upendo kutoka kwa baba yako.
  • 9:16 - 9:25
    P.S. - Natumai utakua na uweza wa kucheza kama mama yako, si kama baba yako!
  • 9:25 - 9:28
    Katika jina la Yesu.
  • 9:31 - 9:40
    Neema na amani kwenu nyote, watu wa Mungu, katika jina kubwa la Yesu Kristo.
  • 9:40 - 9:46
    Kuna matukio mawili katika maisha
  • 9:46 - 9:55
    ambayo inatoa fursa isiyoweza kuepukwa ya kuamka kiroho -
  • 9:55 - 10:05
    kuona mwanzo wa maisha na kuona mwisho wa maisha.
  • 10:05 - 10:13
    Siwezi kufikiria jinsi inavyowezekana mtu kuona
  • 10:13 - 10:19
    kuibuka au kuondoka kwa maisha,
  • 10:19 - 10:29
    bila kufikiria kwa undani juu ya maana ya maisha, juu ya kile maisha yanahusisha kweli.
  • 10:29 - 10:35
    Ninashiriki hii nawe leo, kwa sababu siku chache zilizopita za maisha yangu
  • 10:35 - 10:42
    hakika zimekuwa miongoni mwa matukio ya kukumbukwa, ya ajabu, yenye unyenyekevu,
  • 10:42 - 10:47
    ya changamoto, kuchoka katika maisha yangu-
  • 10:47 - 10:56
    kuwa na fursa ya kushuhudia kuwasili kwa mtoto wetu wa kwanza, Josiah,
  • 10:56 - 11:03
    mnamo Alhamisi, tarehe 29 Mei, 2025.
  • 11:03 - 11:07
    Kwanza kabisa - utukufu kwa Mungu!
  • 11:07 - 11:12
    Asante Yesu kwa zawadi zzuri ya maisha.
  • 11:12 - 11:17
    Nataka pia kumpongeza mke wangu, Allison,
  • 11:17 - 11:22
    na kwa kweli, nataka kuwapongeza akina mama duniani kote.
  • 11:22 - 11:30
    Ninasifu uvumilivu wenu, ustahimilivu, na imani yenu inapohusiana na kuzaa. Wow!
  • 11:30 - 11:37
    Na neno la ushauri kwa waume ambao huenda wananitazama sasa hivi.
  • 11:37 - 11:50
    Wakati mkeo anapojifungua, simama pamoja naye katika maombi.
  • 11:50 - 11:58
    Kaa karibu na yeye kimwili na simama wima na yeye kiroho.
  • 11:58 - 12:09
    Kuwa sauti ya utulivu na kiambuga cha amani katika bahari ya maumivu.
  • 12:09 - 12:14
    Hii ni siri. Ni siri, ndugu zangu na dada zangu katika Kristo -
  • 12:14 - 12:27
    jinsi kitu kizuri namna hiyo kinavyotokana na mchakato wa kitu chenye maumivu makubwa.
  • 12:27 - 12:38
    Lakini hiyo ni kanuni ya maisha. Ni funzo la maisha.
  • 12:38 - 12:48
    Kujisalimisha kwa mchakato wa Mungu hakumaanishi kuondoa maumivu.
  • 12:48 - 12:54
    Lakini maumivu yataisha (Yohanna 16:21).
  • 12:54 - 13:00
    Watu wa Mungu, maumivu yataisha.
  • 13:00 - 13:06
    Labda unatazama sasa hivi na kuna hali ya maumivu katika maisha yako.
  • 13:06 - 13:11
    Maumivu ya mwili. Maumivu ya kihisia. Maumivu ya kiroho.
  • 13:11 - 13:20
    Kama mtoto wa Mungu, maumivu yanaweza kuwa sehemu ya mchakato wa Mungu,
  • 13:20 - 13:26
    lakini maumivu yataisha.
