< Return to Video

Ishi kama unakufa? Kutenda katika mashaka | Ariel Dempsey | TEDxMSU

  • 0:04 - 0:36
    (Muziki unacheza:"A Million Dreams")
  • 2:31 - 2:33
    (Makofi)
  • 2:39 - 2:41
    Ngoja nivute pumzi kidogo ...
  • 2:44 - 2:47
    lakini nitakuambia kipi ni, kinafurahisha sana,
  • 2:47 - 2:48
    Ni kweli
  • 2:50 - 2:54
    wimbo nilioucheza unaitwa
    "Ndoto Millioni Moja"
  • 2:54 - 2:57
    Unatoka katika muvi
    ninayoipenda, iitwayo "
  • 2:58 - 3:00
    Wakati mwingine tunaweza
    kuziona ndoto zetu dhahiri,
  • 3:01 - 3:04
    lakini wakati mwingine mambo
    hayako wazi sana,
  • 3:05 - 3:07
    Je naweza kuamini katika hii?
  • 3:08 - 3:11
    Najuaje kuwa uthubutu huu una faida?
  • 3:11 - 3:13
    Inakuwaje kama siko sahihi?
  • 3:14 - 3:17
    Kwangu , haya si maswali ya kufikirika tu.
  • 3:17 - 3:19
    Ni maswali ninayoishi nayo.
  • 3:20 - 3:22
    Ngoja niwashirikishe kidogo
    kuhusu chimbuko langu.
  • 3:23 - 3:24
    Jina langu ni Ariel,
  • 3:24 - 3:27
    Ni mwanafunzi wa mwaka wa nne wa
    udaktari katika chuo cha Jimbo la Michigan,
  • 3:27 - 3:29
    Ninakaribia kuhitimu na shahada ya Udaktari
  • 3:29 - 3:33
    na ninafanya Shahada ya Udaktari
    wa Falsafa ya sayansi na dini katika chuo cha Oxford.
  • 3:34 - 3:37
    Ninataka kuwa daktari wa kuondoa
    maumivu ya mwili
  • 3:37 - 3:40
    na kuwa pamoja na watu katika
    mwisho wa maisha yao.
  • 3:40 - 3:43
    na pia nataka kuwa mawanazuoni wa theolojia
  • 3:43 - 3:46
    na kuchukua rasilimali za tamaduni zetu za kidini
  • 3:46 - 3:48
    katika huduma za afya.
  • 3:49 - 3:53
    kwa hiyo kama mwanafunzi wa
    utabibu na theolojia
  • 3:53 - 3:56
    Nimekuwa na muda wa kutafakari
    kuhusu tasnia hizi mbili
  • 3:56 - 4:00
    ambazo zinakutana na tashwishi nyingi.
  • 4:00 - 4:02
    katika utabibu na dini,
  • 4:02 - 4:04
    Kuna nyakati ambazo tunatenda,
  • 4:04 - 4:07
    hata pale ambapo hatuwezi kuona.
  • 4:08 - 4:10
    Nitakueleza kitu usiku huu wa leo
  • 4:10 - 4:15
    Kuwa nimetunza siri mbali na
    marafiki zangu wa karibu -
  • 4:16 - 4:18
    hata wale marafiki ambao
    nimewaalika hapa usiku huu.
  • 4:19 - 4:21
    Ingawa ni ngumu kuongelea
    habari zake,
  • 4:21 - 4:23
    Nitawaeleza habari yangu.
  • 4:24 - 4:26
    (Anavuta pumzi kubwa)
  • 4:29 - 4:31
    Januari, 2015
  • 4:31 - 4:33
    Nilikuwa nasafiri kwa ndege
    kwenda Uingereza.
  • 4:33 - 4:36
    Nilikuwa nimetoka kufanya usaili wa
    chuo cha udaktari katika chuo cha Jimbo la Michigan
  • 4:36 - 4:39
    nilikuwa narudi katika chuo cha Oxford
    kwa ajili ya masomo ya theolojia.
