< Return to Video

How to solve one-step equations with fractions and decimals | 6th grade | Khan Academy

  • 0:00 - 0:02
    Hebu tufanye maswali ya
  • 0:02 - 0:04
    kukokotoa milinganyo.
  • 0:04 - 0:08
    Tuchukulie tuna mlinganyo huu, 1/3 jumlisha A
  • 0:08 - 0:11
    ni sawa na 5/3.
  • 0:11 - 0:14
    Je, thamani ya A ni ngapi kwenye mlinganyo?
  • 0:14 - 0:18
    Kama nina 1/3 jumlisha A, je A inatakiwa kuwa ngapi
  • 0:18 - 0:23
    ili tukiijumlisha kwa 1/3 iwe sawa na 5/3?
  • 0:24 - 0:27
    Kuna njia nyingi za kufanya hii,
  • 0:27 - 0:30
    na hiki ni kitu cha kufurahisha kuhusu mlinganyo
  • 0:30 - 0:33
    na hakuna njia moja ya kukokotoa.
  • 0:33 - 0:35
    Hivyo ngoja nifikirie,
  • 0:35 - 0:36
    njia nyepesi ya kutumia.
  • 0:36 - 0:38
    Na kabla sijafanya chochote, unaweza
  • 0:38 - 0:41
    kusubirisha video, na ufanye mwenyewe.
  • 0:41 - 0:46
    Hivyo nachotakiwa ni kuwa na A
  • 0:46 - 0:48
    upande mmoja wa mlinganyo.
  • 0:48 - 0:50
    Kwa kuwa A ipo tayari upande wa kushoto,
  • 0:50 - 0:51
    tuone kama nitaweza kuendelea kuiweka upande wa kushoto,
  • 0:51 - 0:54
    hivyo naiondoa 1/3.
  • 0:54 - 0:56
    Vizuri, njia rahisi ya kuiondoa
  • 0:56 - 0:59
    hii 1/3 ni kutoa 1/3 kutoka upande wa
  • 0:59 - 1:01
    kushoto wa mlinganyo.
  • 1:01 - 1:03
    Siwezi kutoa
  • 1:03 - 1:04
    upande wa kushoto wa mlinganyo peke yake.
  • 1:04 - 1:07
    Kama 1/3 jumlisha A ni sawa na 5/3,
  • 1:07 - 1:10
    na kama nikitoa 1/3 kutoka upande wa kushoto tu,
  • 1:10 - 1:12
    hivyo haiwezi kuwa sawa.
  • 1:12 - 1:14
    Hivyo upande huu utakuwa pungufu ya 1/3,
  • 1:14 - 1:15
    endapo upande huu hautobadilika.
  • 1:15 - 1:17
    Hivyo basi upande wa kushoto utakuwa
  • 1:17 - 1:18
    pungufu ya 5/3.
  • 1:18 - 1:21
    Kwa hiyo ili kupata usawa, nitakachokifanya
  • 1:21 - 1:24
    upande wa kushoto nitakifanya upande wa kulia pia.
  • 1:24 - 1:27
    Hivyo nitatoa 1/3 pande zote.
  • 1:27 - 1:30
    Na kama nikifanya hivyo, upande wa kushoto,
  • 1:30 - 1:32
    1/3 toa 1/3, ndiyo maana
  • 1:32 - 1:35
    nimetoa 1/3 ili kuondoa 1/3,
  • 1:35 - 1:40
    na nimebakiwa na A ni sawa na 5/3 toa 1/3,
  • 1:42 - 1:46
    5/3 toa 1/3,
  • 1:46 - 1:50
    toa 1/3 , tutapata ngapi?
  • 1:50 - 1:53
    Nina tano ya kitu hapa, kwenye hili swali nina 5/3,
  • 1:53 - 1:56
    ninatoa kwa 1/3.
  • 1:56 - 1:59
    Hivyo nitabakiwa na 4/3.
  • 1:59 - 2:04
    Hivyo nitaandika A ni sawa na 4/3.
  • 2:06 - 2:07
    Unaweza kuhakikisha kama ni sahihi.
  • 2:07 - 2:12
    1/3 jumlisha 4/3 ni sawa na 5/3.
  • 2:13 - 2:15
    Hebu tufanye mfano mwingine.
  • 2:15 - 2:20
    Tuchukulie tuna mlinganyo huu, K toa nane