  • 13:26 - 13:36
    Somo la maisha - ikiwa tutajaribu kuchukua njia fupi, kujaribu kuepuka mchakato,
  • 13:36 - 13:41
    kujaribu kuharakisha wakati wa Mungu -
  • 13:41 - 13:49
    tazama, ikiwa utaweza kuepukana na uchungu,
  • 13:49 - 13:57
    usishangazwe kama utaepuka uzuri wake.
  • 13:57 - 14:10
    Kwa sababu maumivu kwenye safari yanafanya mwisho wake kuwa mzuri zaidi.
  • 14:10 - 14:18
    Pia nina neno la ushauri, watu wa Mungu,
  • 14:18 - 14:23
    katika mwangaza wa uzoefu huu, katika siku chache zilizopita.
  • 14:23 - 14:34
    Ikiwa tutatazama Maandiko, mfumo wa Mungu wa familia umeonyeshwa wazi.
  • 14:34 - 14:39
    Tazama kile ambacho Maandiko yasema katika Mwanzo 1:28 na Mwanzo 2.
  • 14:39 - 14:47
    Mfumo wa kimungu wa Mungu kwa familia, kwa ndoa umeonyeshwa wazi.
  • 14:47 - 14:57
    Ni wazi kwamba wajibu wa kulea watoto unapaswa kubebwa ndani
  • 14:57 - 15:08
    agano la ndoa ya kimungu.
  • 15:08 - 15:18
    Ndio maana shetani anashughulikia kwa nguvu kushambulia nyumba, familia, na ndoa.
  • 15:18 - 15:25
    Anataka kubadilisha mpango mkamilifu wa Mungu.
  • 15:25 - 15:36
    Na matokeo ya kuharibu mpango huu kwa kweli ni ya vizazi.
  • 15:36 - 15:47
    Lakini kumbuka - kukimbia kutoka kwa wajibu ni sawa na kukimbia ukweli.
  • 15:47 - 15:52
    Na ni mbio ambayo hutaweza kushinda kamwe.
  • 15:52 - 15:56
    Kwa vijana wanaotazama sasa hivi -
  • 15:56 - 16:03
    ukisema hukotayari kwa watoto, hukotayari kwa ndoa.
  • 16:03 - 16:08
    Kama hauko tayari kwa ndoa, hauko tayari kwa ngono.
  • 16:08 - 16:13
    Tafadhali ikimbie uasherati.
  • 16:13 - 16:20
    Toroka uasherati.
  • 16:20 - 16:33
    Ikiwa tutachochea 'upendo' kabla ya wakati wake, tutazindua tu tamaa.
  • 16:33 - 16:40
    Kwa wale wanaomngojea Bwana kwa ajili ya ndoa - vema.
  • 16:40 - 16:49
    Lakini usimsubiri tu Bwana. Hakikisha unasubiri ukiwa ndani ya Bwana.
  • 16:49 - 16:55
    Kwa sababu wakati wa kusubiri si wakati wa kupoteza.
  • 16:55 - 17:02
    Utiifu unaohitajika ili kukuweka kwa ajili ya ndoa
  • 17:02 - 17:08
    pia inahitajika kukuweka ndani ya ndoa.
  • 17:08 - 17:15
    Usipoteze kusubiri kwako.
  • 17:15 - 17:27
    Masomo unayojifunza katika safari ya imani kwenye barabara kuelekea hatima yako
  • 17:27 - 17:35
    itakuendeleza wewe hadi hatua na kutoka hatua
  • 17:35 - 17:42
    ambapo wakati sahihi utaleta mtu sahihi.
  • 17:42 - 17:45
    Hii ni himizo kwa wale wanaotazama leo.
  • 17:45 - 17:55
    Nina mengi ya kushiriki nanyi kuhusu mada hii baada ya niliyoyapitia siku chache zilizopita.
  • 17:55 - 18:01
    Kuna mafunzo mengi ya kushiriki, lakini nitakomea hapa
  • 18:01 - 18:11
    na kusema tu asante kwa watazamaji wote, marafiki, washirika, na wafuasi wa God's Heart TV.
  • 18:11 - 18:15
    Asante kwa upendo wenu, sala zenu, msaada wenu, na himizo yenu.
