MIPANGO YAKO MIKONONI MWA MUNGU! | Mahubiri ya Ndugu Chris
-
0:00 - 0:08Ukishindwa kumuingiza Mungu katika mipango yako,
unapanga kushindwa. -
0:10 - 0:15Karibuni tena nyote kwenye
Ibada hii ya Maombi Shirikishi. -
0:15 - 0:22Kabla ya jambo lolote, tuombe pamoja.
-
0:22 - 0:32Ninaomba sasa hivi kwa kila moyo
ulioungana na huduma hii -
0:32 - 0:46kwamba wakutane na uhalisia wa uwezo wako, upendo, wema wako katika maisha yao.
-
0:46 - 0:55Katika jina kuu la Yesu Kristo tunaomba.
-
0:55 - 0:59Na watu wa Mungu wakasema, Amina!
-
0:59 - 1:10Kwanza kabisa, wacha niwasalimie nyote
Heri ya Mwaka Mpya 2025. -
1:10 - 1:15Nina neno la kutia moyo
la kukushirikisha leo. -
1:15 - 1:21Ni kawaida katika kipindi hiki - tunapoondoka mwaka mmoja na kuingia mwaka mpya -
-
1:21 - 1:25ni kawaida sana kwetu kuwa na muda wa kutafakari yaliyo mbele.
-
1:25 - 1:29Je, nina mipango gani
kwa mwaka huu unaokuja? -
1:29 - 1:34Inaweza kuwa katika maisha yako ya kibinafsi,
maisha yako ya kitaaluma. -
1:34 - 1:38Inaweza kuwa katika taaluma yako -
'Nataka kupanua biashara hapa.' -
1:38 - 1:43Labda mahusiano - 'Mwaka huu,
nataka kuolewa!' -
1:43 - 1:46'Mwaka huu, tunataka kupata watoto pamoja' - waume na wake.
-
1:46 - 1:48Huu ni wakati ambao tunapanga mipango.
-
1:48 - 1:52Tunafikiria mwaka ujao,
mwaka ujao. Nzuri! -
1:52 - 1:57Ni vizuri kupanga mipango lakini
-
1:57 - 2:09usiingie kwenye makosa ya kupanga mipango ya kesho kana kwamba wewe ndiye mmiliki wake.
-
2:09 - 2:14Fikirini juu ya hilo enyi watu wa Mungu.
-
2:14 - 2:27Usiingie kwenye mtego wa kupanga mipango ya siku zijazo kana kwamba ni yako.
-
2:27 - 2:31Sisemi ni makosa kupanga mipango.
-
2:31 - 2:34Sisemi ni makosa kuangalia mbele.
-
2:34 - 2:40Ninasema unapofanya
mipango kama Mkristo - -
2:40 - 2:44'Nini kinachofuata mnamo 2025? Kipi kilicho mbele?
-
2:44 - 2:46Je! ninataka kuzingatia nini?
-
2:46 - 2:51Ninataka kufikia nini katika kazi yangu, maisha ya kibinafsi, biashara, fedha?
-
2:51 - 2:53Ninataka kufanya nini?'
-
2:53 - 3:01Unapopanga mipango, lazima ufanye hivyo
kwa utambuzi wa mambo matatu. -
3:01 - 3:04Na mimi nataka uandike.
Tafadhali andika hii. -
3:04 - 3:07Ujumbe huu utakusaidia kwa mwaka huu.
-
3:07 - 3:161. Maisha hayana uhakika
-
3:16 - 3:272. Mungu ni mwenye enzi kuu
-
3:27 - 3:363. Kila siku ina riziki yake
-
3:36 - 3:39Nitawaambia tena, watu wa Mungu.
-
3:39 - 3:44Unapopanga mipango, unapopanga juu ya siku zijazo,
-
3:44 - 3:50lazima ufanye hivyo ukiwa na utambuzi huu,
ufahamu huu - -
3:50 - 3:561. Maisha hayana uhakika
-
3:56 - 4:04Wakati fulani tutakabili hali
zilizo nje ya uwezo wetu. -
4:04 - 4:10Kwa nini unapanga mipango
kana kwamba unaudhibiti? -
4:10 - 4:23Wakati mwingine kama mtoto wa Mungu, unaweza
kukutana na matukio yasiyobadilika - -
4:23 - 4:34hakuna kiasi cha maombi, kufunga au
kukomaa kiroho kutabadili. -
4:34 - 4:39Maisha hayana uhakika.
