< Return to Video

Adding fractions with unlike denominators

  • 0:00 - 0:03
    Hebu tuseme kwamba
    tuna sehemu 9/10,
  • 0:03 - 0:08
    na mimi nataka kuongeza sehemu 1/6.
  • 0:10 - 0:13
    Hii itakuwa sawa na nini?
  • 0:14 - 0:15
    Hivyo wakati unaangalia hii, unaweza kusema,
  • 0:15 - 0:17
    "Oh, nina asili tofauti hapa.
  • 0:17 - 0:19
    Siyo kawaida kufanya hesabu kama hizi. "
  • 0:19 - 0:21
    Na njia sahihi ya kufanya hii ni
  • 0:21 - 0:24
    kuanza kwa kutafuta kigawe cha shirika,
  • 0:24 - 0:26
    kubadili sehemu zote hizi mbili kuwa
  • 0:26 - 0:29
    sehemu zenye asili sawa.
  • 0:29 - 0:30
    Hivyo ni jinsi gani unaweza kupata asili ya shirika?
  • 0:30 - 0:32
    Naam, asili ya shirika itakuwa ni
  • 0:32 - 0:36
    kigawe cha shirika cha asili 10 na 6.
  • 0:36 - 0:39
    Hivyo kigawe cha shirika cha 10 na 6 ni kipi?
  • 0:39 - 0:41
    Na ni rahisi kutafuta kigawe kidogo cha shirika,
  • 0:41 - 0:44
    na njia nzuri ya kufanya hii ni kuanza na
  • 0:44 - 0:47
    asili kubwa, 10, na ujiulize, je 10 inagawanyika kwa 6?
  • 0:48 - 0:51
    Hapana. Je 20 inagawanyika kwa 6?
  • 0:52 - 0:56
    Hapana. Je 30 inagawanyika kwa 6?
  • 0:56 - 0:58
    Hapa tulikuwa tunaangalia vigawe vya 10
  • 0:58 - 1:00
    na ni kigawe gani kidogo cha 10
  • 1:00 - 1:04
    ambacho kinagawanyika kwa 6? Na hiko kitakuwa ni 30.
  • 1:04 - 1:06
    Hivyo naweza kuziandika upya hizi sehemu
  • 1:06 - 1:08
    kama namba fulani juu ya 30.
  • 1:08 - 1:10
    Hivyo 9 juu ya 10. Nitaandika vipi hiyo
  • 1:10 - 1:12
    kama kitu fulani juu ya 30? Nitazidisha
  • 1:12 - 1:16
    asili kwa 3.
  • 1:17 - 1:20
    Hivyo nimezidisha asili kwa 3.
  • 1:20 - 1:22
    Kwa hiyo kama sihitaji kubadili thamani ya sehemu ,
  • 1:22 - 1:24
    ninatakiwa kufanya vivyo hivyo kwa kiasi.
  • 1:24 - 1:26
    Nitazidisha kiasi kwa tatu
  • 1:27 - 1:30
    kwa sababu nilizidisha kiasi kwa tatu
  • 1:30 - 1:31
    na asili kwa tatu, na hiyo haitabadili
  • 1:31 - 1:33
    thamani ya sehemu.
  • 1:33 - 1:36
    Hivyo sita mara tatu ni 27.
  • 1:36 - 1:39
    Na hivyo, 9/10 na 27/30
  • 1:39 - 1:41
    zinawakilisha kitu sawa.
  • 1:41 - 1:44
    Nimeandika hii ikiwa na asili 30,
  • 1:44 - 1:46
    na pia naweza kuandika 1/6
  • 1:46 - 1:49
    ikiwa na asili 30. Hebu tufanye hiyo.
  • 1:49 - 1:52
    Hivyo 1/6 ni nini juu ya 30?
  • 1:52 - 1:53
    Nakushauri usimamishe hii video
  • 1:53 - 1:54
    na ujaribu kufanya hiyo.
  • 1:54 - 1:56
    Hivyo tutafanya nini kutoka 6 mpaka 30?
  • 1:56 - 1:59
    Tunatakiwa kuzidisha kwa tano.
  • 2:00 - 2:02
    hivyo kama tukizidisha asili kwa tano,
  • 2:02 - 2:05
    pia tunatakiwa kuzidisha kiasi kwa tano,
  • 2:05 - 2:10
    hivyo moja mara tano ni tano.
  • 2:11 - 2:14
    Hivyo 9/10 ni sawa na 27/30,
  • 2:14 - 2:16
    na 1/6 ni sawa na 5/30.
  • 2:16 - 2:20
    Na sasa tunaweza kujumlisha
  • 2:20 - 2:22
    na iko wazi.
  • 2:22 - 2:23
