< Return to Video

CCOAN Thessalonica MoG George Athanasiadis First Speech 2024 08 25 V2

  • 0:00 - 0:04
    [♪ Muziki ♪]
  • 0:04 - 0:07
    Na tumruhusu ndugu yetu George Athanasiadis aje mbele.
  • 0:07 - 0:27
    [Makofi]
  • 0:27 - 0:30
    Emmanuel! (Mungu yu pamoja nasi - Mathayo 1:23).
  • 0:30 - 0:36
    Jina langu ni George Athanasiadis, na kwa matunda yetu...
  • 0:36 - 0:46
    [Makofi],
  • 0:47 - 0:50
    Kwa matunda yetu mtatutambua.
  • 0:51 - 0:55
    Nataka kumshukuru Mungu Mwenyezi kwa siku hii.
  • 0:55 - 0:59
    Kwa neema Yake na rehema Zake alizonipa.
  • 0:59 - 1:05
    na hazikuniacha nikizurura ulimwenguni kama mamilioni ya watu wanavyofanya.
  • 1:05 - 1:12
    Namshukuru Baba yetu, Bwana Yesu Kristo na Roho Mtakatifu katika jina la Yesu Kristo.
  • 1:12 - 1:18
    [Makofi]
  • 1:19 - 1:24
    Pia ningependa kumshukuru mtumishi wa Mungu Harry,
  • 1:24 - 1:31
    nabii wa kizazi hiki, kamanda na jenerali wa Mungu Mwenyezi.
  • 1:31 - 1:37
    [Makofi]
  • 1:37 - 1:40
    Nabii wa Bwana Mwenyezi,
  • 1:40 - 1:43
    Bwana wa mabwana wote.
  • 1:43 - 1:47
    Nakushukuru, mtumishi wa Mungu, kwa sababu mimi ni jinsi nilivyo kwa sababu yako.
  • 1:48 - 1:50
    Mimi ni jinsi nilivyo kwa sababu yako.
  • 1:50 - 1:52
    Asante kwa uvumilivu wako.
  • 1:52 - 1:57
    Kwa kunichukua (chini ya ulinzi wako) nikiwa dhaifu, katika dhambi.
  • 1:57 - 2:01
    Kwa kunikubali karibu nawe, katika uanafunzi.
  • 2:02 - 2:07
    Kwa kunirekebisha, kunionya kwa hekima ya Mungu.
  • 2:07 - 2:10
    Kwa kunisaidia kukua kiroho
  • 2:10 - 2:14
    Kwa kunisafisha, kunisaidia kupigana na udhaifu wangu,
  • 2:14 - 2:18
    Kwa kunishauri wakati nilipohitaji ushauri wako.
  • 2:18 - 2:25
    Kwa uvumilivu mkubwa kama wa Ayubu, ulinilea.
  • 2:25 - 2:27
    Nakushukuru mtumishi wa Mungu Harry!
  • 2:27 - 2:28
    Mungu akubariki!
  • 2:28 - 2:33
    [ Makofi]
  • 2:33 - 2:40
    Furaha ya Roho Mtakatifu ni kubwa mno ndani yangu sasa.
  • 2:41 - 2:45
    Ningependa kusema machache kuhusu maisha yangu hadi leo hii.
  • 2:46 - 2:47
    Kuhusu malezi yangu.
  • 2:48 - 2:52
    Nilipokuwa nikifikiria kuhusu maisha yangu kufikia hatua hii,
  • 2:52 - 2:56
    I realised that God has saved my life many times over, niligundua kuwa Mungu amenilinda maisha yangu mara nyingi,
  • 2:56 - 2:58
    kutoka kwa mambo ambayo hata sikuyatambua.
  • 2:59 - 3:06
    Nilipokuwa mdogo sana, miezi michache au hata siku chache tu, nilipatwa na bronkiti kali.
  • 3:06 - 3:10
    Ambayo ni hatari sana kwa mtoto mchanga.
