Roho Mtakatifu HUFANYA KAZI APENDAVYO!
-
0:00 - 0:02Kupitia safari hiyo ya uponyaji wangu,
-
0:02 - 0:07Nilitambua kwamba niliongezeka zaidi katika imani
na nikamkaribia Mungu zaidi, -
0:07 - 0:11na uhusiano wangu na Bwana na Mwokozi wangu Yesu Kristo kwa kweli uliboreka.
-
0:18 - 0:21Sawa, ndugu yetu wa Zambia - tuombe.
-
0:21 - 0:27Katika jina la Yesu Kristo!
-
0:27 - 0:36Sasa hivi kila uharibifu kwenye misuli yako, kwenye mifupa yako – urejeshwe kwa jina la Yesu!
-
0:36 - 0:41Urejeshwe kwa jina la Yesu.
-
0:41 - 0:46Ndugu, unaweza kuniinua mguu wako?
-
0:46 - 0:53Katika jina la Yesu Kristo,
uwe mzima sasa hivi. -
0:53 - 1:04Kila maumivu - toka kwake,
kwa jina la Yesu Kristo. -
1:04 - 1:05Asante, Roho Mtakatifu.
-
1:05 - 1:09Ndugu, uko huru kwa utukufu wa Mungu.
-
1:09 - 1:12Unaweza kujiangalia sasa hivi.
-
1:12 - 1:16Najua hutaweza
kuiondoa piopi kwa sasa, -
1:16 - 1:19lakini unaweza kujua kwamba
Mungu amekugusa. -
1:19 - 1:22Jiangalie tu na umshukuru
Mungu kwa uponyaji wako. -
1:22 - 1:23Asante, Bwana.
-
1:25 - 1:31Jina langu ni Francis na
ninatoka Zambia, Afrika. -
1:31 - 1:39Mwaka jana mwezi wa Machi, nilivunjika kigoko(fibula) nilipokuwa nikicheza soka.
-
1:39 - 1:49Lakini hali ya jeraha na mambo ambayo yalisababisha hayakuwa ya asili.
-
1:49 - 1:53Kwa hivyo ilikuwa suala ambalo mahali pa kazi yangu,
-
1:53 - 1:59Nilikuwa katika nafasi ya kaimu
mkuu wa idara. -
1:59 - 2:05Kwa hiyo kwa fursa hiyo, nilileta kipengele cha kuwa na Maandiko na sala
-
2:05 - 2:09mahali pangu pa kazi,
ambayo ni taasisi ya kujifunza. -
2:09 - 2:12Kwa hivyo siku ya Ijumaa, tulikuwa na maombi na wanafunzi.
-
2:12 - 2:17Tulimsifu Bwana, tukashiriki Neno la Mungu, na nilijua hivi ndivyo inavyopaswa kuwa.
-
2:17 - 2:26Siku iliyofuata, Jumamosi, nilienda kucheza mpira wa miguu na marafiki zangu, kama nilivyokuwa nikifanya siku zote.
-
2:26 - 2:31Kabla sijaenda kucheza mechi ya mpira wa miguu,
nilipokea ujumbe mfupi wa maandishi -
2:31 - 2:37kutoka kwa mmoja wa wanafunzi waliokuwa kwenye mkutano wa maombi tuliokuwa nao siku iliyotangulia.
-
2:37 - 2:41Alikuwa na ndoto ambapo aliona
ninashambuliwa - -
2:41 - 2:44kulikuwa na shambulio la karibu
kwenye maisha yangu. -
2:44 - 2:48Kwa hivyo katika siku hiyo ya kutisha,
Jumamosi hiyo hiyo, moyo wangu ... -
2:48 - 2:53Unajua, moyo unajua wakati kitu kibaya lakini nilipuuzia tu
-
2:53 - 2:56nikasema, Baba, mapenzi yako yatimizwe;
-
2:56 - 2:59kwa sababu sikujua jinsi
shambulio hilo lingekuja. -
2:59 - 3:02Nilimshukuru Mungu kwa kila jambo
na kuendelea kucheza soka. -
3:02 - 3:13Kwa hivyo mechi ilianza karibu saa 11 jioni. Ardhi ilikuwa na unyevu kwa sababu ilikuwa imetoka tu kunyesha.