    Tuna namba fulani juu ya 30,
  • 2:23 - 2:25
    na tunajumlisha namba fulani juu ya 30,
  • 2:25 - 2:30
    hivyo 27/30 + 5/30, hiyo itakuwa sawa na
  • 2:30 - 2:35
    27 jumlisha 5,
  • 2:35 - 2:40
    27 + 5,
  • 2:41 - 2:44
    ambayo
  • 2:44 - 2:47
    itakuwa sawa na 32/30.
  • 2:47 - 2:51
    32 juu ya 30, na
  • 2:51 - 2:54
    kama tukitaka, tunaweza kurahisisha hii sehemu.
  • 2:55 - 2:57
    Tuna kigawo cha 32 na 30,
  • 2:57 - 3:00
    zote zinagawanyika kwa 2.
  • 3:00 - 3:04
    Hivyo kama tukigawanya kiasi na asili kwa 2,
  • 3:04 - 3:06
    kiasi gawa kwa mbili ni 16,
  • 3:06 - 3:09
    asili gawa kwa 2 ni 15.
  • 3:09 - 3:13
    Hivyo, hii ni sawa na 16/15, na kama tukitaka
  • 3:13 - 3:16
    kuandika hii kama namba mchanganyiko, 15 inaingia mara moja katika 16
  • 3:16 - 3:18
    na baki moja.
  • 3:18 - 3:20
    Hivyo hii ni sawa na 1 1/15.
  • 3:21 - 3:23
    Hebu tufanye hesabu nyingine.
  • 3:23 - 3:27
    Hebu tuseme tunahitaji kujumlisha
  • 3:27 - 3:32
    1/2 na
  • 3:32 - 3:37
    11/12.
  • 3:37 - 3:38
    Nakushauri usimamishe video
  • 3:38 - 3:41
    na ujaribu kufanya hii.
  • 3:41 - 3:43
    Kama tulivyoona mwanzo, tunatakiwa kutafuta
  • 3:43 - 3:44
    kigawe cha shirika.
  • 3:44 - 3:45
    Kama hizi zina asili sawa,
  • 3:45 - 3:46
    tunaweza kuzijumlisha moja kwa moja,
  • 3:46 - 3:49
    lakini tunatakiwa kutafuta asili ya shirika
  • 3:49 - 3:50
    kwa sababu haziko sawa.
  • 3:51 - 3:53
    Tunachotakiwa kutafuta ni rahisi,
  • 3:53 - 3:56
    kigawe cha shirika cha 2 na12,
  • 3:56 - 3:58
    na ni vizuri kutafuta kigawe kidogo cha shirika cha 2 na 12,
  • 3:58 - 4:00
    na kama tulivyofanya mwanzoni, hebu tuanze na kubwa
  • 4:00 - 4:02
    kati ya hizi mbili, ambayo ni 12.
  • 4:02 - 4:05
    Na sasa tunachukua 12 mara moja ambayo ni 12,
  • 4:05 - 4:08
    na hivyo tunaweza kuona kuwa ni kigawe kidogo cha 12.
  • 4:08 - 4:11
    Na je hiyo inagawanyika kwa mbili? Ndiyo, hakika.
  • 4:11 - 4:13
    12 inagawanyika kwa mbili.
  • 4:13 - 4:16
    Hivyo 12 ni kigawe kidogo cha shirika cha mbili na 12,
  • 4:16 - 4:17
    tunaweza kuandika hizi sehemu mbili
  • 4:17 - 4:19
    kama kitu fulani juu ya 12.
  • 4:19 - 4:22
    Hiyo 1/2 ni nini juu ya 12?
  • 4:22 - 4:24
    Kutoka mbili mpaka 12, utazidisha kwa sita,
  • 4:24 - 4:27
    pia tutazidisha kiasi kwa sita.
  • 4:27 - 4:31
    Sasa tunaona 1/2, na 6/12, hizi ni kitu sawa.
  • 4:31 - 4:34
    Moja ni nusu ya mbili, sita ni nusu ya 12.
  • 4:35 - 4:38
    Na tutaandikaje 11/12 kama kitu fulani juu ya 12?
  • 4:38 - 4:41
    Hii tayari imekwisha andikwa juu ya 12,
  • 4:41 - 4:43
    11/12 tayari ina 12 kama asili,
  • 4:43 - 4:45
    hivyo hatuna sababu ya kubadili hiyo.
  • 4:46 - 4:48
    11/12, sasa tuko tayari kujumlisha.
  • 4:49 - 4:51
    Hivyo hii itakuwa sawa na sita,
  • 4:53 - 4:56
    hii itakuwa sawa na sita jumlisha 11,
  • 4:57 - 5:02
    sita jumlisha 11 juu ya 12.