  • 3:10 - 3:16
    Kwa kawaida huacha madhara ya muda mrefu, kama vile pumu sugu au matatizo ya kupumua.
  • 3:16 - 3:22
    Lakini Bwana Yesu Kristo, kwa neema Yake, aliniponya, na sikupata madhara hayo.
  • 3:22 - 3:31
    Baadaye, nilipokuwa nikikua, nilipata degedege mara tatu, nikiwa mtoto mdogo wa miaka michache tu.
  • 3:31 - 3:34
    Jambo ambalo ni gumu sana kwa wazazi kuwa nalo.
  • 3:34 - 3:40
    Walipeleka hospitalini na kuhusu degedege, mara nyingi hupelekea kugunduliwa kuwa na kifafa.
  • 3:40 - 3:43
    Lakini tena, kwa neema na rehema Zake, sikuwa na kifafa.
  • 3:43 - 3:46
    Bwana alinilinda na kuniponya.
  • 3:46 - 3:50
    Nilipofikia takriban miaka 17,
  • 3:50 - 3:55
    nilikuwa napata maumivu makali machoni mara kwa mara.
  • 3:55 - 4:03
    Kwa sababu hiyo, ilinibidi kufunga madirisha yote chumbani ili kusiwe chanzo cha mwanga kiweze kuonekana, na nililala chini ya blanketi.
  • 4:03 - 4:09
    Macho yangu yalikuwa yananiuma sana, kiasi kwamba nilikuwa najitahidi kulala ili maumivu yapungue.
  • 4:10 - 4:15
    Baada ya muda fulani, niligundulika kuwa na sinusitis ya ndani ya fuvu.
  • 4:15 - 4:22
    Daktari aliniandikia dawa na akatuambia kwamba ikiwa haitafanya kazi, tutaona cha kufanya baadaye.
  • 4:23 - 4:30
    Tulimuuliza maana yake ni nini na daktari alionekana kuwa na wasiwasi na hakutaka kusema zaidi.
  • 4:30 - 4:39
    Kwa neema ya Mungu, tulikuwa na maji ya asubuhi ambayo T. B. Joshua alikuwa ameombea na kututumia.
  • 4:40 - 4:46
    Nilinyunyiza maji hayo ya asubuhi juu yangu, na usiku ule ule pua yangu hatimaye ilifunguka.
  • 4:46 - 4:51
    Nilipoamka, niliona kitandani mwangu, karibu na mto wangu, dimbwi la damu.
  • 4:51 - 4:52
    Bwana...
  • 4:53 - 4:59
    [Makofi]
  • 5:00 - 5:03
    Bwana aliniponya na sikuwa na maumivu machoni tangu siku hiyo.
  • 5:03 - 5:10
    Kwa hivyo, nilikuwa nikifikiria yote hayo na kutambua ukubwa wa neema ya Mungu maishani mwangu.
  • 5:10 - 5:13
    Ambayo imenihifadhi hai hadi leo na namshukuru.
  • 5:13 - 5:16
    Kwa rehema Zake za kiungu na neema Yake.
  • 5:16 - 5:23
    Kuhusu mambo ya Mungu na nafasi yangu ndani yake, namshukuru Mungu kwa kuwatumia wazazi wangu.
  • 5:24 - 5:29
    Kwa kuwa Wakristo waaminifu na kunisaidia kufikisha chochote walichoweza kutoka kwa Neno la Mungu kwangu.
  • 5:29 - 5:32
    Kuchukua hatua za dhati kuelekea kwa Mungu.
  • 5:32 - 5:38
    Kwa kweli, walikuwa wakitafuta kwa bidii nguvu halisi za Mungu, wakipita zaidi ya kile walichokijua tayari.
  • 5:38 - 5:42
    Ili kushuhudia Mungu akifanya kazi, kama alivyofanya katika enzi za kitume za kanisa.
  • 5:42 - 5:48
    Alipomtumia Mwanawe, Yesu Kristo, kuponya, kukomboa, kutabiri (kwa watu).