  • 4:40 - 4:43
    Ghafla, maumivu makali yakanipata kichwani,
  • 4:43 - 4:45
    nikaanza kutapika sana,
  • 4:45 - 4:48
    mapigo ya moyo na shinikizo la damu vikashuka sana,
  • 4:48 - 4:52
    na nikaanza kupoteza na kurudiwa na fahamu.
  • 4:52 - 4:55
    Ndege ilipotua, nilikimbizwa hospitalini,
  • 4:55 - 5:01
    na wiki kadhaa, sikuwa na nguvu ya kusimama,
    kuwaza,au hata ya kuwa macho.
  • 5:02 - 5:04
    Kwa miezi minne,
  • 5:04 - 5:07
    nililala kitandani katika chumba chenye giza cha Uingereza.
  • 5:08 - 5:09
    Mapazia yalifungwa,
  • 5:09 - 5:11
    taa zikazimwa,
  • 5:11 - 5:16
    na nikavaa miwani ya giza kwa kuwa sikuweza kuvumilia mwanga wowote.
  • 5:17 - 5:20
    Chochote kilichotokea katika ndege
  • 5:20 - 5:22
    kiliniacha katika mshtuko,
  • 5:22 - 5:26
    lakini matokeo yangu ya MRI yalinishangaza
    kwa namna ya nyingine.
  • 5:27 - 5:30
    Mama yangu, ambaye alisafiri kuja
    Uingereza kuniuguza
  • 5:30 - 5:31
    alikuwa pembeni yangu
  • 5:31 - 5:34
    wakati daktar alipokuwa anafafanua
    matokeo ya picha ya ubongo,
  • 5:36 - 5:39
    Akaonyesha alama nyeusi inayotoa damu katikati,
  • 5:39 - 5:41
    na akasema,
  • 5:41 - 5:43
    "Ariel,
  • 5:43 - 5:45
    Una shida ya cavernoma
  • 5:45 - 5:48
    au tatizo katika mishipa ya damu ya ubongo.
  • 5:48 - 5:50
    inavuja
  • 5:50 - 5:52
    na mara ikianza kutoa damu
  • 5:52 - 5:54
    itaendelea mara kwa mara kuta damu.
  • 5:54 - 5:58
    na kila damu inapoanza kutoka
    kunaweza kusababisha ulemavu.
  • 5:59 - 6:00
    pia inawezekana
  • 6:00 - 6:03
    mishipa yako ikapasuka ghafla,
  • 6:04 - 6:05
    na kama hii ikitokea,
  • 6:05 - 6:07
    unaweza kufa mara moja,"
  • 6:09 - 6:11
    Na akanipa takwimu mbaya,
  • 6:11 - 6:15
    nikauliza nina muda gani umebaki wa kuishi.
  • 6:15 - 6:17
    Akasema hajui.
  • 6:19 - 6:20
    Usiku ule, katika giza,
  • 6:20 - 6:21
    mama yangu na mimi tukalala kitandani,
  • 6:21 - 6:22
    tukalia
  • 6:22 - 6:25
    na tukacheka ubaya wa yote hayo.
  • 6:26 - 6:28
    Kupoteza kumbukumbu na nguvu ya viungo
  • 6:28 - 6:30
    au kifo cha ghafla.
  • 6:30 - 6:33
    Kama vile , kitu gani kingine kibaya kinaweza kutokea?
  • 6:34 - 6:35
    ninakumbuka
  • 6:35 - 6:37
    nikiwa nimelala katika giza
  • 6:37 - 6:39
    huku chumba kikiwa kinazunguka na nikiwa na miwani yangu,
  • 6:40 - 6:42
    na sikuweza kuona
  • 6:43 - 6:45
    sikuweza kuona maisha yangu yajayo
  • 6:46 - 6:49
    maisha niliyokuwa nikiyaota yaliondoka
  • 6:51 - 6:53
    niliamka asubuhi iliyofuata nikiwa na huzuni,
  • 6:54 - 6:56
    na nilipokuwa ninaomba,
  • 6:56 - 6:58
    nikagundua kitu kilichobadilisha maisha yangu
  • 7:00 - 7:01
    niligundua kuwa
  • 7:02 - 7:05
    sina tofauti na mtu yeyote mwingine.