  • 5:02 - 5:06
    Tuna 6/12 jumlisha 11/12,
  • 5:06 - 5:09
    itakuwa sita jumlisha 11 juu ya 12,
  • 5:11 - 5:15
    ambayo itakuwa sawa, na sita jumlisha 11 ni 17/12.
  • 5:15 - 5:17
    Kama tukitaka kuandika hii kama namba mchanganyiko,
  • 5:17 - 5:19
    12 inaingia mara moja katika 17
  • 5:19 - 5:24
    na baki tano, hivyo ni 1 5/12.
  • 5:25 - 5:26
    Hebu tufanye nyingine kama hii.
  • 5:26 - 5:29
    Hii ni tofauti kidogo.
  • 5:29 - 5:31
    Hebu tuseme tunataka kujumlisha,
  • 5:32 - 5:36
    3/4 na,
  • 5:37 - 5:41
    1/5.
  • 5:41 - 5:44
    Na moja juu ya tano.
  • 5:44 - 5:45
    Hii itakuwa sawa na nini?
  • 5:45 - 5:46
    Na kwa mara nyingine tena, simamisha hii video na
  • 5:46 - 5:48
    ujaribu kufanya mwenyewe.
  • 5:48 - 5:49
    Tuna asili tofauti,
  • 5:49 - 5:52
    na tunataka kuandika hizi
  • 5:52 - 5:53
    zikiwa na asili sawa,
  • 5:53 - 5:55
    hivyo tunatakiwa kutafuta kigawe cha shirika,
  • 5:55 - 5:57
    ni vizuri kiwe kigawe kidogo cha shirika.
  • 5:57 - 6:00
    Je, kipi ni kigawe kidogo cha shirika cha nne na tano?
  • 6:01 - 6:02
    Hebu tuanze na namba kubwa,
  • 6:02 - 6:05
    na tuangalie vigawe vyake
  • 6:05 - 6:07
    mpaka tutakapopata kigawe kitakacho gawanyika kwa nne.
  • 6:07 - 6:10
    Hivyo tano haigawanyiki kwa nne.
  • 6:10 - 6:14
    10 haigawanyiki kwa nne, bila kubaki
  • 6:14 - 6:15
    ndio kitu tunachoangalia zaidi.
  • 6:15 - 6:17
    15 haigawanyiki kwa nne bila kubaki.
  • 6:17 - 6:21
    20 inagawanyika kwa nne, hiyo ni sawa na tano mara nne.
  • 6:21 - 6:24
    Kigawe ni 20. Hivyo tunachotakiwa kufanya ni kuandika
  • 6:24 - 6:27
    sehemu zote mbili zikiwa na asili 20,
  • 6:27 - 6:29
    au 20 kama asili.
  • 6:29 - 6:32
    Hivyo tunaweza kuandika 3/4 kama kitu fulani juu ya 20.
  • 6:33 - 6:35
    Hivyo kutoka nne mpaka 20 katika asili,
  • 6:35 - 6:37
    tunazidisha kwa tano.
  • 6:37 - 6:38
    Pia tutazidisha katika kiasi .
  • 6:38 - 6:41
    Tunazidisha tatu mara tano kupata 15.
  • 6:41 - 6:44
    Tulichofanya ili kupata 20 ni kuzidisha kwa tano.
  • 6:44 - 6:46
    Pia tunatakiwa kufanya sawa kwa kiasi,
  • 6:46 - 6:48
    tatu mara tano ni 15.
  • 6:48 - 6:53
    3/4 ni sawa na 15/20.
  • 6:53 - 6:55
    1/5. Itakuwa sawa na nini juu ya 20?
  • 6:55 - 6:58
    Hivyo kutoka tano mpaka 20, unatakiwa kuzidisha kwa nne.
  • 6:58 - 7:00
    Pia tunatakiwa kufanya sawa na kwa kiasi.
  • 7:00 - 7:04
    Tunatakiwa kuzidisha kiasi kwa nne ili kupata 4/20.
  • 7:04 - 7:07
    Hivyo nimeandika hii badala ya 3/4 jumlisha 1/5,
  • 7:07 - 7:11
    sasa tumeandika 15/20 jumlisha 4/20.
  • 7:11 - 7:13
    Na hiyo itakuwa sawa na nini?
  • 7:13 - 7:18
    Hiyo itakuwa sawa na 15 jumlisha nne ambayo ni 19/20.
  • 7:18 - 7:22
    19/20, na tumemaliza.
Title:
Adding fractions with unlike denominators
Description:

more » « less
Video Language:
English
Team:
Khan Academy
Duration:
07:24

Swahili subtitles

Revisions