-
4:39 - 4:452. Mungu ni mwenye enzi kuu
-
4:45 - 4:53Maisha kukosa uhakika hakubadili
enzi kuu ya Mungu. -
4:53 - 4:56Ndiyo, maisha yamejawa na kutokuwa na uhakika.
-
4:56 - 5:07Lakini jambo moja unaweza kuwa na uhakika nalo - wema wa Mungu, nguvu za Mungu, upendo wa Mungu.
-
5:07 - 5:13Hata katikati ya
wazimu wa dunia hii, -
5:13 - 5:17tunaweza kuwa na uhakika juu ya
wema wa Mungu. -
5:17 - 5:19Yeye ni mwenye enzi.
-
5:19 - 5:33Na kama Wakristo, lazima tutambue maisha yetu, nyakati zetu ziko mikononi mwake.
-
5:33 - 5:35Mungu ni mwenye enzi.
-
5:35 - 5:403. Kila siku ina riziki yake
-
5:40 - 5:46Utupe leo mkate wetu wa kila siku.
-
5:46 - 5:49Mana kwa hitaji la wakati huu.
-
5:49 - 5:58Kila siku ina riziki yake -
Mungu hutoa neema kwa kila siku. -
5:58 - 6:05Ujumbe ninaopaswa kushiriki
nawe, kwa ufupi ni huu: -
6:05 - 6:10'Mipango yako Mikononi mwa Mungu'.
-
6:10 - 6:15Unaweza kusema hivyo sasa hivi. Ikiwa uko na mtu nyumbani, mwambie tu,
-
6:15 - 6:21"Mipango yako mikononi mwa Mungu."
-
6:21 - 6:26Ikiwa uko peke yako, unaweza kujiambia
au unaweza kuniambia, -
6:26 - 6:32"Mipango yangu iko mikononi mwa Mungu."
-
6:32 - 6:37Mwanadamu hupanga; Mungu hutekeleza.
-
6:37 - 6:44Mwanadamu anapendekeza; Mungu huamuru.
-
6:44 - 6:50Kama Mkristo, tazama, sikwambii tena kwamba usifanye mpango,
-
6:50 - 6:58bali panga mipango huku ukifahamu
kuwa maisha yako yako mikononi mwa Mungu. -
6:58 - 7:08Fanya mipango kutoka katika nafasi ya
kujitiisha kwa Mpangaji Mkuu -
7:08 - 7:16ambaye njia zake ni za juu kuliko zetu,
ambaye mipango yake ni mikubwa kuliko yetu. -
7:16 - 7:26Wale wanaoshindwa kuweka
mipango yao mikononi mwa Mungu -
7:26 - 7:32wanajiweka kwenye
njia ya kushindwa. -
7:32 - 7:35Hata nitarahisisha. Nitasema hivi -
-
7:35 - 7:46ukishindwa kumjumuisha Mungu katika mipango yako,
unapanga kushindwa. -
7:46 - 7:52Hebu tuyaangazie Maandiko makini katika Yakobo 4.
-
7:52 - 7:59Ninataka kuangazia ukweli huu ili wakati tunapanga mipango ya kesho,
-
7:59 - 8:07tunafanya hivyo tukiwa na ufahamu sahihi wa
nafasi ya Mungu na nafasi yetu. -
8:07 - 8:13Unapopanga juu ya siku zijazo,
kumbuka ni nani aliye Mkuu. -
8:13 - 8:20Hebu tusome pamoja - Yakobo 4:13.
-
8:20 - 8:29“Haya basi, ninyi msemao, Leo au kesho tutakwenda katika mji fulani;
-
8:29 - 8:34tutakaa huko mwaka mzima, tutanunua na kuuza
na kujipatia faida...” -
8:34 - 8:40'Mnamo 2025, nitaenda huko.
Nitafanya hivi katika biashara yangu. -
8:40 - 8:44Hakika hili litatokea.'
-
8:44 - 8:53“... kumbe hujui kitakachotokea kesho. Kwani maisha yako ni nini?
-
8:53 - 9:08Bali ni mvuke unaoonekana kwa muda mfupi na kisha kutoweka.
-
9:08 - 9:20Badala yake mnapaswa kusema, Bwana akipenda, tutaishi na kufanya hili au lile.
-
9:20 - 9:25"Bwana akipenda, hili litatokea mwaka wa 2025.
-
9:25 - 9:33Bwana akipenda, mpango huu utatimia.'