  • 7:06 - 7:08
    yoyote anayeishi maisha marefu
  • 7:08 - 7:12
    anapoteza uwezo wa kumbukumbu na viungo.
  • 7:12 - 7:14
    Kila mtu atakufa siku moja,
  • 7:14 - 7:16
    na hakuna ajuaye siku hiyo.
  • 7:17 - 7:22
    maisha yetu yote ni mateke na yamejaa mashaka
  • 7:24 - 7:25
    ninogopa
  • 7:26 - 7:29
    lakini sina mashaka zaidi ya mtu yeyote mwingine
  • 7:31 - 7:33
    kwa hiyo nikakubaliwa kujiunga na chuo cha udaktari,
  • 7:33 - 7:36
    lakini kama nitakufa ndani ya mwaka,
  • 7:36 - 7:38
    kwa kujisumbua kwenda?
  • 7:39 - 7:41
    Rafiki yangu wa karibu alikuja kunitembelea,
  • 7:41 - 7:44
    nikamuuliza nifanye nini.
  • 7:45 - 7:46
    Akasema,
  • 7:47 - 7:48
    "Ariel,
  • 7:48 - 7:50
    ishi kama vile unaenda kufa,
  • 7:50 - 7:52
    Jaribu kujifunza vitu vingi kadiri iwezekanavyo
  • 7:52 - 7:55
    na raha nyingi kadiri iwezekanavyo,"
  • 7:56 - 8:00
    Lakini nilijua , "kuishi kama ninakufa"
  • 8:00 - 8:02
    haitakuwa njia yangu.
  • 8:03 - 8:04
    nisingekuwa na furaha kikamilifu.
  • 8:05 - 8:07
    nikafunga macho yangu nisione majibu ya vipimo,
  • 8:07 - 8:10
    nikijisahaulisha na jambo moja hadi jingine,
  • 8:10 - 8:13
    nikijaribu kujipatia raha maishani.
  • 8:14 - 8:15
    Pamoja na hayo,
  • 8:16 - 8:19
    umejaribu kuishi kama vile unaenda kufa?
  • 8:20 - 8:22
    Inachosha
  • 8:23 - 8:26
    ningependa kuishi kama ...
  • 8:26 - 8:28
    ninaishi.
  • 8:30 - 8:32
    Mchungaji wangu alikuja kunipaka mafuta,
  • 8:32 - 8:34
    Nikamuuliza natakiwa kufanya nini.
  • 8:34 - 8:36
    Akasema,
  • 8:36 - 8:38
    "Ariel,
  • 8:38 - 8:40
    sitakwambia nini cha kufanya,
  • 8:40 - 8:42
    lakini nitakwambia hivi,
  • 8:42 - 8:44
    Mungu anajitosheleza,
  • 8:44 - 8:48
    Usiache majibu haya yakutoe katika mstari."
  • 8:50 - 8:51
    Wakati huo,
  • 8:51 - 8:55
    nikaamua kuendelea na njia ambayo nilihisi kuitiwa.
  • 8:56 - 8:58
    nikaamua kufanya kile ambacho ningefanya
  • 8:58 - 9:00
    kama nisingepata majibu haya.
  • 9:01 - 9:03
    kama maisha yangu ni igizo
  • 9:03 - 9:05
    na najiandaa kupanda kuigiza
  • 9:05 - 9:07
    pazia linaweza kufunguliwa muda wowote
  • 9:07 - 9:10
    na nitakutwa nikicheza sehemu yangu vizuri.
  • 9:11 - 9:13
    nikapata ujasiri wa kuchukua hatua.
  • 9:15 - 9:18
    Lakini mwili wangu ukawa unaenda
    taratibu kuliko nilivyotaka.