  • 5:48 - 5:55
    Na kwa njia ya ajabu, Mungu alimtuma dada mmoja kutoka Athene kuzungumza na wazazi wangu.
  • 5:55 - 6:00
    Akawapa kanda za video tulizokuwa nazo wakati mmoja.
  • 6:01 - 6:09
    Zikionyesha Nabii T. B. Joshua akiomba, akiponya, akitoa watu kwa nguvu za Roho Mtakatifu.
  • 6:10 - 6:12
    Wazazi wangu walifurahia sana.
  • 6:12 - 6:18
    Walipenda huduma hii kwa sababu, kama unavyojua, Roho Mtakatifu ndiye anayetuongoza na kutuweka ndani yake.
  • 6:18 - 6:20
    Kutupatia tamaa hii.
  • 6:20 - 6:24
    Hivyo basi, aliwapa wazazi wangu tamaa hii, ambao walijikita kabisa katika huduma hii
  • 6:24 - 6:27
    Baadaye, walianza kutazama Emmanuel TV.
  • 6:27 - 6:31
    Emmanuel TV ilikuwa ni kituo cha setilaiti cha Nabii T. B. Joshua.
  • 6:32 - 6:35
    Sisi watoto pia tulianza kutazama.
  • 6:35 - 6:41
    Kila Jumapili, watu walikuwa wakikusanyika nyumbani kwetu na katika nyumba nyingine za ndugu zetu, wakitazama Emmanuel TV.
  • 6:41 - 6:46
    Wakiona nguvu za Mungu zikifanya kazi kupitia Nabii T. B. Joshua.
  • 6:46 - 6:52
    Wakati fulani, tulitambua kwamba mtu fulani, Mgriki aliyeitwa Charalambos Tsakonidis,
  • 6:52 - 6:55
    alikuwa mwanafunzi wa Nabii T. B. Joshua.
  • 6:56 - 7:02
    [Makofi]
  • 7:03 - 7:13
    Haikuchukua muda mrefu baada ya hapo, ndugu Charalambos Tsakonidis akawa baba, mshauri, mtumishi wa Bwana aliyejazwa upako.
  • 7:13 - 7:16
    Nabii na jemadari wa Bwana Mwenyezi!
  • 7:16 - 7:22
    [Makofi]
  • 7:22 - 7:32
    Kisha akatokea kwenye Emmanuel TV, mtumishi wa Mungu Harry, na kusema kwamba yeye ni Charalambos Tsakonidis na kwamba alikuwa anakuja Ugiriki,
  • 7:33 - 7:39
    na moto wa Roho Mtakatifu kuanzisha huduma na kuhubiri Roho wa Mungu nchini Ugiriki!
  • 7:39 - 7:40
    Amina!
  • 7:40 - 7:46
    [Makofi]
  • 7:48 - 7:55
    Hivyo, wakati uliobarikiwa wa Mungu ukafika, ambapo mtumishi wa Mungu Harry alikuja nchini kwetu
  • 7:55 - 8:00
    Kwa ustahimilivu mkubwa, alijenga huduma yake kutoka mwanzoni.
  • 8:00 - 8:06
    Aliwachukua wote waliompenda Mungu na waliotaka kushiriki, na akaanzisha huduma.
  • 8:06 - 8:11
    And ever since, it started growing exponentially by God's grace. Na tangu wakati huo, ilianza kukua kwa kasi kwa neema ya Mungu.
  • 8:11 - 8:16
    Wakati fulani, mpango wa kuwa wanafunzi ulianzishwa na mtumishi wa Mungu,
  • 8:16 - 8:24
    kwa sababu, kama Bwana wetu na Mwokozi alivyotuamuru, twende kwa mataifa na kufanya wanafunzi
  • 8:24 - 8:29
    kuwafundisha kufanya yale ambayo Bwana Yesu alifanya pia.
  • 8:29 - 8:35
    Hivyo mpango wa kuwa wanafunzi ukaanza, na muda mfupi baadaye, kwa neema ya Mungu, nilikubaliwa.