-
3:13 - 3:16Kwa hivyo katika siku hiyo jaala, kufupisha hadithi hii ndefu, nilipokuwa nikicheza,
-
3:16 - 3:20Niliteleza kwenye makabiliano nikijaribu kucheza mpira.
-
3:20 - 3:24Sikuwa na mawasiliano na mchezaji yeyote, wala sikupiga chochote kigumu.
-
3:24 - 3:27Lakini baada ya kuteleza tu kwenye chenga rahisi,
-
3:27 - 3:30nilipokuwa chini,
niliweza kuhisi kwamba kigoko(fibula) yangu ilivunjika. -
3:30 - 3:35Kwa hivyo mara moja, wenzangu wengi walidhani ninacheza au nikijifanya kuanguka tu,
-
3:35 - 3:37kwa hivyo labda nisingeweza
kushiriki katika mchezo. -
3:37 - 3:43Lakini hapohapo, niliweza kuhisi mfupa wangu ukisonga; Niliweza kuhisi maumivu makali.
-
3:43 - 3:46Na mara moja hili lilipotokea,
-
3:46 - 3:49ilinikumbusha ujumbe
nilioupokea siku hiyo ya maafa. -
3:49 - 3:54Baada ya hapo, nilikimbizwa hospitali
na kisha wakanifanyia X-ray. -
3:54 - 3:59Baada ya kunifanyia X-ray, ndivyo walivyogundua kuwa mfupa wangu wa kigoko(fibula) ulikuwa umevunjika.
-
3:59 - 4:03na mvunjiko wa mfupa ulikuwa kana
kwamba nilipigwa na kitu -
4:03 - 4:07hiyo ilipelekea mifupa kutengana kabisa.
-
4:07 - 4:11Kwa hiyo, kilichofanyika nilipewa piopi.
-
4:11 - 4:18Hiyo piopi niliyopewa ndiyo inayoonyeshwa kwenye video uliyoiona.
-
4:18 - 4:23Na kisha, bila shaka, niliweka dawa za kutuliza maumivu na pia dawa zingine.
-
4:23 - 4:27Lakini nilikuwa na maumivu makali
na nilipewa magongo. -
4:27 - 4:32Kwa hiyo siku hiyohiyo niliwasiliana na Timu ya TV ya Moyo wa Mungu na kueleza hali yangu yote.
-
4:32 - 4:37Na mara nikatuma ujumbe wangu,
Timu ya TV ya Moyo wa Mungu ikajibu. -
4:37 - 4:44Katika siku hiyo ya mahsusi, kwakweli, Ndugu Chris alihubiri Neno la Mungu kwetu
-
4:44 - 4:45kabla ya kutuombea.
-
4:45 - 4:48Alisema kitu ambacho sijawahi
kusahau hadi leo. -
4:48 - 4:53Alisema jambo muhimu, na
ninaamini aliongozwa na Roho Mtakatifu, -
4:53 - 4:56juu ya nini kitatokea, haswa kuhusu hali yangu.
-
4:56 - 5:00Kwa hivyo katika hali nyingi,
ninapotazama TV ya Moyo wa Mungu, -
5:00 - 5:03Ningeona watu wakiombewa ungeona uponyaji mara moja.
-
5:03 - 5:05Watu wangehisi kitu.
-
5:05 - 5:08Wengine wangehisi umeme.
Kwa wengine, itakuwa joto. -
5:08 - 5:10Wangehisi mambo mengi.
-
5:10 - 5:14Lakini kabla Ndugu Chris hajasali kwa ajili ya yeyote kati yetu siku hiyo, alitaja jambo fulani.
-
5:14 - 5:21Alisema, “Unapoombewa, Roho Mtakatifu hufanya kazi apendavyo yeye.”
-
5:21 - 5:26Kwa hivyo hiyo inamaanisha ni kwamba sio lazima uhisi kitu,
-
5:26 - 5:29au nilazima uanguke, au nilazima ujidhihirishe au kwa namna yeyote,
-
5:29 - 5:33kwa sababu tunapokuja kwenye maombi,
tunakuja tukiwa na matarajio mengi. -
5:33 - 5:35Labda utafikiri kwamba
wanapokuombea, -
5:35 - 5:38ili ujue kuwa umepona,
lazima uhisi aina fulani ya umeme. -
5:38 - 5:40Lazima uhisi kitu.
-
5:40 - 5:45Wakati mwingine Roho Mtakatifu - hata hutahisi chochote, lakini Mungu atakuponya.