  • 9:18 - 9:20
    nilikuwa mwanamichezo maisha yangu yote -
  • 9:20 - 9:22
    Nilikuwa mwanariadha katika
    Chuo kikuu cha Michigan;
  • 9:22 - 9:24
    Nikacheza kandanda nikiwa chuo kikuu cha Oxford
  • 9:24 - 9:28
    Lakini sasa, nikahisi mwili wangu ukinisaliti,
  • 9:28 - 9:30
    kama vile sikuweza kuuamini kufanya kazi.
  • 9:32 - 9:33
    Ingawa nilikuwa nimechoka,
    nilijifanya kama nina nguvu kuliko hali halisi
  • 9:33 - 9:34
    Kwa hiyo,
  • 9:34 - 9:37
    Nikafanya mazoezi ya yoga ya bibi kizee -
  • 9:37 - 9:38
    kama hivi -
  • 9:38 - 9:40
    na nikafanya hivi kila siku,
  • 9:40 - 9:42
    hata kama itakuwa kwa dakika chache,
  • 9:43 - 9:45
    sikuweza kufanya vitu vingi,
  • 9:45 - 9:46
    lakini niliweza kulala sakafuni
    na kujinyoosha mara moja,
  • 9:48 - 9:49
    ningeweza kusoma ukurasa huo mmoja,
  • 9:49 - 9:53
    Ningeweza kupata wakati mmoja wa furaha.
  • 9:53 - 9:55
    na kuna wakati nilifanya zaidi.
  • 9:55 - 9:59
    Taratibu, nikaweza kujinyoosha
  • 9:59 - 10:02
    na kucheka kwa nguvu
  • 10:02 - 10:06
    na kupenda zaidi.
  • 10:06 - 10:07
    nikashikilia tafakari kutoka katika
    kitabu cha Common Prayer
  • 10:08 - 10:09
    Kinasema,
  • 10:11 - 10:14
    "Leo ni siku nyingine, ee Bwana,
  • 10:14 - 10:16
    Sijui kipi kitatokea,
  • 10:17 - 10:19
    Lakini nifanye niwe tayari, Bwana,
  • 10:20 - 10:22
    Kwa chochote kitakachotokea,
  • 10:22 - 10:24
    Kama nitaweza kusimama
  • 10:24 - 10:26
    niwezeshe kusimama kishujaa.
  • 10:26 - 10:28
    Kama nitakaa,
  • 10:28 - 10:30
    nisaidie kukaa kimya,
  • 10:31 - 10:32
    Kama nitakaa kimya,
  • 10:32 - 10:34
    nisaidie kuwa na uvumilivu
  • 10:35 - 10:36
    Na kama sitakiwi kufanya chochote
  • 10:36 - 10:38
    nisaidie kutofanya kitu kwa ujasiri.
  • 10:39 - 10:41
    Fanya maneno haya kuwa zaidi ya maneno,
  • 10:41 - 10:44
    na naomba roho ya Yesu.
  • 10:44 - 10:47
    Amen,"
  • 10:47 - 10:49
    Kwa neema ya Mungu,
  • 10:49 - 10:50
    Nikaanza masomo ya udaktari
    wakati wa vuli.
  • 10:51 - 10:53
    Masomo ya udaktari hayakuwa rahisi.
  • 10:53 - 10:56
    Siku ya kwanza,
  • 10:57 - 10:59
    Rafiki yangu kipenzi kutoka shule
    ya Sekondari aliniendesha kwena chuoni
  • 10:59 - 11:00
    kwa sababu nilikuwa bado
    siwezi kuendesha
  • 11:00 - 11:02
    nikaingia katika usaili
  • 11:02 - 11:04
    nikiwa nimevaa miwani.
  • 11:04 - 11:06
    kwa sababu ya jeraha katika ubongo,
  • 11:06 - 11:08
    kusoma ilikuwa shida
  • 11:08 - 11:10
    na sikuweza kufikiri vizuri
    au kujisomea kama zamani.
  • 11:10 - 11:11
    Katika siku nilizohisi kuwa naumwa
  • 11:11 - 11:14
    na kuchoka kujisomea,
  • 11:15 - 11:17
    Kwa nini, " ninafanya hili
    kama nitakufa kesho"?
