< Return to Video

Maombi nchini Uingereza; Muujiza nchini NORWAY!

  • 0:00 - 0:07
    Nilitarajia. Nilijiambia,
    'Kisa hiki kimekaidi maarifa ya matibabu
  • 0:07 - 0:11
    na hakitapinga uwezo wa Mungu.'
  • 0:18 - 0:25
    Ikiwa bado kuna maumivu katika sehemu yoyote ya
    mwili wako, weka mkono wako hapo.
  • 0:25 - 0:34
    Popote pale maumivu hayo yalipo,
    katika jina la Yesu Kristo,
  • 0:34 - 0:37
    upako wa Roho Mtakatifu
    uko hapa kuponya.
  • 0:37 - 0:47
    Upone kwa jina la Yesu!
  • 0:48 - 0:55
    Jina langu ni Ivan na ninaishi hapa Norway.
  • 0:55 - 0:59
    Kwa asili, mimi ni natokea Uganda.
  • 0:59 - 1:07
    Nilikuwa na maradhi ambayo
    yalinitoa kwenye nafasi yangu.
  • 1:07 - 1:10
    Ilibidi hata nichukue wakati wa kupumzika kazini.
  • 1:10 - 1:17
    Na ugonjwa huo ulisababisha
    maumivu kwenye kifua changu,
  • 1:17 - 1:23
    ambapo nilipata maumivu makali.
  • 1:23 - 1:26
    Sikuweza kueleza
    yalikuwa yanatoka wapi.
  • 1:26 - 1:33
    yalikuwa makali sana kiasi kwamba
    sikuweza kufanya chochote.
  • 1:33 - 1:37
    Karibu miaka 15 iliyopita, nilikuwa na
    homa ya mapafu kali (acute pneumonia),
  • 1:37 - 1:41
    nikiwa bado nyumbani Uganda
    kabla sijahamia Norway.
  • 1:41 - 1:52
    Na ugonjwa huu ulikuwa mkali sana kwamba sehemu ya
    ganda la kushoto la pafu langu iliharibika
  • 1:52 - 1:56
    Nililazwa hospitalini kwa mwezi mmoja.
  • 1:56 - 1:59
    Na hata nilipotoka hospitalini,
  • 1:59 - 2:05
    Ilinibidi niwe na kipindi cha kusubiri kupona kidigo kidogo
    kwa takriban mwezi mmoja. Ilikuwa mbaya sana.
  • 2:05 - 2:11
    Kwa hivyo nilipopata maumivu hayo,
    nilianza kiyahusisha na kisa hicho,
  • 2:11 - 2:17
    kwamba pengine inaweza kuwa
    nimonia ilikuwa inajidhihirisha tena.
  • 2:17 - 2:21
    Wakati maumivu yalipoendelea, niliamua ...
  • 2:21 - 2:26
    Kumbuka, wakati huo nilikuwa
    nimeacha kufanya kazi kwa sababu sikuweza kugeuka.
  • 2:26 - 2:34
    Hata lilipokuja suala la kutembea, kupiga hatua, nilihisi maumivu makali ndani.
  • 2:34 - 2:40
    Hata wakati wowote nilipokuwa nimelala,
    nikigeuka kutoka upande mmoja hadi mwingine,
  • 2:40 - 2:44
    ilikuwa shida, ilikuwa tatizo.
  • 2:44 - 2:48
    Kwa hiyo niliamua kuwasiliana na daktari wangu.
  • 2:48 - 2:53
    Alipokuwa akinichunguza,
    alijaribu kugusa eneo hilo
  • 2:53 - 2:58
    kwa sababu nilimwambia kuwa maumivu
    yalikuwa ndani ya kifua changu.
  • 2:58 - 2:59
    Yalikuwa makali sana.
  • 2:59 - 3:03
    Hata sikujua jinsi
    ya kumweleza maumivu yangu.
  • 3:03 - 3:09
    Kwa hivyo kisa hicho, nadhani, kikawa
    kingumu sana kwake.
  • 3:09 - 3:16
    Na kisha akaamua kunielekeza kwenye
    hospitali kubwa zaidi kwa huduma za ushauri.
  • 3:16 - 3:23
    Nikaenda na kufika pale wakanipa
    mapokeo ya dharura.
  • 3:23 - 3:28
    Kwa hiyo nilipata timu ya madaktari na wauguzi.
    Walikuja na kunichunguza.
  • 3:28 - 3:31
    Walinihoji na
    nikawaambia kila kitu.
  • 3:31 - 3:39
    Na kisha wakasema wataenda kuchukua X-ray na kisha kufanya uchunguzi(scan) wa moyo wangu.
  • 3:39 - 3:46
    Kwa hiyo walikuja na kunichukua ndani na kuchukua
    X-ray mbili za sehemu ya kifua changu.
  • 3:46 - 3:52
    Walichukua sampuli za damu kutoka kwangu,
    kwa kweli sampuli nyingi za damu,
  • 3:52 - 3:55
    kwa sababu walilazimika kufanya majaribio kadhaa.
  • 3:55 - 4:02
    Kilichonishangaza ni, baada ya kuchunguza
    mfululizo wa majaribio hayo yote waliyofanya,
  • 4:02 - 4:10
    waligundua kuwa hakuna kitu - kila kitu kiligeuka kuwa hasi.
  • 4:10 - 4:14
    Jumamosi ijayo tungekuwa
    na
  • 4:14 - 4:19
    tukio la mhadhara la 'Acha Mioyo Iamke'
    nchini Uingereza.
  • 4:19 - 4:24
    Nilikuwa na bahati ya kupokea
    kiungo ili nijiunge mtandaoni,
  • 4:24 - 4:27
    kwa hivyo nilikuwa nikitarajia.
  • 4:27 - 4:31