-
9:33 - 9:44Yakobo 4:16 BHN - Lakini sasa mnajivunia majivuno yenu. Majivuno yote kama hayo ni mabaya.”
-
9:44 - 9:52Maandiko hapa, nataka kusisitiza,
hayasemi kamwe usifanye mpango, -
9:52 - 10:00lakini yanakuonya usiichukue nafasi ya Mungu inapokuja kwenye mpango wako.
-
10:00 - 10:08Kama nilivyosema hapo awali, unapotazama mbele, kumbuka ni nani aliye Kichwa - Yesu.
-
10:08 - 10:15Hakuna kitu hatari zaidi kama kuchukua nafasi ya Mungu katika mpango wako.
-
10:15 - 10:28Kuchukua nafasi ya Mungu katika mpango wako ndiyo njia ya uhakika ya kuanguka kwa mpango huo - hatimaye.
-
10:28 - 10:31Sasa, unaweza kunitazama na kusema,
'Unasema nini Ndugu Chris? -
10:31 - 10:39Sichukui nafasi ya Mungu katika mpango wangu. Ningewezaje kuwa Mungu? Mimi si Mungu!'
-
10:39 - 10:46Lakini wengi wetu, kwa jinsi tunavofanya
mipango yetu ya kesho, -
10:46 - 10:52tunafanya hivyo kwa njia inayochukua
umiliki wa kesho. -
10:52 - 10:55Na unajua hatari ya hii?
-
10:55 - 10:59Unapochukua umiliki wa kesho,
-
10:59 - 11:02unabeba uzito ambao hukukusudiwa
kubeba, -
11:02 - 11:11ndiyo maana bila shaka huishia
katika wasiwasi, woga na mashaka. -
11:11 - 11:15'Nini kitatokea? Itakuwaje juu ya hiki?
Vipi kuhusu lile?' -
11:15 - 11:20Wasiwasi ni mwizi wa furaha.
-
11:20 - 11:25Wasiwasi ni mwizi wa amani.
-
11:25 - 11:30Wasiwasi ni mwizi wa hukumu halali,
-
11:30 - 11:36ambayo ni muhimu katika kuwa msimamizi mzuri
wa kile kilicho mikononi mwako leo. -
11:36 - 11:47Ngoja nikukumbushe maneno mazuri ya Bwana wetu Yesu Kristo katika Mathayo 6:34.
-
11:47 - 11:54Yesu alisema, “Basi, msisumbukie
ya kesho; -
11:54 - 12:02maana kesho itajisumbukia na mambo yake. Yatosha kwa siku taabu yake yenyewe.”
-
12:02 - 12:05Kila siku ina riziki yake.
-
12:05 - 12:07Kila siku ina baraka zake.
-
12:07 - 12:08Kila siku ina shida zake.
-
12:08 - 12:10Tazama Yesu anachosema hapa.
-
12:10 - 12:18Lakini kwa nini ni jambo la kawaida kwetu leo kuanguka katika mtego wa kuhangaikia kesho?
-
12:18 - 12:23Kwa sababu tunaanguka katika mtego
wa kujivunia kesho, -
12:23 - 12:32Tunafanya kana kwamba kesho ni yetu,
ilihali leo tu ndio yetu. -
12:32 - 12:34Kesho ni ya Mungu.
-
12:34 - 12:39Sasa ni yako; kinachofuata ni cha Mungu.
-
12:39 - 12:45Ngoja nisome Andiko lingine
kutoka Mithali 27, -
12:45 - 12:49tukirudia maneno ya
Yakobo ambayo tumesoma hivi punde. -
12:49 - 12:53Katika Mithali 27:1, mwenye hekima anasema hivi,
-
12:53 - 13:12"Usijisifu kwa ajili ya kesho, kwa maana hujui yatakayoletwa na siku moja."
-
13:12 - 13:17Ninasisitiza nini kwa kunukuu Maandiko haya, watu wa Mungu,
-
13:17 - 13:20kuzungumza juu ya mada hii?
Kwa sababu ni mwaka mpya. -
13:20 - 13:23Ni wakati tunafikiria mbele, tunapanga mipango.
-
13:23 - 13:25Lengo ni lipi? Tutafanya nini?
-
13:25 - 13:28Sipingani na mipango hiyo, narudia.
-
13:28 - 13:33Mimi sihimizi uvivu.