  • 11:17 - 11:18
    Je unajua,
  • 11:19 - 11:23
    ni mwanafunzi gani wa udaktari aiyeuliza swali
    hilo katika wakati fulani?
  • 11:24 - 11:25
    (Vicheko)
  • 11:25 - 11:28
    Masomo ya udaktari yalinikumbusha
    kuhusu mashaka.
  • 11:28 - 11:29
    Kutokea MRI mpaka maabara
    ya cadaver.
  • 11:29 - 11:33
    Katika chumba cha wagonjwa mahututi,
  • 11:34 - 11:37
    nilimuhudumia binti wa rika langu
    ambaye alikuwa anatoka damu katika uvimbe.
  • 11:37 - 11:38
    Alikuwa amepooza
    na kiufahamu kama mtoto wa miaka mitano
  • 11:38 - 11:42
    majibu yangu niliyafanya kuwa siri kwa
    watu wengi
  • 11:43 - 11:46
    Kwa sababu sikutaka watu wanitambulishe nayo
  • 11:47 - 11:50
    Lakini kuna nyakati,
  • 11:50 - 11:53
    siri yangu ilikuwa ni upweke
  • 11:53 - 11:55
    na mashaka yalijaa giza.
  • 11:55 - 11:57
    Lakini taratibu, nikatiwa nguvu.
  • 11:57 - 12:00
    Unifikirie vibaya, haikuwa rahisi.
  • 12:01 - 12:03
    kulikuwa na nyakati nyingi za kushuka na kupanda.
  • 12:03 - 12:06
    Lakini kwa wakati, yoga ya bibi kizee
  • 12:06 - 12:08
    ikabadilika na kuwa yoga kamili
  • 12:08 - 12:13
    na acroyoga
  • 12:13 - 12:15
    na yoga ya juu
  • 12:15 - 12:17
    na hariri ya juu.
  • 12:17 - 12:18
    Dansi la juu kwangu likawa ni alama
    ua uzuri kutoka majonzi yangu.
  • 12:19 - 12:20
    ikawa ni kikumbusho
  • 12:23 - 12:28
    ya furaha na shukrani
  • 12:29 - 12:31
    ambayo inaangaza maisha yangu,
  • 12:31 - 12:33
    na kama taswira ya ufufuko.
  • 12:33 - 12:34
    kwa hiyo, kitabibu, niko wapi kwa sasa?
  • 12:35 - 12:38
    Sijui.
  • 12:39 - 12:42
    Ninajua nina uvimbe wa cavernoma.
  • 12:44 - 12:46
    najua ulitoa damu hapo kabla.
  • 12:47 - 12:49
    sijui kama utatoa damu tena.
  • 12:49 - 12:51
    labda nitaishi miaka 80,
  • 12:52 - 12:53
    nikiwa na maisha kamili ya afya.
  • 12:55 - 12:57
    labda haitawezekana.
  • 12:57 - 12:59
    Lakinibado nashikilia tafakari ile
    kutoka kitabu cha maombi cha Common Prayer,
  • 13:00 - 13:01
    na kuishi katika mashaka.
  • 13:03 - 13:07
    ninakumbuka kwa undani
  • 13:07 - 13:09
    kuhusu ushauri wa Sir William Osler, Baba
    Utabibu wa Kisasa,
  • 13:10 - 13:12
    ambao aliutoa kwa wanafunzi wake wa udaktari.
  • 13:12 - 13:16
    Akasema,
  • 13:16 - 13:18
    "Kazi yetu si kuangalia kipi kipo gizani kwa mbali
  • 13:18 - 13:20
    lakini kufanya kilicho sahihi hapa karibu."
  • 13:21 - 13:25
    Je kufanya kilicho sahihi sasa
  • 13:25 - 13:28
    na kuona wakti ujao kwa mbali
  • 13:29 - 13:32
    kunakuwaje?
