-
Asimilia tisaini ya ubongo wa mtoto
hukua kabla afike umri wa miaka mitano.
-
Afikapo miaka mitatu,
uunganisho wa ubongo wake
-
huwa umefikia kiwango
cha kwadrilioni tatu.
-
Kwa sababu ya uharaka huo,
wakati huu unaonekana
-
kuwa bora zaidi wa
kukuza ujuzi wa watoto
-
utakaowasaidia katika usomaji wa vitabu.
-
Walezi wanaeza wasaidia watoto
kwa kutumia hizi mbinu tano
-
zilizobuniwa na wataalamu
wa masomo ya watoto.
-
Ya kwanza, kusoma.
-
Akademia ya Madaktari ya Watoto
inashauri kuwa watoto wasomewe
-
vitabu kwa dakika ishirini kila siku.
-
Ya pili, kuimba.
-
Sababu nyimbo huleta hisia za furaha,
inashauriwa watoto waimbiwe
-
sababu itawasaidia kujifunza
kutamka maneno tofauti.
-
Ya tatu, kuongea.
-
Mazungumzo na watoto
ukizingatia ishara pia
-
huwasaidia kujifunza
kuongea na kujieleza.
-
Ya nne, kucheza.
-
Kucheza na watoto hukuza ubunifu
na kufikiria kwa watoto.
-
Ya tano, kuandika.
-
Kuandika hukuza uwezo
wa kushika na kushikilia vitu tofauti
-
kama vile vyombo vya jikoni.
-
Tafuta wakati katika siku na ujaribu
kutumia mbinu hizi tano na wanao
-
kama vile wakati wa kulala,
kuoga, kuvaa nguo na kadhalika.
-
Dakika kadhaa kila siku
zitawasaidia wanao kuwa tayari kusoma.
-
Tembelea Herrick.dl/EarlyLiteracy
kwa maelezo zaidi ya mbinu hizi tano.