    Na moyoni mwangu nilikuwa na imani.
  • 4:31 - 4:39
    Nilifikiria, kama kisa hiki kimekuwa,
  • 4:39 - 4:45
    kigumu sana kwa mwanadamu kufasiri,
    nitakileta mbele za Mungu.
  • 4:45 - 4:48
    Najua lisilowezekana kwa mwanadamu
    linawezekana kwa Mungu.
  • 4:48 - 4:53
    Jumamosi ilifika na nikajiunga.
    Nilitarajia.
  • 4:53 - 5:03
    Nilijua kisa hiki kimekaidi maarifa ya matibabu
    na hakitakaidi uwezo wa Mungu.
  • 5:03 - 5:09
    Kwa hiyo maombi yakaanza na
    tukasikiliza shuhuda.
  • 5:09 - 5:15
    Kisha mtu wa Mungu alipokuja,
    alipokuwa akiwaombea watu,
  • 5:15 - 5:20
    Nilianza kuona nguvu za Mungu
    zikiwagusa watu.
  • 5:20 - 5:22
    Watu walikuwa wakijidhihirisha.
  • 5:22 - 5:27
    Kweli Mungu alikuwa anatembea kwa nguvu
    pale ukumbini.
  • 5:27 - 5:32
    Na alipokuwa akiwaombea watu,
    maombi yangu yalikuwa moja tu.
  • 5:32 - 5:38
    Niliendelea kusema moyoni mwangu, 'Bwana, unapowagusa
    wengine, usinipite.
  • 5:38 - 5:43
    Unapowatembelea wengine, tafadhali Bwana,
    usinipite.
  • 5:43 - 5:51
    niko hapa. Najua umbali sio kizuizi kwa nguvu zako. Unaweza kunigusa.'
  • 5:51 - 5:56
    Lakini mnajua, watu wa Mungu,
    nilichogundua ni
  • 5:56 - 6:02
    kwamba hata kabla ibada
    haijafikia hatua
  • 6:02 - 6:08
    ambapo mtu wa Mungu alijitokeza kuwaombea
    watazamaji waliokuwa wameunganishwa mtandaoni,
  • 6:08 - 6:14
    Niligundua kuwa maumivu yalikuwa
    yametoweka yenyewe.
  • 6:14 - 6:16
    Ndugu Chris alipokuja
    kuwaombea watazamaji,
  • 6:16 - 6:21
    na akasema kwamba watu
    wanapaswa kugusa sehemu hizo
  • 6:21 - 6:29
    ambapo walikuwa na maumivu au usumbufu,
    wakati huo kulikuwa na maumivu kidogo sana
  • 6:29 - 6:35
    nami nikagusa na nadhani hiyo
    ilitia muhuri uponyaji wote kwa ajili yangu.
  • 6:35 - 6:42
    Na baada ya hapo, nilihisi vizuri.
    Usiku huo, nililala vizuri.
  • 6:42 - 6:45
    Siku iliyofuata ningeweza
    kufanya mambo ambayo sikuweza kufanya.
  • 6:45 - 6:49
    Ningeweza kuinama.
    Ningeweza kugeuka.
  • 6:49 - 6:53
    Siku ya Jumatatu, nilirudi kazini
    na nilikuwa sawa.
  • 6:53 - 7:00
    Nilirejeshwa kikamilifu. Utukufu ni kwa Mungu.
    Sasa niko huru kabisa!
  • 7:00 - 7:05
    Kama unavyoona,
    sikuweza kusonga kama hii.
  • 7:05 - 7:07
    Sikuweza kufanya hivi kwa sababu
  • 7:07 - 7:11
    maumivu yangekuwa makali sana
    na kupenya hadi kifuani mwangu.
  • 7:11 - 7:14
    Sikuweza kusimama.
  • 7:14 - 7:18
    Sasa naweza kuruka.
  • 7:18 - 7:22
    Kwa hiyo niko huru kabisa
    kwa utukufu wa Mungu!
  • 7:22 - 7:25
    Je, ulisikia maumivu yoyote wakati wa kufanya mazoezi?
  • 7:25 - 7:30
    Hapana, hata kidogo. Niko huru kwa utukufu wa Mungu.
  • 7:30 - 7:35
    Tafadhali, sasa endelea na ushirikishe
    neno lako zuri la ushauri kwa watazamaji.
  • 7:35 - 7:42
    Tunahitaji kumtegemea Mungu,
    na tunahitaji kutambua
  • 7:42 - 7:46
    ya kwamba yasiyowezekana kwa mwanadamu
    yanawezekana kwa Mungu.
  • 7:46 - 7:51
    Hali yoyote ambayo inaweza kukujia,
    usivunjike moyo.
  • 7:51 - 7:55
    Jua kuwa lililo gumu kwako,
  • 7:55 - 8:00
    lisilowezekana kwa mwanadamu,
    kwa Mungu linawezekana.
  • 8:00 - 8:07
    Mungu anapendezwa nasi kumkazia macho, kumaanisha kumtumaini.
  • 8:07 - 8:13
    Kwa maana Maandiko Matakatifu yasemavyo:
    'Bila imani hatuwezi kumpendeza Mungu.'
  • 8:13 - 8:19
    Mungu anaheshimiwa tunapomtegemea
    , tunapomtumaini.
  • 8:19 - 8:25
    Kwa hivyo ushauri wangu ni, bila kujali hali,
    haijalishi mazingira,
  • 8:25 - 8:27
    hakuna lisilowezekana
    kwa Mungu.
  • 8:27 - 8:30
    Tumtegemee Mungu.
    Tumtumaini Yeye.
  • 8:30 - 8:36
    Na tunapomtumaini Yeye,
    atatujia.
  • 8:36 - 8:41
    Atatugusa, Atagusa
    hali zetu na tutafanywa kuwa wakamilifu.
Title:
Maombi nchini Uingereza; Muujiza nchini NORWAY!
Description:

Umbali sio kizuizi kwa nguvu za Mungu! Ivan alikuwa Norway alipojiunga na 'Acha Mioyo Iamke' - tukio la kwanza la umma la TV Ya Moyo Wa Mungu (God's Heart TV) nchini Uingereza - kupitia Zoom. Ndugu Chris alipokuwa akihudumia wengine maombi, alipokea uponyaji wake mwenyewe kutokana na maumivu makali ya kifua ambayo yalikuwa yamekaidi ujuzi wa kitiba. Kweli, kwa MUNGU hakuna lisilowezekana.

Ili kupokea maombi bila malipo kutoka kwa Ndugu Chris kupitia Zoom, wasilisha ombi lako la maombi hapa - https://www.godsheart.tv/zoom

➡️ Pata Kutiwa Moyo Kila Siku kwenye WhatsApp - https://godsheart.tv/whatsapp/
➡️ Kuwa Mshirika wa TV wa Moyo wa Mungu - https://godsheart.tv/partnership
➡️ Habari kuhusu Maombi ya Pamoja - https://godsheart.tv/interactive-prayer/
➡️ Jitolee kama Mtafsiri wa TV ya Moyo wa Mungu - https://godsheart.tv/translate/
➡️ Shirikisha ushuhuda wako - https://godsheart.tv/testimony
➡️ Jiunge na Ibada yetu ya Maombi ya Moja kwa Moja Jumamosi ya kwanza ya kila mwezi - https://www.youtube.com/godshearttv/live

more » « less
Video Language:
English
Team:
God's Heart TV
Duration:
09:12

Swahili subtitles

Revisions Compare revisions