-
5:45 - 5:50Kwa hiyo Ndugu Chris alivyonifanyia maombi, ilipofika zamu yangu ya maombi,
-
5:50 - 5:55jambo moja ninalokumbuka ni kwamba, nililoweza kuhisi ni kwamba -
nilikuwa na amani ya moyo. -
5:55 - 5:56Hilo ndilo lilikuwa jambo la kwanza nililokuwa nalo.
-
5:56 - 5:58Bila shaka, kulikuwa na mambo mengi
ambayo nilikuwa nikipitia. -
5:58 - 6:00Mvunjiko wa mfupa ulikuwa ni kitu kimoja tu kati ya hayo.
-
6:00 - 6:05Lakini nilikuwa na amani ya moyo na jambo moja ambalo lilikuwa dhahiri kimwili lilikuwa
-
6:05 - 6:08kwamba, maumivu yaliyokuwa kwenye mguu wangu yalipungua.
-
6:08 - 6:12Zaidi ya hayo, sikuhisi aina yoyote ya ...
-
6:12 - 6:15Sikuhisi chochote zaidi
ya maumivu kupungua -
6:15 - 6:21na amani ya moyo ambayo niliipata siku ile ya maafa niliombewa.
-
6:21 - 6:23Na niliweza kupata
nguvu kwenye mguu wangu -
6:23 - 6:27kwa sababu, wakati huo, nilikuwa na maumivu makali.
-
6:27 - 6:32Kwangu mimi, maombi na uzoefu wote ilikuwa ni zaidi ya kuvunjika mguu tu,
-
6:32 - 6:35kwa sababu ninaamini nilikuwa na
mpasuko katika imani yangu. -
6:35 - 6:42Kwa hivyo kupitia uzoefu, uponyaji wangu
ulikuwa maalum kabisa. Ninauchukua kama maalum. -
6:42 - 6:46Baada ya Ndugu Chris kusali,
jambo alilotaja lilikuwa -
6:46 - 6:51kwamba kipengele chochote cha kiroho
kilichosababisha mpasuko -
6:51 - 6:54na kilichoweza kusababisha
matatizo kiondolewe. -
6:54 - 6:58Kwa hivyo katika kisa changu, uponyaji wangu
ulichukua 'zamu ya asili' katika hilo -
6:58 - 7:02Sikupokea
muunganiko wa mfupa mara moja. -
7:02 - 7:07Ilichukua muda na kupitia
safari hiyo ya uponyaji wangu, -
7:07 - 7:11Nilitambua kwamba niliongezeka zaidi katika imani
na nikamkaribia Mungu zaidi, -
7:11 - 7:15na uhusiano wangu na Bwana na Mwokozi wangu Yesu Kristo kwa kweli uliboreka.
-
7:15 - 7:19Sawa, kwa hivyo nina uhakika watu wanaweza
kuona X-rays mbili. -
7:19 - 7:23Ile ya kushoto ni kabla ya maombi.
-
7:23 - 7:30Ile iliyo upande wa kulia ni baada ya maombi,
ambayo niliyapata takriban wiki mbili zilizopita. -
7:30 - 7:34Kwa hivyo hiyo ndiyo ambayo sasa inaonyesha uponyaji wangu kwa sasa.
-
7:34 - 7:37Na utukufu ni kwa Mungu - mifupa yangu imeunganishwa.
-
7:37 - 7:43Yote kwa yote, jeraha langu limepona
na Mungu ameponya maisha yangu. -
7:43 - 7:47Kwa hivyo ikiwa uliona kwenye video,
sikuweza kusimama peke yangu. -
7:47 - 7:49Kwa hiyo kusimama lilikuwa tatizo.
-
7:49 - 7:55Lakini sasa, ninaweza kusimama kwa
miguu yangu miwili kama watu wanavyoona. -
7:55 - 8:00Na, naweza pia kujisawazisha. Kwa hivyo huu ndio mguu
ambao uliathiriwa - mguu wa kushoto. -
8:00 - 8:03Unaweza kuona ninaweza kujisawazisha
na kuwa na nguvu kwenye mguu wangu. -
8:03 - 8:11Ninaweza kujongea kwa uhuru, naweza kutembea kwa uhuru, naweza kuruka na kufanya shughuli nyingi za kimwili
-
8:11 - 8:15ambazo sikuweza kufanya wakati huo.