Mimi sihimizi uzembe. -
13:33 - 13:36Sikuhimii
kukaa tu, kukunja mikono yako -
13:36 - 13:39na kutarajia mambo kushuka kutoka
Mbinguni hadi mapajani mwako. -
13:39 - 13:51Ni vizuri kufanya mipango, lakini ni lazima tufanye hivyo kwa kutambua nafasi ya Mungu.
-
13:51 - 14:00Ikiwa sivyo, unaweza kuanguka katika mtego wa kuwa na wasiwasi juu ya kesho au kujisifu kuhusu kesho.
-
14:00 - 14:02Unaweza hata usijue,
-
14:02 - 14:09lakini jinsi unavyoitikia
mpango wako unapokatizwa itaonyesha hivyo. -
14:09 - 14:13Hii ni hatua ya kujichunguza,
watu wa Mungu. -
14:13 - 14:18Umefanya mpango - 'Nataka kwenda hapa wakati huu; Nataka kufanya hivi katika biashara yangu.'
-
14:18 - 14:24Je, unaitikiaje
mpango huo unapokatizwa? -
14:24 - 14:34Mwitikio wako kwa kukatizwa kwa mpango wako unaonyesha ni mpango wa yupi unauamini hakika.
-
14:34 - 14:37Je, unaanguka pale mipango yako inapoanguka?
-
14:37 - 14:43Unaanza kunung'unika, kulalamika,
kujilinganisha na wengine -
14:43 - 14:47na kujipima kwa
viwango vilivyotengenezwa na mwanadamu. -
14:47 - 14:52Je, furaha yako huanguka pale
mipango yako inapovunjika? -
14:52 - 14:57Je, amani yako husambaratika
pale mpango wako unaposambaratika? -
14:57 - 15:01Inaonyesha hujaweka
mpango wako mikononi mwa Mungu. -
15:01 - 15:06Kwa sababu kile unachokiona kama
usumbufu katika mpango wako -
15:06 - 15:11kinaweza kuwa hatua kuelekea
utimilifu wa mpango wa Mungu. -
15:11 - 15:15Mungu ni mkuu!
-
15:15 - 15:19Anawatunza watoto wake.
-
15:19 - 15:27Wakati mwingine kile unachokiona kama usumbufu kinaweza kuwa uingiliaji kati wa Mungu
-
15:27 - 15:36kukuhifadhi, kukutayarisha, kukuimarisha, kukurekebisha, kukujenga kiroho.
-
15:36 - 15:40Unachokiona kama
usumbufu katika mpango wako -
15:40 - 15:46kinaweza kuwa hatua ya kutimiza mpango wa Mungu.
-
15:46 - 15:56Lakini mara nyingi, mipango yetu inapoingiliwa, inapodukizwa,
-
15:56 - 16:01tunaitikiaje? Je, tunajibuje?
-
16:01 - 16:05Unajibu kwa imani au hofu?
-
16:05 - 16:10Je, unajibu kwa
utulivu au kulalamika? -
16:10 - 16:14Je, unatendaje
mpango wako unapoingiliwa? -
16:14 - 16:16Umefanya kila
linalowezekana kibinadamu. -
16:16 - 16:20Umetekeleza sehemu yako, lakini
mambo yaliyo nje ya uwezo wako -
16:20 - 16:25yakaja na kuusambaratisha huo mpango.
Je, unaitikiaje? -
16:25 - 16:32Ndiyo maana nilisema watu wa Mungu,
mnapopanga mipango ya kesho, -
16:32 - 16:42fanya hivyo ukitambua maisha hayana uhakika, Mungu ni mwenye enzi na kila siku ina riziki yake.
-
16:42 - 16:49Unapaswa kufanya nini?
Zingatia neema ya leo. -
16:49 - 16:55Wengine tunahangaika sana kuhusu kesho, tunajishughulisha sana kufikiria kesho
-
16:55 - 17:03kiasi kwamba hatusimamii ipasavyo, kukifanyia kazi kile kilicho mikononi mwetu leo.
-
17:03 - 17:08Usitarajie tu
-
17:08 - 17:13kwamba neema uliyo nayo leo itapatikana kwako kesho.
-
17:13 - 17:24Usifikirie kuwa unachoweza kufikia leo, utaweza kukifikia kesho.
-
17:24 - 17:29Mungu hutupa neema kwa kila siku.
-
17:29 - 17:33Ndiyo maana ni lazima umwamini Yeye kila siku.
