< Return to Video

UPONYAJI dhidi ya UGONJWA WA TUMBO(GASTRITIS) nchini Marekani! | Ushuhuda wa Maombi ya Mtandaoni

  • 0:01 - 0:06
    Baada ya maombi, nilienda na kula chakula cha aina hiyo ambacho kawaida kinaweza kunisababishia maumivu.
  • 0:06 - 0:10
    na sikuhisi maumivu tena - hadi leo!
  • 0:14 - 0:20
    USHUHUDA
  • 0:21 - 0:27
    Kwa mamlaka katika jina la Yesu Kristo, pokea uhuru wako!
  • 0:27 - 0:30
    Pokea uponyaji wako!
  • 0:30 - 0:32
    Pokea mafanikio yako!
  • 0:32 - 0:35
    Pokea marejesho!
  • 0:35 - 0:41
    Pokea! Pokea leo!
  • 0:42 - 0:52
    Jina langu ni Merick, na ninapatikana Knoxville, Tennessee, Marekani.
  • 0:52 - 1:03
    Ninatoka Afrika Mashariki, Tanzania,
    na nilikuja hapa mwaka wa 2007.
  • 1:03 - 1:13
    Tangu wakati huo, baada ya miaka mitano hivi kupita, nilianza kuona mabadiliko fulani.
  • 1:13 - 1:18
    Nilikuwa nikipata maumivu ndani ya
    tumbo langu, maumivu mengi,
  • 1:18 - 1:24
    hasa nilipokula maharagwe,
    nyanya au maji ya limao.
  • 1:24 - 1:31
    Nilikuwa nikipata maumivu mengi,
    kwa hiyo niliishi nayo kwa muda.
  • 1:31 - 1:37
    Ndipo nikaamua kwenda kumwona daktari na wakapanga miadi.
  • 1:37 - 1:44
    Siku ya matibabu,
    ambapo waliniwekea kamera,
  • 1:44 - 1:51
    matokeo yalikuja kuwa nilikuwa na gesi -
    kulikuwa na gesi nyingi ndani yangu.
  • 1:51 - 1:56
    Waliutaugonjwa wa tumb( gastritis),
    ambao ulisababisha maumivu mengi.
  • 1:56 - 1:59
    Hata wakati fulani nilihisi maumivu ya moyo.
  • 1:59 - 2:05
    Hapo awali, nilikuwa nikifikiria ni suala la moyo - kana kwamba nilikuwa karibu kupata mshtuko wa moyo.
  • 2:05 - 2:08
    Kisha, nilikuwa nikipata maumivu mengi ya kichwa.
  • 2:08 - 2:14
    Kwa hiyo waliniwekea dawa
    na nilikuwa natumia dawa
  • 2:14 - 2:20
    kupunguza gesi kwa sababu hakuna dawa ya kuponya hali hiyo.
  • 2:20 - 2:25
    Niliendelea kunywa dawa.
  • 2:25 - 2:30
    Mwishoni mwa siku, nilifikiri, 'Nitaendelea kutumia dawa sikuzote.'
  • 2:30 - 2:41
    Kisha nikasema, 'Hapana, ninaweza kumwamini Mungu kwa sababu najua Mungu anaweza kuleta mabadiliko ndani yangu.'
  • 2:41 - 2:48
    Na niliendelea kuomba - lakini bado nilikuwa nikipata maumivu ndani yangu.
  • 2:48 - 2:53
    Niliacha kutumia dawa, hivyo kila
    nilipokula vyakula hivyo...
  • 2:53 - 2:57
    Kwa sababu sikuweza kuacha kula chakula walichoniambia niache,
  • 2:57 - 3:03
    ambacho nilikuwa nakula tangu nikiwa Afrika.
  • 3:03 - 3:07
    Nilipata maumivu hayo
    kwa karibu miaka minane.
  • 3:07 - 3:16
    Siku moja nilikuwa kwenye mitandao ya kijamii - na nilimfahamu Ndugu Chris tangu alipokuwa SCOAN.
  • 3:16 - 3:23
    Niligundua alirudi UK,
    na niliendelea kumfuatilia.
  • 3:23 - 3:26
    Ninajua yeye ni mtu mzuri, mnyenyekevu wa Mungu.
  • 3:26 - 3:31
    Na niliona jinsi watu walivyoungana naye na jinsi alivyokuwa akiwatia moyo.
  • 3:31 - 3:36
    Kwa hiyo nilibarikiwa sana na
    motisha yake.
  • 3:36 - 3:41
    Niliendelea kujipa moyo kwa kila alichonitia moyo.
  • 3:41 - 3:44
    Niliendelea kuungana na
    kujipa moyo kwa hilo.
  • 3:44 - 3:49
    Na kisha nikaona kiungo cha mtandao kuhusu
    jinsi ya kuunganishwa kwa maombi.
  • 3:49 - 3:59
    Najua Roho wa Mungu alikuwa akinielekeza kufuata kiungo hicho na kuwasilisha ombi langu la maombi.
  • 3:59 - 4:05
    Nilipotuma ombi langu, nilialikwa kujiunga na Maombi ya Pamoja mnamo Mei 4, 2024.
  • 4:05 - 4:09
    Niliunganisha kwenye ibada,
    nikingoja Ndugu Chris aje.
  • 4:09 - 4:14
    Kwa hiyo nilipokuwa nimeunganishwa,
    ulikuwa ni wakati wa shuhuda.
  • 4:14 - 4:24
    Niliunganishwa, nikisikiliza watu wakishuhudia kile ambacho Mungu alikuwa amefanya katika maisha yao.
  • 4:24 - 4:28
    Mtu wa mwisho, mwanamke kutoka Afrika Kusini,
  • 4:28 - 4:35
    alikuwa akishuhudia kuhusu tatizo lilelile
    nililokuwa nikipitia wakati huo.
  • 4:35 - 4:37
    Hivyo ndivyo alivyokuwa akishuhudia.
  • 4:37 - 4:44
    Nilijua kwamba ilikuwa ni miadi ya kiungu, na nilijua nilikuwa nikipokea uponyaji wangu
  • 4:44 - 4:51
    pale pale baada ya kuamini kuwa Mungu akimponya, angeniponya mimi pia.
  • 4:51 - 4:59
    Kwa hiyo niliendelea na maombi, nikiamini ‘leo ni siku yangu’ na ningepokea uponyaji wangu.
  • 4:59 - 5:06
    Ndugu Chris alipokuja, tuliungana katika maombi. Tuliomba na kuomba.
  • 5:06 - 5:13
    Na tangu wakati huo,
    nilianza kuhisi mabadiliko ndani yangu.
  • 5:13 - 5:18
    Nilianza kuhisi amani.
    Sikuhisi maumivu ya aina yoyote.
  • 5:18 - 5:25
    Na baada ya maombi, nilienda na kula chakula cha aina hiyo ambacho kawaida kingeniletea maumivu.
  • 5:25 - 5:28
    na kamwe sikuhisi maumivu tena - hadi leo!
  • 5:28 - 5:32
    Mungu anaweza na amenitendea.
  • 5:32 - 5:40
    Ninapokula maharagwe au aina yoyote ya chakula kilicho na limao, nyanya au vitu kama hivyo,
  • 5:40 - 5:41
    Sijisikii maumivu tena.
  • 5:41 - 5:50
    Au nikinywa matunda ya mpasheni au juisi ya machungwa,
    siumii tena.
  • 5:50 - 5:52
    Kwa hivyo hakuna maumivu tena.
  • 5:52 - 5:56
    Na kwa kweli, nilikuwa na
    wakati mgumu kulala.
  • 5:56 - 6:00
    Nilipokula, nililazimika
    kulala upande mmoja.
  • 6:00 - 6:05
    Kwa sababu wakati mwingine nilihisi
    kujaa gesi tumboni wakati nimelala.
  • 6:05 - 6:12
    Ningelazimika kutumia mto
    kuinua kichwa changu wakati nimelala.
  • 6:12 - 6:14
    Lakini Mungu alifanya hivyo kwa ajili yangu.
  • 6:14 - 6:20
    Ninataka kuwaambia watu - Mungu wetu ni wa ajabu
    na Yeye ni Baba mwenye upendo.
  • 6:20 - 6:26
    Anajua tunachohisi.
    Anajua uchungu wetu. Anajua kilio chetu.
  • 6:26 - 6:31
    Na daima hutuwekea miadi mitakatifu.
  • 6:31 - 6:34
    Yeye daima anahisi kile tunachohisi.
  • 6:34 - 6:38
    Hakuna mtu anayeweza kuhisi jinsi tunavyohisi - kama Mungu.
  • 6:38 - 6:43
    Hakuna anayeweza kuona machozi yetu - kama Mungu.
  • 6:43 - 6:48
    Kwa hiyo Mungu anatuhurumia siku zote.
  • 6:48 - 6:51
    Kama mtoto wa Mungu, lazima pia uamini.
  • 6:51 - 6:57
    Ikiwa Mungu alinifanyia mimi, atakufanyia wewe pia. Yeye ni Mungu mwema!
Title:
UPONYAJI dhidi ya UGONJWA WA TUMBO(GASTRITIS) nchini Marekani! | Ushuhuda wa Maombi ya Mtandaoni
Description:

Wakati Merick, Mtanzania anayeishi Marekani, akisikiliza ushuhuda wa TV Ya Moyo Wa Mungu kutoka kwa mwanamke mmoja wa Afrika Kusini, imani yake ilichochewa - kwani Mungu alimponya kutoka katika hali ile ile aliyokuwa nayo. Unaposikiliza ushuhuda wake, tunaomba imani yako mwenyewe itachochewa kumwamini Mungu kwa muujiza wako mwenyewe!

Ili kupokea kwa uhuru Maombi ya Pamoja kutoka kwa Ndugu Chris kwenye Zoom, tafadhali wasilisha ombi lako la maombi hapa - https://www.godsheart.tv/zoom

➡️ Pata Kutiwa Moyo Kila Siku kwenye WhatsApp - https://godsheart.tv/whatsapp/
➡️ Kuwa Mshirika wa TV wa Moyo wa Mungu - https://godsheart.tv/partnership
➡️ Habari kuhusu Maombi ya Mwingiliano - https://godsheart.tv/interactive-prayer/
➡️ Jitolee kama Mtafsiri wa TV ya Moyo wa Mungu - https://godsheart.tv/translate/
➡️ Shirikisha ushuhuda wako - https://godsheart.tv/testimony
➡️ Jiunge na Ibada yetu ya Maombi ya Moja kwa Moja Jumamosi ya kwanza ya kila mwezi - https://www.youtube.com/godshearttv/live

more » « less
Video Language:
English
Team:
God's Heart TV
Duration:
07:27

Swahili subtitles

Revisions Compare revisions