Hakuna maumivu katika mfupa! -
8:15 - 8:20Unaweza hata kuona jinsi mguu wangu unavyoonekana -
wengine hawawezi hata kusema kuwa nimevunjika. -
8:20 - 8:23Imepona vizuri na
hakuna ulemavu kwenye mguu wangu. -
8:24 - 8:30Napenda kuwashauri tu
ndugu zangu - -
8:30 - 8:32unapokaribia kupokea maombi,
-
8:32 - 8:39moja ya mambo ya kukumbuka ni kwamba huwezi kumpendeza Mungu bila imani (Waebrania 11:6).
-
8:39 - 8:43Kwa hiyo naamini, kwa kadiri tunavyotaka kupokea uponyaji wa kimwili
-
8:43 - 8:45au maombi kwa aina yoyote ya shida tuliyo nayo,
-
8:45 - 8:49kwanza tunapaswa kuamini kwamba Mungu
atatuponya matatizo yetu. -
8:49 - 8:54Na kisha Mungu anapotuponya,
Mungu anataka wokovu kwa ajili yetu. -
8:54 - 8:58Kwa hiyo inampasa kwanza kujenga
uhusiano huo ndani yetu pamoja naye -
8:58 - 9:01hiyo itatuwezesha kudumisha uponyaji.
-
9:01 - 9:05Kwa sababu ninaweza kupokea uponyaji leo,
lakini ikiwa sitadumisha uhusiano wangu -
9:05 - 9:08pamoja na Bwana na Mwokozi wangu Yesu Kristo,
ninaweza kupoteza baraka hiyo. -
9:08 - 9:11Najua wengine wanaomba
kupandishwa vyeo, ajira - -
9:11 - 9:13kuna mambo mengi sana ambayo
watu wanaomba. -
9:13 - 9:17Lakini jambo la muhimu zaidi ni - utadumishaje baraka?
-
9:17 - 9:21Na katika kisa changu, Mungu alinionyesha uvumilivu na pia ustahamilifu.
-
9:21 - 9:23na jinsi ya kudumisha baraka yangu.
-
9:23 - 9:28Na hadi leo, ninashukuru kwa zawadi nyingi ambazo Mungu ameonyesha maishani mwangu.
- Title:
- Roho Mtakatifu HUFANYA KAZI APENDAVYO!
- Description:
-
Francis alivunjika kigoko(fibula) alipokuwa akicheza soka na marafiki zake nchini Zambia - lakini hali iliyopelekea kuumia kwake haikuwa ya kawaida.
Baada ya kupokea maombi katika jina la Yesu Kristo kutoka kwa Ndugu Chris, maumivu yaliondoka mara moja na amani ikaja papo hapo. Kilichofuata ni safari ya pekee ya kupona, ambayo hatimaye ilimtia nguvu kiroho. Tunaomba utiwe moyo na ushuhuda wake, tukijua kwamba Roho Mtakatifu anafanya kazi kama apendavyo na inapokuja suala la kuingilia kati kwa Mungu, hatuwezi kutenganisha suluhisho na wokovu!
Ili kupokea maombi bila malipo kutoka kwa Ndugu Chris kupitia Zoom, wasilisha ombi lako la maombi hapa - https://www.godsheart.tv/zoom
➡️ Pata Kutiwa Moyo Kila Siku kwenye WhatsApp - https://godsheart.tv/whatsapp/
➡️ Kuwa Mshirika wa TV wa Moyo wa Mungu - https://godsheart.tv/partnership
➡️ Habari kuhusu Maombi ya Pamoja - https://godsheart.tv/interactive-prayer/
➡️ Jitolee kama Mtafsiri wa TV ya Moyo wa Mungu - https://godsheart.tv/translate/
➡️ Shirikisha ushuhuda wako - https://godsheart.tv/testimony
➡️ Jiunge na Ibada yetu ya Maombi ya Moja kwa Moja Jumamosi ya kwanza ya kila mwezi - https://www.youtube.com/godshearttv/live - Video Language:
- English
- Team:
God's Heart TV
- Duration:
- 09:59
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for The Holy Spirit WORKS As He WILLS! | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for The Holy Spirit WORKS As He WILLS! | |
![]() |
georgejbudeba edited Swahili subtitles for The Holy Spirit WORKS As He WILLS! |