  • 18:15 - 18:23
    Na nakwambia hivi - kuwasili kwa Josiah kumeongeza tu hamu yetu
  • 18:23 - 18:29
    kuendelea kueneza Habari Njema kwenye pembe nne za dunia,
  • 18:29 - 18:37
    kuhubiri Habari Njema za Yesu Kristo kwa nguvu ya Roho Mtakatifu.
  • 18:37 - 18:46
    Na hakuna njia bora kwangu kusema, 'Asante, Yesu', kwa zawadi hii ya thamani ya maisha
  • 18:46 - 18:51
    kuliko kufanya kile Mungu ameniita nifanye.
  • 18:51 - 18:56
    Hivi sasa nataka kukuombea kwa jina la Yesu.
  • 18:57 - 19:06
    Hivi sasa, hebu tuombe kwa ajili ya wanandoa ambao wamo pamoja nasi wakati huu.
  • 19:06 - 19:13
    kutafuta uso wa Mungu kwa ajili ya mtoto.
  • 19:13 - 19:19
    Tumia mfano wa Josiah kama mahali pa kushikilia.
  • 19:19 - 19:24
    Wacha ushuhuda huu uwashe imani yako.
  • 19:24 - 19:35
    Chukua nafasi hii kuweka hitaji juu ya upako.
  • 19:35 - 19:45
    Kwanza kabisa, kumbuka hili - kiungo kikuu cha nyumba iliyo na amani ni moyo ulio na amani.
  • 19:45 - 19:50
    Chochote kinachokusumbua moyo wako - Nasema, pata utulivu sasa hivi!
  • 19:50 - 19:58
    Tulia katika jina kuu la Yesu Kristo!
  • 19:58 - 20:06
    Ni kipi kimezuia uzazi wako?
  • 20:06 - 20:22
    Kizuizi hicho kinachohusiana na kutopata mtoto - kiondolewe kwa jina kuu la Yesu!
  • 20:22 - 20:30
    Kila roho ya kuharibika kwa mimba - Nasema, ondoka sasa hivi!
  • 20:30 - 20:37
    Ondoka, katika jina kuu la Yesy!
  • 20:37 - 20:44
    Nini hicho kinachoathiri uzalishaji wako?
  • 20:44 - 20:45
    Je, ni uvimbe katika mfuko wa uzazi?
  • 20:45 - 20:48
    Je, ni uvimbe wa ovari?
  • 20:48 - 20:51
    Je, ni hesabu ya mbegu za kiume kuwa chini?
  • 20:51 - 20:53
    Je, ni homoni kutokuwa sawa?
  • 20:53 - 21:00
    Lolote lililopo, kwa damu ya thamani ya Yesu Kristo, uponyaji upo.
  • 21:00 - 21:02
    Ponywa katika tumbo lako!
  • 21:02 - 21:04
    Ponywa katika viungo vyako!
  • 21:04 - 21:06
    Ponywa katika mfumo wako!
  • 21:06 - 21:10
    Pokea uponyaji katika jina kuu la Yesu!
  • 21:10 - 21:18
    Pokea uzalishaji katika jina kuu la Yesu!
  • 21:18 - 21:26
    Kila shambulio la kiroho dhidi ya nyumba yako, familia yako, ndoa yako -
  • 21:26 - 21:34
    Hio ndoto mbaya isiyoeleweka, nasema kiondolewe!
  • 21:34 - 21:36
    Kiondolewe katika jina la Yesu.
  • 21:36 - 21:42
    Hio ndoto mbaya wakati wa kutafuta mtoto,
  • 21:42 - 21:49
    Hio ndoto mbaya isiyoeleweka - kiondolewe katika jina kuu la Yesu.
  • 21:49 - 21:52
    Asante, Bwana.
  • 21:52 - 21:58
    Nitaombea wazazi wanaotazama kipindi hiki.
  • 21:58 - 22:09
    Kumbuka, kulea mtoto, kulea watoto ni kazi kutoka kwa Mungu.