  • 2:21 - 2:25
    ni sawa na 11.8.
  • 2:25 - 2:28
    Kwa mara nyingine, natafuta thamani ya K.
  • 2:28 - 2:29
    Nina K upande wa kushoto.
  • 2:29 - 2:33
    Sihitaji kuwa na hii, toa nane hapa.
  • 2:33 - 2:36
    Hivyo ili kuondoa hii nane, hivyo tuongeze nane
  • 2:36 - 2:37
    upande wa kushoto.
  • 2:37 - 2:38
    Hivyo, kama nafanya hivi upande wa kushoto,
  • 2:38 - 2:40
    nitafanya hivyohivyo upande wa kulia.
  • 2:40 - 2:43
    Hivyo tunaongeza nane pande zote.
  • 2:43 - 2:46
    Upande wa kushoto, unatoa nane
  • 2:46 - 2:46
    na pia unajumlisha nane.
  • 2:46 - 2:48
    Hii inaisha,
  • 2:48 - 2:50
    na unabakiwa na K.
  • 2:50 - 2:53
    Na upande wa kulia, 11.8 jumlisha nane.
  • 2:53 - 2:58
    Vizuri, 11 jumlisha nane ni 19, itakuwa 19.8.
  • 2:59 - 3:01
    Na tumemaliza,
  • 3:01 - 3:03
    Unaweza kuhakikisha kama umepata jibu sahihi.
  • 3:03 - 3:08
    19.8 toa nane ni 11.8.
  • 3:08 - 3:11
    Hebu tufanye nyingine, hii inavutia.
  • 3:11 - 3:16
    Sawa, tuchukulie nina 5/13 ni sawa na
  • 3:16 - 3:20
    T toa 6/13.
  • 3:20 - 3:22
    Vizuri, hii inavutia kwa sababu sasa nina mtajo
  • 3:22 - 3:24
    upande wa kulia.
  • 3:24 - 3:25
    Hivyo naiacha hapa.
  • 3:25 - 3:28
    Tuone kama tunaweza kutafuta thamani ya T kwa kuondoa
  • 3:28 - 3:29
    namba yoyote upande wa kulia.
  • 3:29 - 3:34
    Na kama tulivyofanya awali, kama natoa 6/13,
  • 3:34 - 3:36
    kwa nini nisiijumlishe?
  • 3:36 - 3:37
    Kwa nini nisijumlishe 6/13?
  • 3:37 - 3:39
    Siwezi kufanya hivyo upande wa kushoto.
  • 3:39 - 3:41
    Hizi pande mbili hazitakuwa sawa,
  • 3:41 - 3:43
    nitafanya hivyo upande wa kulia kama ninataka
  • 3:43 - 3:45
    kupata usawa.
  • 3:45 - 3:47
    Hivyo nini kitatokea?
  • 3:47 - 3:48
    Nini kitatokea?
  • 3:48 - 3:50
    Upande wa kushoto nina
  • 3:50 - 3:52
    ngoja niache nafasi kidogo,
  • 3:52 - 3:57
    nina 5/13 jumlisha 6/13,
  • 3:58 - 4:02
    jumlisha 6/13 ni sawa na ,
  • 4:02 - 4:04
    ni sawa na
  • 4:04 - 4:07
    Nilitoa 6/13, sasa najumlisha 6/13.
  • 4:07 - 4:09
    Hizi zitatupatia sifuri.
  • 4:09 - 4:13
    6/13 toa 6/13 inabaki sifuri, hivyo umebakiwa na T.
  • 4:13 - 4:14
    Hivyo T ni sawa na hii.
  • 4:14 - 4:17
    Kama nina 5/13 na najumlisha na hii 6/13,
  • 4:17 - 4:19
    Nitapata 11/13.
  • 4:19 - 4:24
    Hivyo hii itakuwa 11/13 ni sawa na T,
  • 4:24 - 4:25
    au naweza kuiandika kwa njia nyingine.
  • 4:25 - 4:30
    Naandika T ni sawa na 11/13.
Title:
How to solve one-step equations with fractions and decimals | 6th grade | Khan Academy
Description:

more » « less
Video Language:
English
Team:
Khan Academy
Duration:
04:32

Swahili subtitles

Revisions