  • 8:36 - 8:42
    .Nikiwa kando yake, nilifundishwa uzoefu mwingi wa kiroho, nikajifunza mafundisho sahihi.
  • 8:42 - 8:50
    Nilimwona Mungu akifanya kazi mbele ya macho yangu, kama Yesu Kristo alivyofanya nyakati zile.
  • 8:50 - 8:56
    . [Makofi]
  • 8:56 - 9:05
    Nikiwa naye, nilisafiri kote ulimwenguni kwa ajili ya mikutano ya uamsho ya babu yetu, Nabii T. B. Joshua.
  • 9:06 - 9:13
    Kwa sababu tu nilikuwa mahali pazuri, kwa wakati mzuri, kando ya miguu ya mshauri wangu, nikafundishwa naye.
  • 9:13 - 9:16
    !Nilijifunza mengi kutoka kwake!
  • 9:16 - 9:23
    Kwa kifupi, katika miaka hii 9, Bwana alinipa maarifa na hekima Yake.
  • 9:24 - 9:31
    Namshukuru Mungu kwa kuniona nafaa leo kunitia mafuta na kunitumia kuwasaidia watu Wake.
  • 9:31 - 9:34
    Kuwakomboa na kuwaweka huru watu Wake.
  • 9:34 - 9:36
    Asante, Bwana Yesu Kristo!
  • 9:36 - 9:41
    [Makofi]
  • 9:41 - 9:43
    Kuna mambo matatu ya msingi tunayohitaji.
  • 9:43 - 9:48
    Kwanza kabisa, unahitaji fumbo la Neema ya Mungu.
  • 9:49 - 9:50
    Hii ni nini?
  • 9:50 - 9:59
    Fumbo la Neema ya Mungu ni kwamba linachukua watu wa kawaida na kuwaweka katika Ufalme Wake milele.
  • 9:59 - 10:08
    Ninaposema "wa kawaida", simaanishi wenye vipaji, werevu au wenye busara, bali wale ambao watu huwaona kuwa hawafai.
  • 10:09 - 10:17
    Wale ambao si wepesi, wenye busara wala wenye vipaji. Anawachukua, wapumbavu wa ulimwengu huu.
  • 10:17 - 10:21
    Na kuwaweka katika Ufalme Wake milele, ili mtu yeyote asijivune.
  • 10:21 - 10:25
    [Makofi]
  • 10:25 - 10:37
    Pili, unahitaji kumpata mshauri ambaye ni mwenye busara zaidi, mwenye akili zaidi na mwenye nguvu zaidi katika Bwana, ili kukuongoza katika njia za Bwana.
  • 10:37 - 10:41
    Nami namshukuru Bwana Yesu Kristo kwa mshauri wangu, mtumishi wa Mungu Harry.
  • 10:44 - 10:50
    Tatu, unahitaji kufanya uamuzi wa kuweka maono yako mbele ya mawazo yako.
  • 10:51 - 10:53
    Unajuaje umefanya hivyo?
  • 10:53 - 11:03
    Utajua, kwa sababu unapofanya hivyo, ghafla hakuna kitu kinachoweza kukufanya ulalamike, kwa sababu unajua kwamba unapolalamika unarudi nyuma.
  • 11:03 - 11:08
    Utajua kwamba huwezi kulalamika, kwa sababu kila hali inakuandaa kwa ajili ya maono yako.
  • 11:08 - 11:19
    Namshukuru Baba, Mwana na Roho Mtakatifu kwa Neema Yake kunifikia mimi, wa kawaida, nisiyefaa na kunifanya nistahili kwa ajili ya utukufu Wake.
  • 11:19 - 11:28
    Namshukuru mtumishi wa Mungu Harry tena, na namsalimu kwa jina la Yesu Kristo!
  • 11:28 - 11:42
    [♪ Muziki ♪]
Title:
CCOAN Thessalonica MoG George Athanasiadis First Speech 2024 08 25 V2
Description:

more » « less
Video Language:
Greek
Duration:
11:45

Swahili subtitles

Incomplete

Revisions Compare revisions