  • 13:32 - 13:34
    Nahisi inaonekana kama kudansi
    na hariri ukiwa na kitambaa usoni,
  • 13:34 - 13:35
    kama kuzunguka angani,
  • 13:36 - 13:39
    bila kujua uko wapi,
  • 13:39 - 13:41
    Kipi kinachokuwa nawe mkononi?
  • 13:41 - 13:44
    naweza kuzungusha hivi,
  • 13:44 - 13:46
    naweza kufunga hivi.
  • 13:46 - 13:48
    naweza kuachia kama hivi.
  • 13:48 - 13:50
    siwezi kuona,
  • 13:50 - 13:52
    lakini naweza kufanya -
  • 13:53 - 13:54
    nikidansi katika mashaka
  • 13:55 - 13:56
    bila kujali tunazungumzia utabibu au dini
  • 13:57 - 14:00
    au mahusiano au shule au kazi
  • 14:02 - 14:06
    au ndoto zetu
  • 14:06 - 14:10
    au hata muda wa kifo chetu chenyewe
  • 14:10 - 14:11
    wote tunaishi katika mashaka
  • 14:11 - 14:14
    majibu yangu ya vipimo yananikumbusha kuwa
    maisha hayana uhakika.
  • 14:15 - 14:18
    Lakini labda,
  • 14:20 - 14:24
    maisha hayahitaji hakika
  • 14:25 - 14:26
    ili kuyaishi
  • 14:26 - 14:28
    wote tunaona lakini kwa hafifu
  • 14:28 - 14:30
    Na kama vile daktari mzuri
    Osler anavyotukumbusha,
  • 14:32 - 14:34
    wote tunaweza kufanya kile kilicho dhahiri.
  • 14:35 - 14:38
    labda
  • 14:38 - 14:42
    tunaweza kufanya,
  • 14:44 - 14:45
    hata
  • 14:45 - 14:47
    pale tusipoona.
  • 14:48 - 14:49
    (Muziki wa: "A Million Dreams")
  • 14:49 - 14:51
    (Cheers)
  • 15:17 - 15:20
    (Makofi)
Title:
Ishi kama unakufa? Kutenda katika mashaka | Ariel Dempsey | TEDxMSU
Description:

Linapokuja suala la kufuatilia maono yetu, ni rahisi kuhisi kushindwa kufanya kitu kutokana na mashaa; tunawezaje kupata ujasiri wa kutenda, hata pale tusipoweza kuona?

Ariel Dempsey shares a story she has kept secret from many: her story of receiving a terminal diagnosis and recovering from traumatic brain injury. As a medical student at Michigan State and a PhD student in science and religion at Oxford, she draws on both medicine and spirituality to reflect on living with uncertainty. She embodies her message in a beautiful and inspiring performance danced in aerial silks.

Ariel Dempsey ni mwanafunzi wa mwaka wa nne wa udaktari ambaye anakaribia kuhitimu kutoka chuo kikuu cha Jimbo la Michigan akiwa na shahada ya Udaktari na akielekea kukamilisha shahada ya Udaktari wa Falsafa (PhD) katika sayansi na dini katika chuo kikuu cha Oxford. Anatazamia kuwa daktari wa kuhudumia watu wasiojiweza akihusisha elimu ya udaktari na ya dini. Ukiacha masomo yake, Ariel anapenda dansi la kuzunguka angani na sanaa ya sarakasi. Ni sehemu ya kikundi huko Grand Rapids kiitwacho Bangarang Circus na amesafiri pwani ya California akitumbuiza mitaani kuchangisha pesa kwa ajili ya kusaidia shirika la WorldVision na kuchangisha pesa kwa ajili ya huduma za Afya.

Mazungumzo haya yalifanyika katika tukio la TEDx kwa kutumia muundo wa mkutano wa TED lakini likiandaliwa na jamii ya watu wa eneo husika. Jifunze zaidi hapa https://www.ted.com/tedx

more » « less
Video Language:
English
Team:
closed TED
Project:
TEDxTalks
Duration:
17:36

Swahili subtitles

Revisions