-
17:33 - 17:37Ndiyo maana unahitaji kuwa na
uhusiano naye. -
17:37 - 17:42Ndio, unapanga mipango yako. Ndiyo, unafanya kazi kwa bidii kuelekea utimizo huo.
-
17:42 - 17:47Ndio, unatoa ubora wako ukiwa na
ufahamu: -
17:47 - 17:52Nani mwenye kauli ya mwisho?
Yehova ndiye mwenye kauli ya mwisho. -
17:52 - 17:54Unakumbuka wimbo huo!
-
17:54 - 18:03Nani mwenye usemi wa mwisho
Yehova ndiye mwenye usemi wa mwisho -
18:03 - 18:06Mungu ndiye mwenye neno la mwisho katika maisha yetu.
-
18:06 - 18:10Mipango yetu si kuchukua nafasi yake.
-
18:10 - 18:16Ukifanya mpango, uweke mikononi Mwake.
-
18:16 - 18:21Hili ni neno langu la kutia moyo
kwenu leo watu wa Mungu. -
18:21 - 18:24Narudia, sikukatishi tamaa
kufanya mpango huo. -
18:24 - 18:26Kwa kweli, ninahimiza!
-
18:26 - 18:31Ukiwa Mkristo, tafakari kwa makini na kwa sala mwaka ujao.
-
18:31 - 18:36Fanya mpango. Utafuteni uso wa Mungu kwa ajili yake. Ni nzuri!
-
18:36 - 18:39Wakati mwingine watu huenda
mbali sana kwa njia nyingine. -
18:39 - 18:44Wanasema, ‘Vema, kama Mungu
ameniahidi hilo, basi -
18:44 - 18:48Yeye ndiye atakayeileta
kwangu.' - kama hivyo. -
18:48 - 18:49Wacha niiweke kama hii:
-
18:49 - 18:56Kumngoja Bwana si kisingizio
cha kutokufanya sehemu yako. -
18:56 - 18:59'Namngoja Bwana kwa baraka hii.
-
18:59 - 19:01Namngoja Bwana
kwa ajili ya mafanikio hayo. -
19:01 - 19:05Ninamngojea Bwana
ahadi hiyo itimie.' Nzuri! -
19:05 - 19:07Je, unamngojeaje Bwana kwa ufanisi?
-
19:07 - 19:10Unatumia kile kilicho
mikononi mwako leo. -
19:10 - 19:12Kumngoja Bwana si
kisingizio cha uvivu. -
19:12 - 19:16Tusisingizie mambo ya kiroho juu ya usimamizi mbaya .
-
19:16 - 19:25Mungu hatabariki uwakili usiowajibika kwa mafanikio.
-
19:25 - 19:28Unaomba, 'Mungu, ibariki biashara yangu'
-
19:28 - 19:32lakini unasimamia vibaya kile
kilicho mikononi mwako leo. -
19:32 - 19:35Sala hiyo inawezaje kutimia?
-
19:35 - 19:38Natumaini mtafuata ninachosema
, watu wa Mungu. -
19:38 - 19:43Tumia kile kilicho mikononi mwako leo
kwa neema ya leo. -
19:43 - 19:45Wacha niiweke kama hii:
-
19:45 - 19:51Changanya kazi ngumu na
imani tulivu kwa Mungu kwa siku zijazo. -
19:51 - 19:56Fanya bidii kuelekea ndoto yako. Ndoto yako haitafanya kazi kwa niaba yako.
-
19:56 - 20:03Fanya bidii kuelekea mpango wako. Mpango wako
hautapanda mbegu kwa ajili yako. -
20:03 - 20:10Lakini unapofanya kazi kwa bidii, unapotoa ubora wako, unafanya hivyo ukiwa na ufahamu -
-
20:10 - 20:16maisha yangu yako mikononi mwa Mungu;
nyakati zangu ziko mikononi mwa Mungu. -
20:16 - 20:22Acha nikusomee methali moja zaidi,
wakati huu kutoka Mithali 16. -
20:22 - 20:29Mwenye hekima anaiweka wazi.
Mithali 16:9 inasema hivi, -
20:29 - 20:36"Moyo wa mtu huifikiri njia yake,
bali Bwana huziongoza hatua zake." -
20:36 - 20:42Mipango yako mikononi mwa Mungu.
-
20:42 - 20:49Wana wa Mungu, liwekeni neno hili moyoni.