  • 22:09 - 22:20
    Naomba upokee nguvu kutoka juu ili uendelee kuzingatia kazi hiyo,
  • 22:20 - 22:27
    kubaki na wajibu huo, kubaki gangari kwenye wajibu huo,
  • 22:27 - 22:31
    katika jina kuu la Yesu.
  • 22:31 - 22:40
    Je, una mtoto au watoto wenye tabia ya kuasi?
  • 22:40 - 22:41
    Wacha niombee mtoto huyo.
  • 22:41 - 22:44
    Wacha niombee watoto hao sasa hivi.
  • 22:44 - 22:48
    Wacha na kuwa na mabadiliko.
  • 22:48 - 22:55
    Na iwe na mabadiliko yasiyo ya kawaida kutoka ndani hadi nje!
  • 22:55 - 23:04
    Pokea mabadiliko hayo katika jina kuu la Yesu.
  • 23:04 - 23:12
    Kuchelewa kwa muujiza wa Hana ulikuwa tu maandalio
  • 23:12 - 23:18
    Kwa mtoto wa ajabu wa ahadi kutoka juu.
  • 23:18 - 23:27
    Watu wa Mungu, je, unakumbana na kuchelewa katika kutafuta mtoto?
  • 23:27 - 23:34
    Usijaribu kukata tamaa kwa sababu ya kuchelewa.
  • 23:34 - 23:40
    Usikate tamaa kwa sababu ya kuchelewa.
  • 23:40 - 23:46
    Jazwa kustahimili!
  • 23:46 - 23:56
    Jazwa kuvumulia bila uoga, katika jina kuu la Yesu!
  • 23:56 - 24:04
    Ndio, najua kuna wale wanatazama sasa hivi ambao wako na uchungu.
  • 24:04 - 24:11
    Uchungu wa kimwili, uchungu wa hisia, uchungu wa mawazo, uchungu wa kiroho.
  • 24:11 - 24:17
    Kama mtoto wa Mungu, uchungu huo utapita.
  • 24:17 - 24:32
    Kila roho nyuma ya hio uchungu - ondoka! Ondoka katika jina la Yesu!
  • 24:32 - 24:38
    Kila aina ya uchungu - uchungu wa kimwili, uchungu wa kiroho, uchungu wa hisia -
  • 24:38 - 24:43
    pokea uponyaji katika jina la Yesu!
  • 24:43 - 24:58
    Pokea uponyaji kupitia damu ya thamana ya Yesu Kristo.
  • 24:58 - 25:12
    Watu wa Mungu, mchakato wa Mungu hauwezi kuondoa uchungu.
  • 25:12 - 25:15
    lakini uchungu utapita.
  • 25:15 - 25:21
    Nakuhakikishia - uchungu utapita.
  • 25:21 - 25:31
    Naomba sasa hivi upokee nguvu ya kustahimili bila kuingiza uoga.
  • 25:31 - 25:36
    Usikubali sauti ya uchungu ikupoteze kwa uoga.
  • 25:36 - 25:49
    Pokea nguvu ya kustahimili katika jina la Yesu, ukijua uchungu utapita.
  • 25:49 - 25:57
    Kama vile kuwasili kwa Josiah kumeleta furaha, kama mtoto wa Mungu, furaha ni sehemu yako!
  • 25:57 - 26:00
    Na kuwe na sherehe katika nyumba yako.
  • 26:00 - 26:03
    Na kuwe na kushangilia katika familia yako.
  • 26:03 - 26:12
    Na kuwe na ushuhuda wa kipekee katika nyumba yako katika jina kuu la Yesu.
  • 26:12 - 26:22
    Asante, Yesu, kwa zawadi ya thamana cha maisha.
  • 26:22 - 26:27
    Katika jina kuu la Yesu tumeomba, amina.
Title:
Barua Kwa Mwanangu Mpendwa!
Description:

more » « less
Video Language:
English
Team:
God's Heart TV
Duration:
26:58

Swahili subtitles

Revisions Compare revisions