-
20:49 - 20:57Unapoweka kila kitu mikononi mwa Mungu,
-
20:57 - 21:03muda si mrefu utaiona
mikono ya Mungu katika kila kitu. -
21:03 - 21:11Lazima uamini kwamba mkono Wake unafanya kazi
-
21:11 - 21:19hata wakati huwezi
kuyaona maandishi ya mkono Wake. -
21:19 - 21:26Labda sijui mwisho wa simulizi,
-
21:26 - 21:32Lakini ninamwamini Mwandishi wa simulizi.
-
21:32 - 21:37Naweza nisione taswira kamili.
-
21:37 - 21:41Lakini ninamwamini Mpangaji Mkuu.
-
21:41 - 21:44Naweza nisione bidhaa iliyokamilishwa.
-
21:44 - 21:49Lakini ninamwamini Mbunifu wa Kimungu.
-
21:49 - 21:53Huu ndio msimamo wetu kama Wakristo.
-
21:53 - 21:58Ngoja ninukuu kitu
alichosema Nabii TB Joshua -
21:58 - 22:01kufikisha ujumbe huu kwenye hitimisho.
-
22:01 - 22:09Baada ya kufanya
kila linalowezekana kibinadamu, -
22:09 - 22:15mwachie Mungu suala hilo ili aisahishe kazi yako.
-
22:15 - 22:21Hivi ndivyo unavyoweka
mipango yako mikononi mwa Mungu. -
22:21 - 22:27Shetani anataka tukazie fikira kile ambacho hatuna, na kukazia fikira kile ambacho hatujui.
-
22:27 - 22:33Kwa sababu hii husababisha wasiwasi,
malalamiko, usimamizi mbaya. -
22:33 - 22:37Lakini kama Mkristo, unajua nini?
Mungu ni mwenye enzi. Mungu ni mwema. -
22:37 - 22:41Anaona picha kubwa zaidi.
-
22:41 - 22:44Una nini? Neema kwa leo.
-
22:44 - 22:53Tumia kile kilicho mikononi mwako leo na acha kila kitu mikononi mwake kwa ajili ya kesho.
-
22:53 - 23:01Mungu abariki neno hili la kutia moyo katikati ya mioyo yetu.
- Title:
- MIPANGO YAKO MIKONONI MWA MUNGU! | Mahubiri ya Ndugu Chris
- Description:
-
Je, tujipange vipi kwa ajili ya kesho bila kuingia katika mtego wa kujisifu kuhusu kesho au kuhangaikia kesho? Je, unapangaje mipango, kama Mkristo? Katika mahubiri haya halisia na Ndugu Chris yenye kichwa, 'Mipango Yako Mikononi mwa Mungu' - gundua jinsi ya kupanga mapema huku ukikumbuka ni nani aliye Mkuu - Yesu Kristo!
"Unapopanga mipango, lazima ufanye hivyo ukiwa na ufahamu wa mambo matatu:
1. Maisha hayana uhakika.
2. Mungu ni mwenye enzi kuu.
3. Kila siku ina riziki yake.➡️ Pata Kutiwa Moyo Kila Siku kwenye WhatsApp - https://godsheart.tv/whatsapp/
➡️ Kuwa Mshirika wa TV wa Moyo wa Mungu - https://godsheart.tv/partnership
➡️ Habari kuhusu Maombi Shirikishi - https://godsheart.tv/interactive-prayer/
➡️ Jitolee kama Mtafsiri wa TV ya Moyo wa Mungu - https://godsheart.tv/translate/
➡️ Shirikisha ushuhuda wako - https://godsheart.tv/testimony
➡️ Jiunge na Ibada yetu ya Maombi ya Moja kwa Moja Jumamosi ya kwanza ya kila mwezi - https://www.youtube.com/godshearttv/live - Video Language:
- English
- Team:
God's Heart TV
- Duration:
- 23:32
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for YOUR PLANS in GOD'S HANDS! | Brother Chris Sermon | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for YOUR PLANS in GOD'S HANDS! | Brother Chris Sermon | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for YOUR PLANS in GOD'S HANDS! | Brother Chris Sermon | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for YOUR PLANS in GOD'S HANDS! | Brother Chris Sermon | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for YOUR PLANS in GOD'S HANDS! | Brother Chris Sermon | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for YOUR PLANS in GOD'S HANDS! | Brother Chris Sermon | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for YOUR PLANS in GOD'S HANDS! | Brother Chris Sermon | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for YOUR PLANS in GOD'S HANDS! | Brother Chris Sermon |